Sitaki kusema Uhalisia wangu wa Kimaisha ( ambao Yeye ndiyo Kutwa ) anahangaika kutaka Kuujua na kumuonyesha kuwa sipo hivyo anavyonidhania Yeye au anavyodanganywa ( alivyodanganywa ) nimemtajia Mtu ambaye ananijua vyema, anaijua Familia yangu na mpaka nilipokulia ambaye ni JamiiForums Founder na Mtani wangu wa Kihaya
Maxence Melo bila kumsahau na Mdogo wangu wa damu kabisa
steveachi na Jirani yangu mkubwa katika Mji mwingine wa Familia Mbezi Beach aitwae
Bujibuji Simba Nyanaume na wengine Wachache ambao kwa Unyeti wa Nafasi zao nawahifadhi ila ID hii wanaijua na wananijua Physically.
Wengine hatujakuzwa katika Tabia za Kujitapa, Kujionyesha au Kujisifia hovyo ( sometimes ) Kiuwongo na Kweli hapa JamiiForums kama ambavyo Watu wengi wanapenda Kufanya hivyo bali tumekuzwa katika kuishi Maisha ya Kawaida na Kuridhika na kilichopo au na hali uliyonayo.
Na siyo kwamba nachukia Maisha ya Vijijini ( tena ndiyo huwa nayapenda ) kwani yananifanya niweze kujua zaidi Changamoto za Kwetu huko Butuguri ( Wilayani Butiama ) kwa Wazanaki ili basi na Mimi huko mbeleni Mwenyezi Mungu akina Baraka za Kiuchumi niweze Kuwasaidia na Kuwainua Ndugu zangu Wapendwa wa huko na hata wa Mkoa mzima wa Mara ( Musoma ) ambako ndiyo Asili yangu.
Wa Kijijini ( Mshamba ) nimeshamaliza Kufafanua nawasubiri wa Mjini Masaki na Oysterbay na Matajiri wa JamiiForums nzima waje na waendelee Kunidhihaki ili wafurahishe Nafsi zao huku Wakijidanganya na Wakidanganyana pia.
Natural Charm yangu inawatesa Wengi.