binti kiziwi
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 11,201
- 28,642
Bajeti inajadiliwa na nani kule, hakuna mtu bungeni mkuu! Watu wote wanapigania roho zao majimboni. Spika hayupo, Naibu Spika hayupo, Mawaziri hawapo! Wamebaki manaibu mawaziri wachache sana. Bajeti ya nchi inajadiliwa lakini wenye dhamana hawapo. Siamini hata kama waziri wa fedha yupo manake namuona Malima tu huku Mwigulu akitafuta wadhamini mikoani. Waziri Mkuu anasaka wadhamini, mawaziri lukuki wanaska wadhamini. Serikali kama haipo Bungeni ma wabunge kama hawapo Bungeni. Siku ya kupitisha bajeti itapidi wapige kura kwa simu/whatsapp kama zile kura za Bunge la Katiba.
Jana kwa idadi yao nadhani walikuwa 20 tu, teh teh.