Wema atakwa kujifunza kuweka breki mdomoni

cute b

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2014
Posts
16,878
Reaction score
34,276
SALAMU nyingi zikufikie mrembo usiyechuja umaarufu tangu mwaka 2006, Wema Isaac Sepetu ‘Madam' vipi uko poa? Mishemishe zinakwendaje?

Ukitaka kujua afya yangu, mimi namshukuru Mungu kwani ni mzima, hofu na mashaka ni kwako wewe uliye mbali na upeo wa macho yangu. Kitambo kidogo kimepita sijakuona lakini naamini u-mzima wa afya.

Mbali na kukusalimia, dhumuni la barua hii ni kutaka kukumbusha juu ya umuhimu wa mdomo wako kuwa na staha. Kuna vitu vya kuzungumza lakini kuna ambavyo vinapaswa kuwekwa ‘spea'.

Binafsi sikufurahishwa na namna ambavyo ulimpa maneno makali aliyekuwa rafiki yako, Kajala Masanja kupitia kipindi cha televisheni wiki iliyopita.Si busara kumtusi mwenzako hadharani kiasi kile. Hata kama amekukosea kiasi gani, wewe ni mtu maarufu unapaswa kuhakikisha kile unachokizungumza kitakuwa na matokeo gani mbele ya jamii inayokuzunguka.

Ugomvi wenu wewe na Kajala una historia ndefu, kibusara hakukuwa na sababu ya kuendeleza mjadala ambao hata watu tayari walishaanza kuusahau. Vitabu vya dini vinatufundisha, kusamehe na kusahau.

Nilishawahi kukuandikia barua huko nyuma, nilikusihi usamehe hili suala liishe. Nilisema hivyo kwa sababu mara kadhaa Kajala ameshaonesha nia ya kutaka yaishe lakini wewe ukaendeleza vita. Kwa nini usimsamehe? Mbaya zaidi hata huyo mwanaume ambaye inasemekana alikuibia naye nimetonywa kuwa ameshaachana naye.

Nyinyi mlishibana kama marafiki wa kuambiana kila kitu, la kwako la Kajala na la Kajala la kwako watu wanashindwa kuwaelewa kama kweli mlishibana kwa nini msikae na kuanza ukurasa mpya?

Sijawahi kumsikia Kajala anakuzungumzia vibaya lakini wewe kila siku unamsema. Unafikiri yeye hana mabaya yako? Akiyaanika hadharani utafurahi? Haiwezi kuwa sawa.Nakulaumu wewe zaidi katika hili maana historia inaonesha haudumu na marafiki. Uliwahi kuwa na urafiki na kina Jack wa Chuz, Rose Ndauka, Jamila na wengine kibao lakini wote uliwaacha njiani.

Kama hiyo haitoshi, Aunt naye mmedumu kwenye ushosti kwa muda mrefu lakini naye pia miezi kadhaa iliyopita mlitofautiana na sina hakika kama hadi sasa mpo sawa kama zamani japo mlipatanishwa.

Nikusihi, badilika. Kuwa na staha, chunga sana kauli zako kwani wewe unaheshimika katika jamii.

Nikushukuru kwa kunisoma!

Mimi ni kaka yako,

Erick Evarist..
 
Reactions: PNC
Amekusoma,amekuelewa lakini kwa upuuzi wake hatozingatia
 
Sema tu sasa namsamehe badala ya kujiandikia thread yote. We msamehe mwenzako hakuna atakayekulaumu kwa hilo. Huna sababu ya kuandaa mazingira.
 
Tabia kama ngozi..huezi kubadil!!! Ndo kashajizoelea kuropokwaa..!! We si unamuona mama ake alivyo?? Unategemea mtoto atakuajee
 
Mbunge mtarajiwa ahaahahahahaaaa!!woooooiyiiii!kutoka Kikatiti mpaka usa river,tigo wamefikaaaaaa!
 
Katika swala la speedgovernor ya mdomo, Wema sepetu na Nassib Abdul wanahitaji makufuli kabisaa


yaan umeniuaaa dadeeekiii,,,HIV kwanza umejiandika wewe kabla sijakuchongea ban
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…