Waziri wa Kusambaza Mitungi ya Gesi anataka kuwa Rais?

Waziri wa Kusambaza Mitungi ya Gesi anataka kuwa Rais?

Kuna kuongea ili uonekane unaongea, ila hakuna unachoongea. Makamba ni mnafiki wa hatari, ila mnaotumika na anayewatuma kumshambulia ndio vilaza, maana mnamuongezea mtaji wa kisiasa. Matatizo yote nchini, ila kamama kanapoteza muda kuwaza katarudi vipi uchaguzi ujao. Tuna nchi ya kipuuzi sana.
 
Makamba ni moja kati ya mambumbu wakubwa wanaoishi kwa nadharia ya uongo waliojiaminisha wenyewe kuwa ni wateule.
The guy is in denial with a belief that he is the chosen one.......

Tatizo la watu design ya Makamba ni kuhisi ni haki yao kuwa viongozi kwa vile tu baba zao walikuwa viongozi. Ni mfano dhahiri wa rich spoilt kids, ambao wakiahidiwa kitu na baba lazima wakipate. Sasa baba alipokuwa na relevance alimuahidi kuwa atakuwa raisi, mtoto nae akalibeba kuwa ni uhalisia.
Makamba kashindwa kutofautisha kukubalika na familia yake na kukubalika na taifa. Umaarufu pekee wa January ni kuwa mtoto wa Yusuf.
 
Huyu mtu badala ya kutafuta na kushawishi uwekezaji na usambazaji gesi ya kupikia majumbani maeneo ya mijini, anafanya comedy ya kupeleka mitungi ya gesi vijijini.......hivi anajiona kabisa yuko innovative kwenye hicho anachokifanya.​
 
Why apromoti Gesi ya Mtwara? Why asaidi TPDC kuwezesha Upatikanaji wa Funds ku malizia mradi wa kusambaza Gesi ya Kupikia katika jiji la Dar es salaam ambao umekwama kutokana na Kukosekana Fundings na mabomba tayari yapo mpaka maeneo ya Meeda Sinza?

Anampango gani kama Waziri mwenye Dhamana kuongeza matumizi ya Gesi yetu ili iweze kuongeza pato la taifa na kuwezesha patikana hela za kulipa China waliotupa mkopo na kutujengea Miundo mbinu ya Gesi- maana Deni linaongezeka kila kukicha na marejesho kizungu mkuti
Amekua dalali wa taifa gesi
 
Makamba ni moja kati ya mambumbu wakubwa wanaoishi kwa nadharia ya uongo waliojiaminisha wenyewe kuwa ni wateule...
Kwani huyo baba yake mwenyewe kafanya muujiza gani mpaka awe decreed kuwa na miliki ya national cake??

Ni jambo tu ambalo lipo kwenye fikra zao ambalo halina uhalisia wowote.
 
Ujue watu wanazani kuongea Kwa nguvu ndio akili but intelligent people hawaeleweki Hadi matokea makubwa yapatikane
 
Tanzania ndio nchi pekee ambayo viongozi wenye dhamana hulalamika na raia maskini nao hulalamika.
 
Hahahaaa!! Bora hata gesi kuliko kupiga pushapu
 
Why apromoti Gesi ya Mtwara? Why asaidi TPDC kuwezesha Upatikanaji wa Funds ku malizia mradi wa kusambaza Gesi ya Kupikia katika jiji la Dar es salaam ambao umekwama kutokana na Kukosekana Fundings na mabomba tayari yapo mpaka maeneo ya Meeda Sinza?

Anampango gani kama Waziri mwenye Dhamana kuongeza matumizi ya Gesi yetu ili iweze kuongeza pato la taifa na kuwezesha patikana hela za kulipa China waliotupa mkopo na kutujengea Miundo mbinu ya Gesi- maana Deni linaongezeka kila kukicha na marejesho kizungu mkuti
Kwahiyo, (kama ingekua ni kweli) kutokui promote gas ya Mtwara, kutokuiwezesha TPDC (iwasambazie gesi watu wa DSM), kunafanya jitihada za kuwapelekea gesi ya kupikia ya mitungi (LPG) wakazi wa Manyoni, Kibondo, Tandahimba, Kilosa, Chakechake, Rorya, Pangani na Monduli kuwa ni haramu ?
 
Shida kubwa Tanzania ina Vilaza wengi kuliko walio smart. So tatizo huwa inaogopesha mgombea Urais anapokuwa kilaza maana ana back up kubwa nyuma yake. Usifanye mchezo na vilaza. Ni kundi kubwa. Wanakuwa hatari zaidi wanapochagua viongozi
Okay nadhani nimekuelewa vizuri baada ya kusema sehemu ambayo tatizo kubwa lilipo.

Je mtu anaweza kuwa anafanya kosa endapo ataamua kujinufaisha na hili kundi kubwa la vilaza ?
 
Tatizo ni kuwapa nafasi watoto wa vigogo ambao hata wakiboronga kumuwajibisha mbaka babazao waombwe kwanza.

Hakuna kitu kibaya kama kumuongoza mtu ambae anajiamini kwamba hagusiki kirahisi.
Kwahiyo kwenye hili la kuhamasisha matumizi ya gesi kwa ajili ya kupikia kosa la waziri (ambaye ni mtoto wa kigogo kama ulivyodai) ni lipi ?

Au alitakiwa kuhamasisha matumizi ya kuni na mkaa (ikiwamo kupita na malori ya mkaa na kuni akigawia wananchi) ?
Nifafanulie mkuu.
 
Kwahiyo, (kama ingekua ni kweli) kutokui promote gas ya Mtwara, kutokuiwezesha TPDC (iwasambazie gesi watu wa DSM), kunafanya jitihada za kuwapelekea gesi ya kupikia ya mitungi (LPG) wakazi wa Manyoni, Kibondo, Tandahimba, Kilosa, Chakechake, Rorya, Pangani na Monduli kuwa ni haramu ?
Haramu kivipi?? Huko Vijijini Watanzania wanatakiwa wapelekewe systems za kuzalisha Bio Gas inayotokana na mabaki ya vyakula, Shambani n.k. Amewagawia Mitungi sawa je Ges ikiisha wana pesa ya kununua mipya?? Wakati ata elfu Tano za kuchangia watoto wao waliopo mashukeni ni shida kutokana na vipato vyao duni! Wewe mfano kule kijijini Kwenu Mama ako , Wajomba na Shangazi zao wana pesa za kununua mitungi ya Ges anayoisambaza Mweshimiwa??? Yetu macho ila yana Mwisho haya. Watanzania ipo Siku Mungu atawapigania nao watakaa kimiya
 

Attachments

  • 20220717_224949.jpg
    20220717_224949.jpg
    143.7 KB · Views: 3
  • 20220717_224936.jpg
    20220717_224936.jpg
    21.9 KB · Views: 3
Haramu kivipi?? Huko Vijijini Watanzania wanatakiwa wapelekewe systems za kuzalisha Bio Gas inayotokana na mabaki ya vyakula, Shambani n.k. Amewagawia Mitungi sawa je Ges ikiisha wana pesa ya kununua mipya?? Wakati ata elfu Tano za kuchangia watoto wao waliopo mashukeni ni shida kutokana na vipato vyao duni! Wewe mfano kule kijijini Kwenu Mama ako , Wajomba na Shangazi zao wana pesa za kununua mitungi ya Ges anayoisambaza Mweshimiwa??? Yetu macho ila yana Mwisho haya. Watanzania ipo Siku Mungu atawapigania nao watakaa kimiya
Kijijini kwetu tunatumia kuni na mkaa, ambavyo hatuvipati bure. Kwa kuendelea kutumia kuni na mkaa tunamaliza misitu, tukimaliza misitu mvua zinapungua, mvua zikipungua wakazi wa Daslam (na kwingineko) mnatangaziwa mgao wa maji na umeme. Mnaambiwa Kidatu, Mtera na Ruvu chini kina cha maji kimepungua.

Yeyote atakayetusaidia kutupa mitungi ya gesi bure, ili sisi tujaze gesi kwa pesa zetu, atakua ametusaidia, na ameisaidia misitu.
Kama kwa sasa serikali haitununulii mkaa na kuni, basi hakuna hoja katika kutaka serikali itununulie gesi pale mitungi itakapoishiwa gesi.

Suala lako la bayogesi ni jambo jema sana, tena ni jema mno (kama lilivyo la gesi ya kupikia), maana yote mawili yanapunguza utegemezi katika kuni na mkaa (misitu) kwa ajili ya kupikia.

Ni vema watu wa wizara ya nishati wakatekeleza haya yote mawili kulingana na mazingira (panapofaa kuweka bayogesi pawekwe, panapofaa gesi ya mitungi pawekwe, panapofaa gesi ya mabomba pawekwe, panapofaa vyote pawekwe).

Kwa namna yoyote ile, kuendelea kutegemea kuni na mkaa kama nishati kuu ya kupikia, kutatuletea machozi mengi (na milio mingi) hapo baadae.

Nimeacha mambo mengi sana kwenye andiko lako bila kuyajadili au kuyajibu, kwa sababu nimeona sio muhimu.
Mfano: Umesema wajomba na shangazi hawawezi kumudu kujaza gesi hivyo wasipelekewe mitungi, wakati huo huo umependekeza hao hao wapelekewe biogas schemes. Maintenance costs za biogas kwangu mimi ziko juu kuliko mtungi wa gesi, halafu pia gharama za kujenga biogas kwenye kaya 10 ziko juu kuliko kugawa mitungi kwenye hizo kaya 10.
 
Back
Top Bottom