Wazulu wa Imhambane, Kwalikunyu - Msumbiji katika kupigania Uhuru wa Tanganyika

Wazulu wa Imhambane, Kwalikunyu - Msumbiji katika kupigania Uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
WAZULU WA IMHAMBANE, MOZAMBIQUE KATIKA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA

Kisa hiki nimekitoa hapa hapa barzani nikizungumza na ndugu yangu Abdulkarim.

"Abdulkarim, jina hasa ni Saudtz Thomas Plantan.

Baba yake ni Thomas Saudtz Plantan na alikuwa Mwalimu Mkuu wa Mchikichini Primary School na kabla ya hapo alifundisha Dodoma.

Mmoja wa wanafunzi wake ni Job Lusinde aliyekuja kuwa waziri katika serikali ya Tanganyika.

Babu yake Sauti ni Chief Mohosh kutoka Shangaan Afrika ya Kusini.

Chief Shangaan na watu wake walikimbia kwao na kuingia Mozambique, Imhambane kukwepa vita vya Shaka.

Mjerumani Hermann von Wissman alifika Imhambane kijiji cha Kwalikunyi kutafuta askari mamluki waje Germany Ostafrika kupigana na Abushiri bin Salim Al Harith na Mtwa Mkwawa.

Hii ni baada ya Berlin Conference 1886.

Chief Mohosh na jeshi lake wakiongozwa na Wissman walikuja na manowari hadi Pangani na kuweka kambi hapo.

Katika jeshi hili la Wazulu alikuwapo Sykes Mbuwane ambae huko walikotoka dada yake aliolewa na Chief Mohosh.

Alikuwapo pia Ally Katini ndugu yake Sykes Mbuwane aiyekuwa kipofu.

Huyu Ally Sykes aliyekuja kuwa mtu maarufu sana jina hilo lake amepewa jina la huyu babu yake Ally Katini nduguye Sykes Mbuwane.

Huyu Sykes Mbuwane ndiye baba yake Kleist ambae mama yake ni Mnyaturu.

Kleist Sykes alizaliwa hapo Pangani 1894.

Hili jeshi lilikuwa pia na Wanubi kutoka Sudan wote wamechukuliwa na Wissman.

Wissman aliwaambia Wazulu katika mkataba wao kuwa wakishinda vita watatawala nchi kwa pamoja yaani Wajerumani na Wazulu watakuwa na madaraka sawa.

Ingawa Wajerumani waliweka ahadi hiyo jeshi hili maofisa walikuwa Wajerumani wenyewe na Wazulu walikuwa askari lakini kiongozi wao alikuwa Chief Mohosh ambae sasa akiwa katika nchi ya ugenini akabadili jina akawa Affande Plantan.

Baada ya kumshinda Abushiri ambae walimnyonga hapo Pangani jeshi likaelekea Kalenga kupambana na Mkwawa.

Vita hizi mbili zina historia kubwa lakini hapa naeleza kwa kifupi.

Wahehe wakashindwa vita na Mkwawa akajiua.

Wakati wanarudi kutoka Kalenga baada ya kushinda vita Sykes Mbuwane akafa maji Mto Ruaha akamwacha mwanae Pangani bado mdogo.

Haukupita muda na mama yake Kleist akafa.

Kleist akachukuliwa kulelewa na Affande Plantan.

Nchi ikatulia na hawa Wazulu na Wanubi wakawa ndiyo jeshi la kulinda himaya na likaitwa Germany Constabulary na mkuu wa jeshi hili alikuwa Affande Plantan.

Wajerumani walikuwa wanaliheshimu sana jeshi lao na waliliweka kambini na kutoa hudumu zote muhimu.

Wakajenga shule ilipo leo Ocean Road Hospital na katika shule hii ndipo walipowasomesha watoto wa askari wao.

Kwanza waliwafunza Kijerumani na elimu zote, pamoja na ufundi kisha wakawatia katika jeshi.

Hii ndiyo sababu watoto wote wa Affande Plantan: Thomas, Schneider, Mashado na Kleist walipata elimu ya juu kwa wakati ule na wote walikuwa askari jeshi.

Hawa wote walikuwa wakizungumza Kijerumani kama maji.

Hawa watoto wa Affande Plantan pamoja na mwanae wa kulea Kleist walipata fursa kubwa na walifanikiwa sana katika maisha yao hasa baada ya WWI Waingereza walipotawala Tanganyika kuanzia 1918.

Kleist alijulikana Dar-es-Salaam kama Kleist Plantan hadi alipofariki Affande Plantan ndipo alipochukua jina la baba yake mzazi, Sykes.

Watoto hawa walitawala siasa za Dar es Salaam wakati wa Waingereza na wakajenga msingi wa kudai uhuru wa Tanganyika kupitia African Association kisha TANU.

Kleist Sykes akaasisi African Association 1929 akiwa katibu muasisi na Mwalimu Thomas Plantan alikuja akawa rais wa TAA katika kipindi cha WWII.

Schneider Plantan yeye ndiye 1950 aliyeshinikiza TAA uongozi uende kwa vijana na akafanikiwa kuwatia Dr. Vedasto Kyaruzi na Abdul Sykes katika nafasi ya rais na katibu.

Historia hii ni ndefu na ina mengi.

Ikutoshe tu kuwa Schneider na Kleist Affande walivaa uniform ya Kaiser kupigana vita dhidi ya Waingereza katika Vita Vya Kwanza Vya Dunia 1914 - 1918."

Haya ndiyo aliyoandika Kleist Sykes na kutuachia kama urithi wetu kabla hajafa mwaka wa 1949.

Mswada huu alikuwanao Abdul Sykes hadi alipofariki 1968.

Historia ina kawaia ya kujirudia.

Vita Vya Pili Vya Dunia Abdul Sykes na Ally Sykes, watoto wa Kleist na wajukuu wa Sykes Mbuwane walivaa unifomu ya Mfalme wa Uingereza kupigana dhidi ya Wajerumani wakiwa katika King's African Rifles (KAR) 6th Battalion.

Picha hiyo ya kwanza kushoto ni Kleist Abduwahid Kleist Sykes Mbuwane, Ebby Abdulwahid Kleist Sykes Mbuwane, Saudtz Thomas Saudtz Plantan, Abdulwahid Ally Kleist Sykes Mbuwane.

Hawa ni vitukuu vya koo mbili hizi za Sykes Mbuwane na Chief Mohosh kutoka Imhambane, Mozambique.

Picha ya pili ni Thomas Saudtz Plantan na ya tatu ni Kleist Sykes.

Picha ya nne kulia ni Abdul Sykes na Ally Sykes katika unifomu ya KAR wakiwa Burma katika Vita Vya Pili Vya Dunia.

Screenshot_20211121-142852_Facebook.jpg
 
Usipokuwa na heshima kwa mtu usiyemjua hata unao wajua huna heshima wewe ok ana anapendelea upande mmoja nawe si uandike upande unao onewa punguza roho mbaya na kuweka vitu moyoni kwa hiyo ulikuwa unamfatilia na chuki zako.
nilishamsikia hata akiongea, anafanyaga kampeni ili ionekana Tanzania ilipiganiwa uhuru na watu wa dini yake, hivyo wanaotakiwa kutawala ni watu wa dini yake, sijaanza kumsikia leo wala jana. anapandikiza chuki ili ionekana watu wa dini yake wanapunjwa kiutaawala, kieliu n.k, hii nimbaya na ndiyo iliyoibua kipindi kile vijana wengi wanaharakati hadi kuchapisha vipeperushi kwamba nyerere alikuwa audui wa uislam. mtu anayepandikiza chuki hata kama ni mtu mzima hatufai hapa Tz, hivi unafikiri chuki ikisambaa kwamba waislam wanaonewa wao ndio walipigania uhuru hivyo wanatakiwa kupata share kubwa kuliko wengine, patatosha? kwani hao watu wengine hawana m chango wowote? wewe nawe naona una vimelea vya udini, mmeshachelewa. nawashauri somesheni watoto wenu ili wapate elimu washindane kwa hoja na sio kwa imani. nchi hii ni secular, ni ya kila mtu.
 
nilishamsikia hata akiongea, anafanyaga kampeni ili ionekana Tanzania ilipiganiwa uhuru na watu wa dini yake, hivyo wanaotakiwa kutawala ni watu wa dini yake, sijaanza kumsikia leo wala jana. anapandikiza chuki ili ionekana watu wa dini yake wanapunjwa kiutaawala, kieliu n.k, hii nimbaya na ndiyo iliyoibua kipindi kile vijana wengi wanaharakati hadi kuchapisha vipeperushi kwamba nyerere alikuwa audui wa uislam. mtu anayepandikiza chuki hata kama ni mtu mzima hatufai hapa Tz, hivi unafikiri chuki ikisambaa kwamba waislam wanaonewa wao ndio walipigania uhuru hivyo wanatakiwa kupata share kubwa kuliko wengine, patatosha? kwani hao watu wengine hawana m chango wowote? wewe nawe naona una vimelea vya udini, mmeshachelewa. nawashauri somesheni watoto wenu ili wapate elimu washindane kwa hoja na sio kwa imani. nchi hii ni secular, ni ya kila mtu.
Naomba unijibu maswali yangu
1:Ni wapi mtoa mada alisema waislamu ndio wahusika wakuu kupigania uhuru kwenye mada zake iwe hapa au huko unakomfatilia
2:Ni wapi aliandika watu wa dini yake wamepunjwa.
Jibu hoja acha lawama zisizokuwa na faida
 
Naomba unijibu maswali yangu
1:Ni wapi mtoa mada alisema waislamu ndio wahusika wakuu kupigania uhuru kwenye mada zake iwe hapa au huko unakomfatilia
2:Ni wapi aliandika watu wa dini yake wamepunjwa.
Jibu hoja acha lawama zisizokuwa na faida
nilimsikia kwa masikio yangu akiongea, nimerefer alichokuwa anaongea nikimsikia. wewe naona ni mohamed said kwenye ID yako nyingine. pole.
 
nilimsikia kwa masikio yangu akiongea, nimerefer alichokuwa anaongea nikimsikia. wewe naona ni mohamed said kwenye ID yako nyingine. pole.
Kumbe una lalamika pasipo kuwa na ushahidi nikwambie Ukome na ushike adabu yako kumzushia uwongo Mzee wetu kama haupendi imani yake au anachoandika tafadhali acha kusoma mada zake na kukoment
 
Kumbe una lalamika pasipo kuwa na ushahidi nikwambie Ukome na ushike adabu yako kumzushia uwongo Mzee wetu kama haupendi imani yake au anachoandika tafadhali acha kusoma mada zake na kukoment
ushahidi gani? nimesema nilimsikia kwa masikio yangu, na sio mara moja. unataka nikwambie nini?Kwa akili yako unafikiri ningezuka tu na kumzushia huyu mzee mambo haya? mbona ingekuwa zambi?
 
ushahidi gani? nimesema nilimsikia kwa masikio yangu, na sio mara moja. unataka nikwambie nini?Kwa akili yako unafikiri ningezuka tu na kumzushia huyu mzee mambo haya? mbona ingekuwa zambi?
Acha uwongo wewe chuki zako udini zitakupa uchizi au unaona donge Mungu kumpa ufahamu Mzee wetu ulitaka awe mtu wa dini yako
 
huyu ni mdini na ni sumu na anaganga njaa hajawahi kua upande mmoja. anazeeka vibaya.
 
Acha uwongo wewe chuki zako udini zitakupa uchizi au unaona donge Mungu kumpa ufahamu Mzee wetu ulitaka awe mtu wa dini yako
Ashura Atanas umeona hio video naman anavyopandikiza chuki? alikuwa sambamba na shehe ilunga na kwenye kuchapisha zile CD, na kuanzisha vijana wengi wa kigaidi zenji. huyu jamaa ni adui wa taifa kabisa.
 


huyu ni mdini na ni sumu na anaganga njaa hajawahi kua upande mmoja. anazeeka vibaya.
Chapwa...
Kuwa nina dhiki hilo si kweli.

Nimeandika mengi na si mimi peke yangu.

Padri Sivalon kaeleza haya (1992).

P van Bergen (1981) kaeleza makubwa kunishinda na kitabu chake, "Religion and Development," kikiuzwa Cathedral Bookshop na ilipojulikana kitabu kimesema nini kikazuiwa.

Hamza Njozi kaandika na kitabu "Mwembechai Killings..." (2002)kikapigwa marufuku.

Serikali haijatukabili kutusuta kusema sisi ni waongo tunaeneza chuki.

Aboud Jumbe kaeleza haya (1992)
Prof. Malima yeye akiwa Waziri wa Elimu kaeleza haya katika barua rasmi kwa Rais Mwinyi (1987).

Wewe si Msemaji wa Serikali.
Iache serikali itupe sisi majibu.

Sheikh Ilunga katembea nchi nzima kueleza tatizo hili.

Kusema ni tatizo la uzee ni kichekesho.

Kitabu cha Abdul Sykes nimeandika nikiwa na miaka 30.

Tafuta vitabu hivi usome utaelewa kwa nini serikali ipo kimya miaka yote hii haijaweza kuliweka mezani tatizo hili.

Sikiliza kwa makini video hiyo ni moja kati ya mihadhara yangu inayopendwa sana.

Angalia watu wangapi wameiangalia toka 2009.

Ingia mohamedsaidsalum.blogspot.com kuna makala na video nyingi.
 
Ashura Atanas umeona hio video naman anavyopandikiza chuki? alikuwa sambamba na shehe ilunga na kwenye kuchapisha zile CD, na kuanzisha vijana wengi wa kigaidi zenji. huyu jamaa ni adui wa taifa kabisa.
Chapwa...
Adui ni yule anaekandamiza jamii moja na kunyanyua nyingine.

Huyu asietaka haki na usawa ndiye adui na lazima apigwe vita kwa dhulma yaani kuzuia haki za wengine.

Huyu ndiye sumu na adui mkubwa wa taifa hili hastahili kuachiwa aeneze fitna zake.

Soma historia ya uhuru utajifunza mengi kutoka kwa wazee wetu nini walifanya kuleta umoja.
 
Chapwa...
Adui ni yule anaekandamiza jamii moja na kunyanyua nyingine.

Huyu asietaka haki na usawa ndiye adui na lazima apigwe vita kwa udhalimu yaani kuzuia haki za wengine.
kwahiyo Mohamed Said unaamini wakristo wanakandamiza waislam Tanzania? waislam wanyimwa elimu? hivi, ni shule ngapi za wakristo zimeporwa ili zisiwe za mission, na zilianzishwa hata kabla hao watu wako hawajaanza kudai uhuru? hivi bila kanisa kuleta elimu hata wewe hapo uwezo wa kuandika kitabu chako ungepata wapi wakati waarabu walileta tu dini hawakuleta elimu? umeelimishwa halafu unasema umeonewa? udini umekujaaa, uliropoka sana kipindi kile cha shehe ilunga mkasababisha makanisa mengi kuchomwa zanzibar na watu kumwagiwa tindikali, haujatosheka.

kwa hali ilivyo Tanzania, mnataka wakristo wawafanyie nini ili mridhike, sema hapa hapa unataka tufanye nini? tuache kazi zote serikalini mshike ninyi? tuwapatie shule zote mshike ninyi sisi tujenge mpya? mbona chuo cha morogoro mlipewa lakini hata hakisikiki mnafundisha dini tu hamfundishi masomo? ini mtanata tufanye. sema hapahapa. umeona unavyoonyesha udini na siasa za chuki? unazeeka vibaya wewe.
 
Chapwa...
Kuwa nina dhiki hilo si kweli.

Nimeandika mengi na si mimi peke yangu.

Padri Sivalon kaeleza haya (1992).

P van Bergen (1981) kaeleza makubwa kunishinda na kitabu chake, "Religion and Development," kikiuzwa Cathedral Bookshop na ilipojulikana kitabu kimesema nini kikazuiwa.

Hamza Njozi kaandika na kitabu "Mwembechai Killings..." (2002)kikapigwa marufuku.

Serikali haijatukabili kutusuta kusema sisi ni waongo tunaeneza chuki.

Aboud Jumbe kaeleza haya (1992)
Prof. Malima yeye akiwa Waziri wa Elimu kaeleza haya katika barua rasmi kwa Rais Mwinyi (1987).

Wewe si Msemaji wa Serikali.
Iache serikali itupe sisi majibu.

Sheikh Ilunga katembea nchi nzima kueleza tatizo hili.

Kusema ni tatizo la uzee ni kichekesho.

Kitabu cha Abdul Sykes nimeandika nikiwa na miaka 30.

Tafuta vitabu hivi usome utaelewa kwa nini serikali ipo kimya miaka yote hii haijaweza kuliweka mezani tatizo hili.

Sikiliza kwa makini video hiyo no moja kati ya mihadhara inayopendwa sana.

Angalia watu wangapi wanaiangalia toka 2009.
amini usiamini we mzee, akili ikitawaliwa na dini peke yake huwa haiwazi sahihi, unaishia kuwa msambaza chuki tu ndo maana nilisema hata vitabu vyako havinaga mantiki ndio maana hata sio maarufu kwasabbu sio objective, ni vitabu vilivyoandikwa na mtu wa aina ya huyo anayeongea kwenye miihadhara ukisambaza chuki kwenye mioyo ya vijana wa kiislam.

ajabu yake, the more unasambaza chuki haiwasaidii vijana, hawapambani kwene maisha wakiamini wamepunjwa, kwahiyo wakristo waachie ngazi zooote mpate ninyi? tuachie hata shule tulizojenga? angalia shule tumejenga baada ya uhuru, ni nyingi mno na zinafanya vizuri, zanzibar nako ambako wakristo ni wachache wanachapwa fimbo wakila chakula siku za mfungo utasema kuna mfumo kristo? mbona wanashika mkia kila mwaka elimu? we mzee kweli umesoma na una elimu wewe?
 
MOhamed said, orodhesha kwa numbering kabisa hapa chini. tutajie haki zipi za waislam unasema wamenyimwa, na mwisho toa suluhisho unataka serikali ifanye nini. hata ukisema unataka serikali iwape viti maalumu bungeni, au iwafaulishe hata bila kufanay mtihani sema tu. orodhesha hapa chini pengine utaeleweka.
 
nilishamsikia hata akiongea, anafanyaga kampeni ili ionekana Tanzania ilipiganiwa uhuru na watu wa dini yake, hivyo wanaotakiwa kutawala ni watu wa dini yake, sijaanza kumsikia leo wala jana. anapandikiza chuki ili ionekana watu wa dini yake wanapunjwa kiutaawala, kieliu n.k, hii nimbaya na ndiyo iliyoibua kipindi kile vijana wengi wanaharakati hadi kuchapisha vipeperushi kwamba nyerere alikuwa audui wa uislam. mtu anayepandikiza chuki hata kama ni mtu mzima hatufai hapa Tz, hivi unafikiri chuki ikisambaa kwamba waislam wanaonewa wao ndio walipigania uhuru hivyo wanatakiwa kupata share kubwa kuliko wengine, patatosha? kwani hao watu wengine hawana m chango wowote? wewe nawe naona una vimelea vya udini, mmeshachelewa. nawashauri somesheni watoto wenu ili wapate elimu washindane kwa hoja na sio kwa imani. nchi hii ni secular, ni ya kila mtu.
Chapwa...
Ikiwa unadhani tatizo ni kuwa Waislam hawapendi shule basi wala huna sifa ya kujadili chochote na mimi.
 
MOhamed said, orodhesha kwa numbering kabisa hapa chini. tutajie haki zipi za waislam unasema wamenyimwa, na mwisho toa suluhisho unataka serikali ifanye nini. hata ukisema unataka serikali iwape viti maalumu bungeni, au iwafaulishe hata bila kufanay mtihani sema tu. orodhesha hapa chini pengine utaeleweka.
Chapwa...
Wewe una mamlaka gani?
Serikali inajua.

Tosheka na ukweli huu.
 
Back
Top Bottom