Huwa nawashangaa sana hawa watu wanaosema mtu mweusi ni mteule, sijui mzungu anaujua ukweli hivyo anamharibu mweusi..
How comes mteule akawa kilaza kabisa, yaani hata kujikwamua kwa vitu vidogo hawezi...
Ni kawaida ya mtu mweusi kulaumu pale anaposhindwa jambo, hutafuta wa kumlaumu au kumuachia Mungu.
Tawala zetu ni vibaraka wa wazungu.
Kila sera inayopitishwa na mzungu lazima ifuatwe, na mara nyingi inakuwa si kwa maslahi ya wananchi.
Sera ya elimu ni hovyo, waliofeli ndio walimu,
Elimu yetu inazalisha watu wasiozalisha ( makasuku) Si ajabu Afrika kumkuta daktari bingwa wa binadamu anagombea ubunge. Maslahi makubwa yapo kwenye siasa.
Angalia sera za afya, kila dawa tunazoamriwa.kutumia sisi tunatumia tu bila tafiti. Mfano maralia na Covid nk.
Kilimo tumeshauriwa kuachana na mbegu zetu, tumeletewa madawa na mbolea ambayo kimsingi yameongeza mimea kushambuliwa na magonjwa. Nayo tumepokea.
Afrika akitokea kiongozi mwenye kwenda tofauti na sera za whites lazima atauwawa.
Demokrasia ya mzungu ndio adui mkubwa wa Afrika.
Waafrika kwa ujumla wasilaumiwe mambo yote yanaamriwa na wanasiasa. Ambao wengi wao bongo zao zimejaa kamasi.
Wanacho waza wao ni ufisadi na kujilimbikizia mali na wala sio maendeleo ya taifa. Na wala hawawazi huko mbeleni taifa litakuwaje.
Wamejaa ubinafsi uliotukuka. Sio ajabu kiongozi wa Afrika kuiba nchini kwake na kwenda kuwekeza ulaya na arabuni.
Ni aibu na fedheha kuzaliwa mwafrika mweusi.
Viongozi Afrika ***** zenu!