Wazulu wa Imhambane, Kwalikunyu - Msumbiji katika kupigania Uhuru wa Tanganyika

Wazulu wa Imhambane, Kwalikunyu - Msumbiji katika kupigania Uhuru wa Tanganyika

Chapwa...
Hayo mengine ulioanzanayo hayana maana sana ila hili la elimu.

Ukisoma historia ya elimu utakugundua kuwa Waislam ndiyo waliokuwa na ujuzi wa zile zinaitwa 3Rs yaani Writing, Reading and Arithmetic.

Na alphabet zilizokuwa zinatumika ni Arabic script.

Elimu yote hii ilikuwa ikitolewa kupitia madras.

Krapf alipofika kwa Chief Kimweri Vuga alishangaa sana kumkuta Chief Kimweri na wanae wote wanajua kuandika na kusoma wakitumia herufu za Kiarabu.

Hii ilitia hasad ndani ya nyoyo yake na wakoloni walipoingia katika Pwani ya Afrika ya Mashariki jambo la kwanza walilofanya ilikuwa kupiga marufuku matumizi ya herufi za Kiarabu.

Hapo ndipo wakajenga shule Wamishionari wakishirikiana na serikali.

Na elimu ikawa inatolewa kwa ubaguzi wa imani.

Yako mengi.
Sasa herufi za Kiarabu zinahusiana nini na Uislamu?
 
WAZULU WA IMHAMBANE, MOZAMBIQUE KATIKA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA

Kisa hiki nimekitoa hapa hapa barzani nikizungumza na ndugu yangu Abdulkarim.

"Abdulkarim, jina hasa ni Saudtz Thomas Plantan.

Baba yake ni Thomas Saudtz Plantan na alikuwa Mwalimu Mkuu wa Mchikichini Primary School na kabla ya hapo alifundisha Dodoma.

Mmoja wa wanafunzi wake ni Job Lusinde aliyekuja kuwa waziri katika serikali ya Tanganyika.

Babu yake Sauti ni Chief Mohosh kutoka Shangaan Afrika ya Kusini.

Chief Shangaan na watu wake walikimbia kwao na kuingia Mozambique, Imhambane kukwepa vita vya Shaka.

Mjerumani Hermann von Wissman alifika Imhambane kijiji cha Kwalikunyi kutafuta askari mamluki waje Germany Ostafrika kupigana na Abushiri bin Salim Al Harith na Mtwa Mkwawa.

Hii ni baada ya Berlin Conference 1886.

Chief Mohosh na jeshi lake wakiongozwa na Wissman walikuja na manowari hadi Pangani na kuweka kambi hapo.

Katika jeshi hili la Wazulu alikuwapo Sykes Mbuwane ambae huko walikotoka dada yake aliolewa na Chief Mohosh.

Alikuwapo pia Ally Katini ndugu yake Sykes Mbuwane aiyekuwa kipofu.

Huyu Ally Sykes aliyekuja kuwa mtu maarufu sana jina hilo lake amepewa jina la huyu babu yake Ally Katini nduguye Sykes Mbuwane.

Huyu Sykes Mbuwane ndiye baba yake Kleist ambae mama yake ni Mnyaturu.

Kleist Sykes alizaliwa hapo Pangani 1894.

Hili jeshi lilikuwa pia na Wanubi kutoka Sudan wote wamechukuliwa na Wissman.

Wissman aliwaambia Wazulu katika mkataba wao kuwa wakishinda vita watatawala nchi kwa pamoja yaani Wajerumani na Wazulu watakuwa na madaraka sawa.

Ingawa Wajerumani waliweka ahadi hiyo jeshi hili maofisa walikuwa Wajerumani wenyewe na Wazulu walikuwa askari lakini kiongozi wao alikuwa Chief Mohosh ambae sasa akiwa katika nchi ya ugenini akabadili jina akawa Affande Plantan.

Baada ya kumshinda Abushiri ambae walimnyonga hapo Pangani jeshi likaelekea Kalenga kupambana na Mkwawa.

Vita hizi mbili zina historia kubwa lakini hapa naeleza kwa kifupi.

Wahehe wakashindwa vita na Mkwawa akajiua.

Wakati wanarudi kutoka Kalenga baada ya kushinda vita Sykes Mbuwane akafa maji Mto Ruaha akamwacha mwanae Pangani bado mdogo.

Haukupita muda na mama yake Kleist akafa.

Kleist akachukuliwa kulelewa na Affande Plantan.

Nchi ikatulia na hawa Wazulu na Wanubi wakawa ndiyo jeshi la kulinda himaya na likaitwa Germany Constabulary na mkuu wa jeshi hili alikuwa Affande Plantan.

Wajerumani walikuwa wanaliheshimu sana jeshi lao na waliliweka kambini na kutoa hudumu zote muhimu.

Wakajenga shule ilipo leo Ocean Road Hospital na katika shule hii ndipo walipowasomesha watoto wa askari wao.

Kwanza waliwafunza Kijerumani na elimu zote, pamoja na ufundi kisha wakawatia katika jeshi.

Hii ndiyo sababu watoto wote wa Affande Plantan: Thomas, Schneider, Mashado na Kleist walipata elimu ya juu kwa wakati ule na wote walikuwa askari jeshi.

Hawa wote walikuwa wakizungumza Kijerumani kama maji.

Hawa watoto wa Affande Plantan pamoja na mwanae wa kulea Kleist walipata fursa kubwa na walifanikiwa sana katika maisha yao hasa baada ya WWI Waingereza walipotawala Tanganyika kuanzia 1918.

Kleist alijulikana Dar-es-Salaam kama Kleist Plantan hadi alipofariki Affande Plantan ndipo alipochukua jina la baba yake mzazi, Sykes.

Watoto hawa walitawala siasa za Dar es Salaam wakati wa Waingereza na wakajenga msingi wa kudai uhuru wa Tanganyika kupitia African Association kisha TANU.

Kleist Sykes akaasisi African Association 1929 akiwa katibu muasisi na Mwalimu Thomas Plantan alikuja akawa rais wa TAA katika kipindi cha WWII.

Schneider Plantan yeye ndiye 1950 aliyeshinikiza TAA uongozi uende kwa vijana na akafanikiwa kuwatia Dr. Vedasto Kyaruzi na Abdul Sykes katika nafasi ya rais na katibu.

Historia hii ni ndefu na ina mengi.

Ikutoshe tu kuwa Schneider na Kleist Affande walivaa uniform ya Kaiser kupigana vita dhidi ya Waingereza katika Vita Vya Kwanza Vya Dunia 1914 - 1918."

Haya ndiyo aliyoandika Kleist Sykes na kutuachia kama urithi wetu kabla hajafa mwaka wa 1949.

Mswada huu alikuwanao Abdul Sykes hadi alipofariki 1968.

Historia ina kawaia ya kujirudia.

Vita Vya Pili Vya Dunia Abdul Sykes na Ally Sykes, watoto wa Kleist na wajukuu wa Sykes Mbuwane walivaa unifomu ya Mfalme wa Uingereza kupigana dhidi ya Wajerumani wakiwa katika King's African Rifles (KAR) 6th Battalion.

Picha hiyo ya kwanza kushoto ni Kleist Abduwahid Kleist Sykes Mbuwane, Ebby Abdulwahid Kleist Sykes Mbuwane, Saudtz Thomas Saudtz Plantan, Abdulwahid Ally Kleist Sykes Mbuwane.

Hawa ni vitukuu vya koo mbili hizi za Sykes Mbuwane na Chief Mohosh kutoka Imhambane, Mozambique.

Picha ya pili ni Thomas Saudtz Plantan na ya tatu ni Kleist Sykes.

Picha ya nne kulia ni Abdul Sykes na Ally Sykes katika unifomu ya KAR wakiwa Burma katika Vita Vya Pili Vya Dunia.

View attachment 2018683
Kwa hakika ni vizuri kumshukuru sana Mohamed Said juhudi zake za kutujuza kuhusu historia ya nchi yetu. Histora ya Afrika, hususan ya Tanganyika ni pungufu mno haijaelezwa kwa ukamilifu. Huyu mwenzetu anatuletea maandiko hata ushuhuda ambao umefichika. Ila tukubaliane kuwa simulizi sahihi ni kitu kimoja ila maana ya simulizi, tafsiri na matumizi ya simulizi ni vitu viwili tofauti na hiyo tofauti lazima pande zote zikubali kuwa hakuna mwenye ukiritimba. Hivi akina Sykes walipokuwa wanapigana na Chief Mbano, kwa mfano, si hii ilikuwa Mzulu mwingine anapigana na mwenziwe ila mmoja katua Pangani meli kuingia Tanganyika mwingine kaja kwa mguu kutoka Zululand Afrika ya Kusini? Simulizi inaweza kuwa sahihi, je? Lakini jambo la kujivunia hapo ni lipi? Je, kweli Waislam wanaamini kwa dhati kabisa kuwa Nyerere hakuwathamini na kutambua mchango wa Waislam hapa Tanzania? Kwani alipotaifisha shule na hospitali alikuwa anataka kuwanufaisha akina nani? Mimi nilisoma Sekondari ya Mission Alliance Rungwe mwaka 1965 kabla ya shule kutaifishwa. Pale niliwakuta wanafunzi Waislam wengi wakitokea Iringa wakilazimishwa na wenyewe waende na wakae kwenye madarasa yao kujifunza elimu ya dini ya Kiislam wakati wa vipindi vya dini ambavyo hata sisi Wakristo tulilazimishwa kujifunza! Pia waliwezeshwa wakati wa Mfungo wa Ramadhan kutimiza hiyo Ibada. Headmaster wetu alikuwa Mzungu na alifanya hivyo akijua kuwa huo ndiyo ulikuwa msimamo wa Rais Nyerere wakati huo. Haya kuhusu mchango wa Waislam katika kupigania uhuru kutowekwa dhahiri kwa maandishi, kwani hapa Tanzania hilo ni geni? Sasa hivi huwa mnaelezwa mchango wa watu binafsi au kundi kwenye masuala mengi ya kheri,iwe ushindi wa vita, elimu, afya au masuala ya maendeleo mengine. Mimi najua mashujaa kadhaa ambao wamezikwa kawaida wakati viongozi wao hata robo ya mchango wao hawakuufikia. Historia na michango yao imefichika. Sifa zinakwenda Serikalini au kwa Rais wa wakati huo kumbe pengine hawakuchangia hata kidogo kufanikisha jambo lenyewe, ilikuwa juhudi binafsi ya mtu au kundi la watu. Kwa mfano, hivi sasa orodha ya Makatibu wakuu bora, askari bora, daktari bora waliowahi kutokea katika historia ya nchi hii iko wapi ? Kwenye nchi zilizojiita za ujamaa ndiyo ilikuwa marufuku kabisa kusifu mtu au kikundi ila "Zidumu fikra za kiongozi" husika ndiyo ulikuwa wimbo uliokubalika na kuzoeleka. Huo ndiyo urithi wetu. Tusigombane bure. Wakristo, Waislam na wengine wote tumekuwa na mchango kadri ya kila mmoja wetu alivyojaaliwa na Mola wetu! Tuendelee kuishi pamoja na kushirikiana.
 
WAZULU WA IMHAMBANE, MOZAMBIQUE KATIKA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA

Kisa hiki nimekitoa hapa hapa barzani nikizungumza na ndugu yangu Abdulkarim.

"Abdulkarim, jina hasa ni Saudtz Thomas Plantan.

Baba yake ni Thomas Saudtz Plantan na alikuwa Mwalimu Mkuu wa Mchikichini Primary School na kabla ya hapo alifundisha Dodoma.

Mmoja wa wanafunzi wake ni Job Lusinde aliyekuja kuwa waziri katika serikali ya Tanganyika.

Babu yake Sauti ni Chief Mohosh kutoka Shangaan Afrika ya Kusini.

Chief Shangaan na watu wake walikimbia kwao na kuingia Mozambique, Imhambane kukwepa vita vya Shaka.

Mjerumani Hermann von Wissman alifika Imhambane kijiji cha Kwalikunyi kutafuta askari mamluki waje Germany Ostafrika kupigana na Abushiri bin Salim Al Harith na Mtwa Mkwawa.

Hii ni baada ya Berlin Conference 1886.

Chief Mohosh na jeshi lake wakiongozwa na Wissman walikuja na manowari hadi Pangani na kuweka kambi hapo.

Katika jeshi hili la Wazulu alikuwapo Sykes Mbuwane ambae huko walikotoka dada yake aliolewa na Chief Mohosh.

Alikuwapo pia Ally Katini ndugu yake Sykes Mbuwane aiyekuwa kipofu.

Huyu Ally Sykes aliyekuja kuwa mtu maarufu sana jina hilo lake amepewa jina la huyu babu yake Ally Katini nduguye Sykes Mbuwane.

Huyu Sykes Mbuwane ndiye baba yake Kleist ambae mama yake ni Mnyaturu.

Kleist Sykes alizaliwa hapo Pangani 1894.

Hili jeshi lilikuwa pia na Wanubi kutoka Sudan wote wamechukuliwa na Wissman.

Wissman aliwaambia Wazulu katika mkataba wao kuwa wakishinda vita watatawala nchi kwa pamoja yaani Wajerumani na Wazulu watakuwa na madaraka sawa.

Ingawa Wajerumani waliweka ahadi hiyo jeshi hili maofisa walikuwa Wajerumani wenyewe na Wazulu walikuwa askari lakini kiongozi wao alikuwa Chief Mohosh ambae sasa akiwa katika nchi ya ugenini akabadili jina akawa Affande Plantan.

Baada ya kumshinda Abushiri ambae walimnyonga hapo Pangani jeshi likaelekea Kalenga kupambana na Mkwawa.

Vita hizi mbili zina historia kubwa lakini hapa naeleza kwa kifupi.

Wahehe wakashindwa vita na Mkwawa akajiua.

Wakati wanarudi kutoka Kalenga baada ya kushinda vita Sykes Mbuwane akafa maji Mto Ruaha akamwacha mwanae Pangani bado mdogo.

Haukupita muda na mama yake Kleist akafa.

Kleist akachukuliwa kulelewa na Affande Plantan.

Nchi ikatulia na hawa Wazulu na Wanubi wakawa ndiyo jeshi la kulinda himaya na likaitwa Germany Constabulary na mkuu wa jeshi hili alikuwa Affande Plantan.

Wajerumani walikuwa wanaliheshimu sana jeshi lao na waliliweka kambini na kutoa hudumu zote muhimu.

Wakajenga shule ilipo leo Ocean Road Hospital na katika shule hii ndipo walipowasomesha watoto wa askari wao.

Kwanza waliwafunza Kijerumani na elimu zote, pamoja na ufundi kisha wakawatia katika jeshi.

Hii ndiyo sababu watoto wote wa Affande Plantan: Thomas, Schneider, Mashado na Kleist walipata elimu ya juu kwa wakati ule na wote walikuwa askari jeshi.

Hawa wote walikuwa wakizungumza Kijerumani kama maji.

Hawa watoto wa Affande Plantan pamoja na mwanae wa kulea Kleist walipata fursa kubwa na walifanikiwa sana katika maisha yao hasa baada ya WWI Waingereza walipotawala Tanganyika kuanzia 1918.

Kleist alijulikana Dar-es-Salaam kama Kleist Plantan hadi alipofariki Affande Plantan ndipo alipochukua jina la baba yake mzazi, Sykes.

Watoto hawa walitawala siasa za Dar es Salaam wakati wa Waingereza na wakajenga msingi wa kudai uhuru wa Tanganyika kupitia African Association kisha TANU.

Kleist Sykes akaasisi African Association 1929 akiwa katibu muasisi na Mwalimu Thomas Plantan alikuja akawa rais wa TAA katika kipindi cha WWII.

Schneider Plantan yeye ndiye 1950 aliyeshinikiza TAA uongozi uende kwa vijana na akafanikiwa kuwatia Dr. Vedasto Kyaruzi na Abdul Sykes katika nafasi ya rais na katibu.

Historia hii ni ndefu na ina mengi.

Ikutoshe tu kuwa Schneider na Kleist Affande walivaa uniform ya Kaiser kupigana vita dhidi ya Waingereza katika Vita Vya Kwanza Vya Dunia 1914 - 1918."

Haya ndiyo aliyoandika Kleist Sykes na kutuachia kama urithi wetu kabla hajafa mwaka wa 1949.

Mswada huu alikuwanao Abdul Sykes hadi alipofariki 1968.

Historia ina kawaia ya kujirudia.

Vita Vya Pili Vya Dunia Abdul Sykes na Ally Sykes, watoto wa Kleist na wajukuu wa Sykes Mbuwane walivaa unifomu ya Mfalme wa Uingereza kupigana dhidi ya Wajerumani wakiwa katika King's African Rifles (KAR) 6th Battalion.

Picha hiyo ya kwanza kushoto ni Kleist Abduwahid Kleist Sykes Mbuwane, Ebby Abdulwahid Kleist Sykes Mbuwane, Saudtz Thomas Saudtz Plantan, Abdulwahid Ally Kleist Sykes Mbuwane.

Hawa ni vitukuu vya koo mbili hizi za Sykes Mbuwane na Chief Mohosh kutoka Imhambane, Mozambique.

Picha ya pili ni Thomas Saudtz Plantan na ya tatu ni Kleist Sykes.

Picha ya nne kulia ni Abdul Sykes na Ally Sykes katika unifomu ya KAR wakiwa Burma katika Vita Vya Pili Vya Dunia.

View attachment 2018683

Ok, kumbe kwa asili akina Abdul Sykes walikuwa wazulu. Nimenote kitu leo.
 
Kwa hiyo kilwa ya karne ya tisa ile ya maghorofa na shilingi yake yenyewe ilijengwa na mzungu ewe mfia dini? Unazijua kweli Arabic numerals? Unaijua kweli historia ewe mfia dini? Hiyo hekaya kwamba hapakuwa na maendeleo kakudanganya nani? Ni kweli hufahamu kwamba mkoloni alipigana na Bwana heri upande wa pili akaingia makubaliano na makafiri? Ee masih mwana wa maryam

Unaimuita mwenzako mfia dini wakati na wewe Ni mdini. Eti makafir. Makafir walikuwa wapi?. Acheni kilujiona Bora kuliko dini zingine.
 
Na ww hutaki waislamu wajue kama wanamchango mkubwa kwenye uhuru na jinsi nyerer alivyofanya hila kuwadhulu.Ukweli unatabia ya ajabu sana hata ikichukua miaka 400 kufichwa ila utajulikana tu.Swali muhimu watu wenye akili wanalojiuliza hv Nyerere ni peke yake aliyeleta uhuru wa nchi hii?Jibu hapana alikua na wenzake .
Swali wenzie ni akina nan hapo ndio kazi ilpo

Kasome historia vizuri. Nyerere alimshinda Abdul Sykes kwa Kura kwenye ukumbi wa annatouglo Dar. Kama Sykes angeshinda siku hiyo basi ndio angekuwa Baba wa Taifa leo.
 
Kwa hakika ni vizuri kumshukuru sana Mohamed Said juhudi zake za kutujuza kuhusu historia ya nchi yetu. Histora ya Afrika, hususan ya Tanganyika ni pungufu mno haijaelezwa kwa ukamilifu. Huyu mwenzetu anatuletea maandiko hata ushuhuda ambao umefichika. Ila tukubaliane kuwa simulizi sahihi ni kitu kimoja ila maana ya simulizi, tafsiri na matumizi ya simulizi ni vitu viwili tofauti na hiyo tofauti lazima pande zote zikubali kuwa hakuna mwenye ukiritimba. Hivi akina Sykes walipokuwa wanapigana na Chief Mbano, kwa mfano, si hii ilikuwa Mzulu mwingine anapigana na mwenziwe ila mmoja katua Pangani meli kuingia Tanganyika mwingine kaja kwa mguu kutoka Zululand Afrika ya Kusini? Simulizi inaweza kuwa sahihi, je? Lakini jambo la kujivunia hapo ni lipi? Je, kweli Waislam wanaamini kwa dhati kabisa kuwa Nyerere hakuwathamini na kutambua mchango wa Waislam hapa Tanzania? Kwani alipotaifisha shule na hospitali alikuwa anataka kuwanufaisha akina nani? Mimi nilisoma Sekondari ya Mission Alliance Rungwe mwaka 1965 kabla ya shule kutaifishwa. Pale niliwakuta wanafunzi Waislam wengi wakitokea Iringa wakilazimishwa na wenyewe waende na wakae kwenye madarasa yao kujifunza elimu ya dini ya Kiislam wakati wa vipindi vya dini ambavyo hata sisi Wakristo tulilazimishwa kujifunza! Pia waliwezeshwa wakati wa Mfungo wa Ramadhan kutimiza hiyo Ibada. Headmaster wetu alikuwa Mzungu na alifanya hivyo akijua kuwa huo ndiyo ulikuwa msimamo wa Rais Nyerere wakati huo. Haya kuhusu mchango wa Waislam katika kupigania uhuru kutowekwa dhahiri kwa maandishi, kwani hapa Tanzania hilo ni geni? Sasa hivi huwa mnaelezwa mchango wa watu binafsi au kundi kwenye masuala mengi ya kheri,iwe ushindi wa vita, elimu, afya au masuala ya maendeleo mengine. Mimi najua mashujaa kadhaa ambao wamezikwa kawaida wakati viongozi wao hata robo ya mchango wao hawakuufikia. Historia na michango yao imefichika. Sifa zinakwenda Serikalini au kwa Rais wa wakati huo kumbe pengine hawakuchangia hata kidogo kufanikisha jambo lenyewe, ilikuwa juhudi binafsi ya mtu au kundi la watu. Kwa mfano, hivi sasa orodha ya Makatibu wakuu bora, askari bora, daktari bora waliowahi kutokea katika historia ya nchi hii iko wapi ? Kwenye nchi zilizojiita za ujamaa ndiyo ilikuwa marufuku kabisa kusifu mtu au kikundi ila "Zidumu fikra za kiongozi" husika ndiyo ulikuwa wimbo uliokubalika na kuzoeleka. Huo ndiyo urithi wetu. Tusigombane bure. Wakristo, Waislam na wengine wote tumekuwa na mchango kadri ya kila mmoja wetu alivyojaaliwa na Mola wetu! Tuendelee kuishi pamoja na kushirikiana.
Peter...
Kweli shule zilitaifishwa lakini kwa bahati mbaya sana pakawa na tatizo katika nafasi za Waislam kwenda sekondari kufikia chuo kikuu.

Hili ni tatizo kubwa na hapa tushajadili sana.

Rais Mkapa alipochukua urais katika mkutano aliofanya na Waislam Diamond Jubilee Hall kuna mengi alielezwa na yeye akasema kuwa kama Waislam wana ushahidi wa kisayansi kuwa wanadhulumiwa na watendaji ndani ya serikali wautoe.

Hii ndiyo sababu ya Hamza Njozi kuandika kitabu, ''Mwembechai Kiliings...'' (2002).
Yaliyoelezwa mle ndani yaliishtua serikali.

Kitabu kikapigwa marufuku.
 
Bahati mbaya sana kaka, unajua achilia mbali hii historia ya juzi ya Mohamed said, bali hata ile ya Tanganyika ya Enzi hizo ilikuwa ya waislamu kabla ya kuja kina vasco dagama na hasadi zao kubomoa miji ya pwani, mimi nitaungana nawe ikiwa Mohamed said tutasikitika nae kwa kule kuwa wa Africa wa kizulu kuja kupambana na wa africa wenzao kama kina chief Mkwawa au Songea Mmbano n. K kwa hilo nitakuunga mkono ila bahati mbaya kwako ni kule kutokiri kwamba hao wakoloni ndio walikuwa wa dini wakubwa wakikristo
kwani Tanganyika ya zamani ilikuwa pwani tu, haikuwa na mikoani? nijuavyo mimi, Tanganyika ya zamani ilijaa waislam upande wa pwani, na wapagani waliochanganyana na wakristo mikoani huko. kuna route chache ambazo waarabu walipita kibiashara, huko ndiko walijenga uislam. angalia kwamfano route ya katikati, kuanzia bagamoyo, dodoma kondoa, tabora hadi ujiji kigoma, ni sehemu zile tu walipita waarabu walijenga uislam. nje ya hapo wamebaki wapagani hadi leo. kuna maeneo hapa tanzania unatembea kilimita hata 100 hukuti msikiti, huko mikoani. ni makanisa. kwahiyo ukisema Tanganyika ilikuwa ya waislam, ujue waislam walitawala tu pwani (along the coast), huko mikoani hawakuwepo hadi waarabu walipopita. na hata hivyo idadi yao sio nyingi kiivyo, wanaongezwa tu na Zanzibar, ukisikia waislam Tanzania ni asilimia fulani, jua na wazanzibar ambao wanakaribia 2m wapo ndani. wakijitenga na bara waislam watakuwa minority. trust me.
 
Na ww hutaki waislamu wajue kama wanamchango mkubwa kwenye uhuru na jinsi nyerer alivyofanya hila kuwadhulu.Ukweli unatabia ya ajabu sana hata ikichukua miaka 400 kufichwa ila utajulikana tu.Swali muhimu watu wenye akili wanalojiuliza hv Nyerere ni peke yake aliyeleta uhuru wa nchi hii?Jibu hapana alikua na wenzake .
Swali wenzie ni akina nan hapo ndio kazi ilpo
kuna wakati nafikiria kwamba, kama kweli nyerere atakuwa alifanya hivyo, basi namshukuru sana sana, kwasababu kwa namna baadhi yenu hasa kina mohamed said mnavyotuchukia mngeshika nchi mapema, sasaivi Tanzania ingekuwa ya kiislam. na mngeshatuchinja wote. asante nyerere (kama kweli alifanya hivyo). hivi kwa chuki zenu za aina hii mngetawala tungeishi kweli. Ashukuriwe Mungu kwa kumtumia Nyerere.
 
Kasome historia vizuri. Nyerere alimshinda Abdul Sykes kwa Kura kwenye ukumbi wa annatouglo Dar. Kama Sykes angeshinda siku hiyo basi ndio angekuwa Baba wa Taifa leo.
Economist.
Bahati mbaya sana Mwalimu hakueleza vipi aliingia katika nafasi ya juu ya TAA.

Mwalimu hakupata hata kusema kuwa aliingia katika uongozi wa TAA mwaka wa 1953 kwa kugombea nafasi hiyo dhidi ya Abdul Sykes aliyekuwa Secretary na Act. President wa TAA kuanzia 1951.

Mwalimu hakupaa kusema kuhusu uhusiano wake na Abdul Sykes na Hamza Mwapachu.

Hii ni historia ambayo kwa mara ya kwanza ilielezwa na Judith Listowel katika kitabu chake, ''The Making of Tanganyika,'' (1965).

Mimi nilipokuja kuandika kitabu cha Abdul Sykes (1998) ndiyo nikaeleza kwa kirefu kuhusu kutafutwa kiongozi wa TAA 1953 na kuundwa kwa TANU 1954.

Katika hili wazalendo wawili, Hamza Mwapachu na Abdul Sykes walihusika sana.
Abdul yeye alitaka nafasi ya rais wa TANU ikamatwe na Chief David Kidaha Makwaia.

Hamza Mwapachu yeye mtu wake alikuwa Julius Nyerere.

Hawa watu wawili walipokubaliana kuwa Nyerere ndiye achukue uongozu wa TAA 1953 na iundwe TANU 1954 hili jambo likawa ndilo limepita.

Na Abdul alisaidia Nyerere kushinda uchaguzi wa rais wa TANU uliofanyika Arnautoglo tarehe 17 April 1953.

Kamati ya ndani ilikubaliana kuwa Nyerere ndiye atakaeongoza harakati za kudai uhuru chini ya TANU kwa hiyo achaguliwe katika uchaguzi ule wa 1953 na 1954 TANU inaundwa na Mwalimu ataongoza harakati za kudai uhuru.

Katika uchaguzi ule Julius Nyerere ''alishinda'' na uoongozi wa TAA ulikuwa kama hivi:

J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias naWaziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer na Ally K. Sykes Assistant Treasurer; Wanakamati Dr. Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.[1]

[1] Tanganyika Standard, 19 th June 1953.

Sasa hapo hakuna suala la Abdul Sykes kushinda uchaguzi ule kwa kuwa makubaliano yalikuwa Nyerere akabidhiwa uongozi 1953 TANU iundwe na Nyerere aongoze mapambano ya kudai uhuru.

Ndiyo sababu unaona TANU ilipoundwa mwaka wa 1954 kadi no. 1 Julius Kambarage Nyerere, kadi no2. Ally Kleist Sykes na kadi no. 3 Abdulwahid Kleist Sykes.

Bahati mbaya sana Nyerere hakupata kueleza historia hii.
Sijua kwa nini.

1648147186885.png
 
kuna wakati nafikiria kwamba, kama kweli nyerere atakuwa alifanya hivyo, basi namshukuru sana sana, kwasababu kwa namna baadhi yenu hasa kina mohamed said mnavyotuchukia mngeshika nchi mapema, sasaivi Tanzania ingekuwa ya kiislam. na mngeshatuchinja wote. asante nyerere (kama kweli alifanya hivyo). hivi kwa chuki zenu za aina hii mngetawala tungeishi kweli. Ashukuriwe Mungu kwa kumtumia Nyerere.
Chapwa...
Unasema tu maneno kama yanavyokuja akilini bila kufikiri na kujua athar ya maneno yako.

Tuwe pamoja hapa na usome historia ya wazee wangu vipi walimpokea Nyerere na wakamweka mbele kama kiongozi wa harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Utatujua na huenda ukabadili fikra zako.
Angalia picha hiyo hapo chini:

1648147545143.png

kwani Tanganyika ya zamani ilikuwa pwani tu, haikuwa na mikoani? nijuavyo mimi, Tanganyika ya zamani ilijaa waislam upande wa pwani, na wapagani waliochanganyana na wakristo mikoani huko. kuna route chache ambazo waarabu walipita kibiashara, huko ndiko walijenga uislam. angalia kwamfano route ya katikati, kuanzia bagamoyo, dodoma kondoa, tabora hadi ujiji kigoma, ni sehemu zile tu walipita waarabu walijenga uislam. nje ya hapo wamebaki wapagani hadi leo. kuna maeneo hapa tanzania unatembea kilimita hata 100 hukuti msikiti, huko mikoani. ni makanisa. kwahiyo ukisema Tanganyika ilikuwa ya waislam, ujue waislam walitawala tu pwani (along the coast), huko mikoani hawakuwepo hadi waarabu walipopita. na hata hivyo idadi yao sio nyingi kiivyo, wanaongezwa tu na Zanzibar, ukisikia waislam Tanzania ni asilimia fulani, jua na wazanzibar ambao wanakaribia 2m wapo ndani. wakijitenga na bara waislam watakuwa minority. trust me.
Chapwa...
Hili suala ni nyeti sana lakini nitakuwekea yale niliyoandika katika kitabu cha Abdul Sykes (1998) uongeze maarifa yako:

Religious Distribution in Tanzania

In order to appreciate the impending danger we need to agree that Muslims are a majority[18] in Tanzania and in any civil upheaval large numbers carry psychological advantages.

The government has over the years been making deliberate efforts to conceal this fact and to portray to the world that Muslim-Christian religious distribution is more or less the same and at times to give an impression that Tanzania is a Christian nation and Muslims are a minority.

[19]The government to say the least has been very evasive on this question.[20] When the government went into its first census after independence the government did not envisage that the results would show Muslims as a majority. In the 1957 census Muslims outnumbered Christians at a ratio of three to two. Ten years after in 1967, in the post-independence census Muslims were 30%, Christians 32% and local belief 37%.

Reasons were not given for this sudden decrease of Muslims or the growth of pagans. It is on record that the 1967 statistics were doctored to show that Muslims were trailing behind Christians in numerical strength.[21]D.B. Barret gives statistics which show Muslims as a minority: Muslims 26%, Christians 45% and local belief 28%. Tanzania National Demographic Survey figures for 1973 have Muslims at 40%, Christians 38.9% and local belief 28%. Africa South of the Sahara shows that Muslims are a majority in Tanzania at 60% this figure has remained constant in all its subsequent publications since 1991.[22]
 
Kazi kweli kweli! 20/70?
ni udini udini tu.
Naanza kuamini kuwa Manchurian wapo na sio hadithi za abunuasi.
 
Kazi kweli kweli! 20/70?
ni udini udini tu.
Naanza kuamini kuwa Manchurian wapo na sio hadithi za abunuasi.
Syll...
Harakati za kudai uhuru zilikwenda vizuri sana kwa umoja na mshikamano wa hali ya juu kabisa.

Ikutoshe tu kuwa kwa kuwa madai mengi dhidi ya Waingereza yalikuwa yakipitishwa kupitia African Association viongozi wa wakati ule Mzee bin Sudi President na Kleist Sykes Secretary waliona si siwa walitaka AA isiguswe na hisia za Waislam na Uislam ibakie "apolitical."

Kwa ajili hii wakaunda Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika mwaka wa 1933.
Bila ya kuijua historia hii utahangaika sana.

Hutojua kwa nini leo tumejikuta katika hali hii.

Unatakiwa ujue kwa nini Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU alifukuzwa chama mwaka wa 1958.

Unatakiwa ujue historia ya Sheikh Hassan bin Ameir na Sheikh Suleiman Takadir katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ujue historia ya kupigwa marufuku EAMWS nk. nk.
Vinginevyo hakika utahangaika.

Bahati mbaya tunajifanya kama vile historia hii na watu hawa hawakupata kuwepo katika kupigani uhuru wa Tanganyika wala hawakupata kuwa viongozi wakuwa katika TANU.

1648226178234.png

Mzee bin Sudi aliishi hadi 1972 na nimuasisi wa African Association 1929.
 
Back
Top Bottom