Waziri wa Ulinzi Dkt. Stergomena amtembelea Jenerali mstaafu Robert Mboma

Waziri wa Ulinzi Dkt. Stergomena amtembelea Jenerali mstaafu Robert Mboma

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
2.JPG
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Lawrence Tax amemtembelea Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali (Mstaafu) Robert Philemon Mboma nyumbani kwake Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kumjulia hali.

Waziri Stergomena amemtembelea Jenerali Mboma akiwa ni mwendelezo wa utaratibu wake aliojiwekea wa kuwatembelea na kufanya Mazungumzo na wastaafu hao tangu ateuliwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan.

Stergomena alianza utaratibu huo, kwa kumtembelea Mkuu wa Majeshi wa Kwanza, Jenerali (Mstaafu) Mirisho Sami Hagai Sarakikya, akifuatiwa na Jenerali (Mstaafu) David Bugozi Msuguri na Jenerali (Mstaafu) Davis Adolf Mwamnyange.

Wakuu wa Majeshi waliowahi kuliongoza Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) tangu kuanzishwa kwake Septemba 01, 1964 ni:

Jenerali (Mstaafu) Mirisho Sami Hagai Sarakikya (1964 - 1974)
Marehemu Jenerali Abdallah Twalipo (1974 – 1980)
Jenerali (Mstaafu) David Bugozi Msuguri (1980 - 1988)
Marehemu Jenerali Ernest Mwita Kyaro (1988 -1991)
Jenerali (Mstaafu) Robert Philemon Mboma (1991 - 2001)
Jenerali (Mstaafu) George Mwita Waitara (2001 - 2007)
Jenerali (Mstaafu) Davis Adolf Mwamunyange (2007 - 2017)
na Jenerali Venance Salvatory Mabeyo (2017 - sasa).

3.JPG

4.JPG
 
Kuna watu wamejaariwa uhai na afya.....mtu kastafu 2001,...hadi leo ana afya tele.....ukiwaona vijana na mabinti wadogo waliozaliwa 2001,wanajihusisha na matumizi ya mihadarati,pombe,ngono zembe na kujiuza unaona kabisa wamezeeka hata kufika robo ya miaka ya generali ni mtihani
 
Ila Mama pis kali kinoma,inaonekana anaomba ushauri maana hiyo wizara haihitaji waziri wala naibu katibu mkuu tu anatosha tena wamteue wao.
 
Kuna watu wamejaariwa uhai na afya.....mtu kastafu 2001,...hadi leo ana afya tele.....ukiwaona vijana na mabinti wadogo waliozaliwa 2001,wanajihusisha na matumizi ya mihadarati,pombe,ngono zembe na kujiuza unaona kabisa wamezeeka hata kufika robo ya miaka ya generali ni mtihani
Jenerali Msuguri ana miaka 101 sasa na bado anaonekana shupavu
 
Muhuni .mstaafu alimshawishi huyu Generali akachukue form ya Kugombea Ubunge kule Mbeya nae akaingiza Miguu na kama kawaida ya Wajumbe wakamuonesha kazi kama alivyooneshwa Hayati Bregadier Generali Afande Jaji Mstaafu Augustine Ramadhan
 
Moja ya vitu vinavyowafanya kujiingiza kwny life hilo baya ni msingi mbovu wa maisha
Kuna watu wamejaariwa uhai na afya.....mtu kastafu 2001,...hadi leo ana afya tele.....ukiwaona vijana na mabinti wadogo waliozaliwa 2001,wanajihusisha na matumizi ya mihadarati,pombe,ngono zembe na kujiuza unaona kabisa wamezeeka hata kufika robo ya miaka ya generali ni mtihani
 
Hayati Mama yake Mzazi alikuwa Mtu wa Vyombo sana hadi Huyu Waziri akiwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika mashariki wakati wa Bakari Mwapachu yule Bi Mkubwa alikuwa ana nguvu sana na akiamua kutimba pale Palm beach kumwagia Moyo alikuwa anachukua taxi na anatukuta pale na kutupiga offer sie team Juice

Huyu Binti kafuata roho ya ubinadamu, upendo na utu ya Bi Mkubwa wake


Ila Mama pis kali kinoma,inaonekana anaomba ushauri maana hiyo wizara haihitaji waziri wala naibu katibu mkuu tu anatosha tena wamteue wao.
 
Mzee Mboma bado yuko fit sana..

Kila la heri kwake.
 
yoga twaomba story zinazo husiana na na hawa wazee. Wapo kama hawapo je ukimya wao ni jibu kuwa hawajihusishi na maswala mazito ya nchi hii?
 
Back
Top Bottom