Wazo la Leo: Aliyeumwa na Nyoka...

Wazo la Leo: Aliyeumwa na Nyoka...

Why huwa mna list NBC...??

NBC inaingiaje kama mfano mbaya??

Mbona bank za Serikali zilizo Baki mikononi mwa NBC zote zimefeli kuliko NBC???
 
Ni kawaida yao kutangaza neema zijazo halafu baadae tunagundua tulipigwa.

Yaani tumegeuka kama watu wa nchi ya kusadikika ambayo mwandishai Shaban Robert anasema wana kawaida ya kutafuta fimbo baada ya kwisha kung'atwa na nyoka!
 
Wananchi walimkubali Magufuli, kisha Magufuli akapora uchaguzi! Sasa kama wananchi walimkubali bado akapora uchaguzi, wangekuwa hawamkubali ingekuwaje?
Na ukiangalia yule marehemu ameonyesha dira ni namna gani rais ama chama kinaweza tumia vbaya mamlaka yake bila kufanywa chochote
 
Hapana kwa kwelly hata kama mm sio mtaalamu lakini kwa hapa . Tumepigwa
Screenshot_20230613-224409.png
 
Una hakika mikataba waliyosaini DP World Uingereza ni ya hovyo kama ilivyo hapa kwetu? muhimu tambua tu, ujinga wa msaliti wetu sio universal.

Hivi wewe kwa akili zako timamu unaweza vipi kutoa "Exclusive Rights" kwa mgeni anayekuja kuwekeza nchini kwako?

Yani unamuacha mgeni ndio awe bosi wako wewe mwenyeji, huu kwangu sio ujinga tu, ni ujinga unaoambatana na laana, elimu ya huyu msaliti lazima ichunguzwe, anaweza kuwa alighushi vyeti, sasa nina mashaka nae sana.
Mkataba tuliosaini na Dp World una u hovyo gani?
 
Twiga bank imefilisika..
Tib bank imeenda..
Bank ya wanawake imeenda
Bank ya wakulima imeenda..
Tcb inayumba ...haijaweza fikia NBC licha kuwa iko serikalini...
Nani wamefilisi hizo bank? Salama ya NBC ni awamu ya tano. It was going down the drain.....pengine kufunga
Maduka ya kubadili pesa...pengine kudhibiti wakopaji wenye agenda za kutolipa...ila hatuna cha kujivunia kwenye uwekezaji so far.
 
Tatizo siyo DP World... tatizo ni kumbukumbu zetu... Sababu zinazotolewa ni zilezile na serikali inayotoa ni ya Chama kilekile...

NBC
TANESCO
ATC
TRC
UDA

Mwisho wa siku tukajikuta tunarudisha mikomoni mwa "wazalendo"...

Hili la bandari ni majaribio yaleyale ya kushindwa kwetu?
Tatizo kubwa ni uendeshaji na waendeshaji wa mashirika hata hizo bandari wakisema sheria ibadilike iwe ruhusa kwa watu au kampuni binafsi kuwekeza ktk ujenzi na huduma za bandari yaani kuwe na private ports zilipe kodi kama kampuni nyingine si yatatokea yale yale kama ya ttcl ujio wa hizi kampuni binafsi za simu zimeuwa ttcl sokoni ,watanzania wengi watapiga makelele mengi sana kwa kuwa tu wanafuata mkumbo kwa kuwa fulani kasema wanamheshimu ila likifika suala la utashi binafsi wa kupata huduma utawaona machaguo yao huwa yanakuwa tofauti na makelele yao.
Ila ni wakati sasa haya mashirika ya umma yaache kusubiri ruzuku yatafute mikopo yaboreshe mitaji yao na teknolojia na yafanye biashara yalipe mikopo yapeleke faida serikalini taifa lifaidike na uwepo wao.
 
Back
Top Bottom