Weka picha ya gari namba 'E' kuonesha utajiri wa Tanzania

Weka picha ya gari namba 'E' kuonesha utajiri wa Tanzania

Ukiacha siasa alichosema Mwigulu alikuwa sahihi, watu hawawezi nunua gari kwa fujo hiv kama hakuna pesa mtaani,
Tazama jinsi namba E inavyokwenda speed, tena sio gari za ovyo, ni Subaru, dualis, outlander, Mazda C5 na nyingine za hivyo
Lini watu waliacha kununua magari, lini watu waliacha kukesha bar hata bia zipande bei.
 
Halafu humu kutwa kuwaponda wasioenda shule eti wana mawazo mgando wakati huo wasomi wenyewe kama wakina mwigulu wao wanaupima uchumi kwa namba E za magari....hivi hata unapoambiwa libya kuna vita unadhani kila sehemu?
 
Amekuambia yeye ni la saba B na hawezi kushindana na mwenye PhD. Ukitafakari alichoandika utagundua yeye sio mjinga bali ametumia lugha flani hivi ya kuwakilisha.

Ukimjua huyu mwenye PhD alisema nini kuhusu gari namba E nadhani ndo uta-conclude kama mleta uzi ni mjinga au mwerevu
Ila huyu PhD wetu ana upeo mdogo sana wa kufikiri tena sana elimu yake ni sufuri kabisa
 
Ukiacha siasa alichosema Mwigulu alikuwa sahihi, watu hawawezi nunua gari kwa fujo hiv kama hakuna pesa mtaani,
Tazama jinsi namba E inavyokwenda speed, tena sio gari za ovyo, ni Subaru, dualis, outlander, Mazda C5 na nyingine za hivyo
PhD nyingine hii
 
Eeh!!! Ina maana jamiiforum ina watu wajinga kiasi hiki???
Ulisoma fasihi?
Miaka ya nyuma Kuna mzee alokuwa anatembea na taa ya chemli mchana wa jua kali akidai kuwa anamtafuta kiongaozi atakayetukomboa Watanzania na bado hajamuona!! Kwa miaka hiyo alionekana mjinga ila Hali halisi ni kuwa had leo hatujapata kiongaozi wa kweli
 
Lini watu waliacha kununua magari, lini watu waliacha kukesha bar hata bia zipande bei.
Kama nchi bado tunajadili walionunua magari second hand yenye namba E. Safari bado ndefu sana, tena anayeongea ni Waziri wa Fedha.
 
Ukiacha siasa alichosema Mwigulu alikuwa sahihi, watu hawawezi nunua gari kwa fujo hiv kama hakuna pesa mtaani,
Tazama jinsi namba E inavyokwenda speed, tena sio gari za ovyo, ni Subaru, dualis, outlander, Mazda C5 na nyingine za hivyo
Wengine vichwa vyenu huwa mnavitumia kama dispenser ya kuhifadhia mate tu, ni jambo jema pia
 
Mimi nimeishia la saba B, hivyo siwezi bishana na mwenye PhD. Leo nilikuwa natembea nikaona gari kadhaa za namba E, nimezipiga picha. Kwa wengine kama mkiyaona yapigeni picha kuonesha utajiri wa watu wa nchi hii.

Pia kama ukipita bar au club piga picha nyomi tuone utajiri wa nchi.
View attachment 2929103
Na hata elfu kumi kumi zimekuwa nyingi mtaani. pHD zetu ni Kali Sana kuliko za std
 
Mimi nimeishia la saba B, hivyo siwezi bishana na mwenye PhD. Leo nilikuwa natembea nikaona gari kadhaa za namba E, nimezipiga picha. Kwa wengine kama mkiyaona yapigeni picha kuonesha utajiri wa watu wa nchi hii.

Pia kama ukipita bar au club piga picha nyomi tuone utajiri wa nchi.
View attachment 2929103
Yaani hakika wewe ni darasa la saba sana. Nakumbuka awamu ya nne waswahili wanaongoza kina sophia simba wanasema nchi iko vizuri kiuchumi maana jijini dar magari mengi hadi msongamano wa magari.
 
Ukiacha siasa alichosema Mwigulu alikuwa sahihi, watu hawawezi nunua gari kwa fujo hiv kama hakuna pesa mtaani,
Tazama jinsi namba E inavyokwenda speed, tena sio gari za ovyo, ni Subaru, dualis, outlander, Mazda C5 na nyingine za hivyo
Tabaka la wenye uwezo kumiliki gari, achilia mbali hiyo namba E, ni wangapi kwenye nchi hii??
 
Kama nchi bado tunajadili walionunua magari second hand yenye namba E. Safari bado ndefu sana, tena anayeongea ni Waziri wa Fedha.
Hizo ndo zinaitwa cheap politics.

Kuna watu vijiweni hawaelewi, wanatumia hoja ya huyo Magulu sijui njigulu kupotosha watu.
 
Back
Top Bottom