Waziri wa Elimu, kuna shule zinawachapa viboko wanafunzi kwa kukosa mahitaji ya shule, watoto wanahusikaje?

Waziri wa Elimu, kuna shule zinawachapa viboko wanafunzi kwa kukosa mahitaji ya shule, watoto wanahusikaje?

kipara kipya

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2016
Posts
18,833
Reaction score
23,276
Waziri wa elimu hebu litupie macho hili la walimu kuwaadhibu wanafunzi kukosa michango na mahitaji ya shule,kama hao watoto ndio watafutaji wa hayo mahitaji.

Kwanini usimuite mzazi ukamuadhibu kwa hilo kosa la kutomtimizia mtoto wake mahitaji, unamchapa viboko mtoto ana kosa gani?

Pili hiyo michango ni ya nini, nasi tunaambiwa elimu ni bure. Hao waalimu wa sayansi wa kujitolea kwanini wasiajiriwe huko.

Kwa kweli mnazingua watoto mwisho wa siku wakichoka viboko, watoto kiume wanaingia mitini kwenda kuvuta ngada na wakike wanakwenda kupewa mimba hebu kuweni makini kidogo kuwaelimisha na kuwasimamia hao walimu wenu wahuni.

Tunazalisha taifa la namna gani 2025 sio mbali mjue!
 
Upo sahihi kwakua yeye hata ukimchapa kama mimi mzazi sina haitasaidia ni bora hata tuitwe wazazi tuwe tunachezea bakora ili tukomae kutafuta hayo mahitaji.

Kabla hatujaenda mihangaikoni tunapitia shule tunakula bakora mbili na wakati tunarudi mihangaikoni tunapitia kula mbili tena au tunaelekezwa nyumbani kwa mwalimu tuwe tunazifuata bakora huko nyumbani kwake.
 
Kwahiyo kwa akili zako unataka waitwe wazazi ndo wa chapwe? Kila mbuzi ina kula kwa ulefu wa kamba yake. Kwanini ukubali kwenda shule bila mahitaji mgomee mzazi ili akulete mwenyewe, wazazi wengi kuwalazimisha kufika shule ni vigumu paka uchape mwanae ndo afike. Usione hivo kwa juju shule za sarikali ni ngumu kuendesha.
 
Hiv kwann serikali isitoe tenda kweny viwanda vya nguo washone uniform za wanafunzi nchi nzima na wazigawe bure!
 
Kwahiyo kwa akili zako unataka waitwe wazazi ndo wa chapwe? Kila mbuzi ina kula kwa ulefu wa kamba yake......kwanini ukubali kwenda shule bila mahitaji mgomee mzazi ili akulete mwenyewe, wazazi wengi kuwalazimisha kufika shule ni vigumu paka uchape mwanae ndo afike.........usione hivo kwa juju shule za sarikali ni ngumu kuendesha.
Majibu yanaonyesha wewe ni mwalimu kama wizara haitawakomesha subiri kila mmoja achukue hatua yake anayoijua!
 
Majibu yanaonyesha wewe ni mwalimu kama wizara haitawakomesha subiri kila mmoja achukue hatua yake anayoijua!
Mzazi analeta mtoto hata bila sare unategemea mimi ni mchekee huyu mtoto hajui kwamba shule wanavaa sare.......paka umchape ndo akili zinarudi ajue shule sio msibani.
 
Ila bongo n hatari

Nina kabinti kangu kameanza darasa la kwanza shule zetu hz za umma hapa dsm

Kila siku akirud nyumban ananiambia ticha kawaagiza wabebe tsh mia tano ya kununua chocolate za mwalimu na wasipobeba anawachapa

Nilipofuatilia n kwel mwl anauza vitu hvyo darasan

Tunasomesha shule za serikal n vile hatuna uwezo TU lakn huko changamoto n nyingi

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Wanahisi wanafunzi wanapewa pesa za ada na hawafikishi mahali husika au kuwakomesha tu
 
Majibu yanaonyesha wewe ni mwalimu kama wizara haitawakomesha subiri kila mmoja achukue hatua yake anayoijua!
Hao walimu bado wanawadekeza sana. Ilitakiwa wawaite na nyinyi wazazi, halafu wawatandike viboko mbele ya hao watoto wenu.

Yaani tupo kwenye karne ya 21, bado mnataka vitu vya bure bure tu! Mnazaliana kama simbilisi, halafu watoto wasome bure! Hovyo kabisa.
 
Hao walimu bado wanawadekeza sana. Ilitakiwa wawaite na nyinyi wazazi, halafu wawatandike viboko mbele ya hao watoto wenu.

Yaani tupo kwenye karne ya 21, bado mnataka vitu vya bure bure tu! Mnazaliana kama simbilisi, halafu watoto wasome bure! Hovyo kabisa.
Hapo watakuwa sahihi mkosaji ni mzazi si kumuadhibu mtoto!
 
Back
Top Bottom