Wema Sepetu, Mr. Blue, TID, Recho wahusishwa na Dawa za Kulevya. Watakiwa kuripoti kituo cha Polisi

I hope jamaa ana ushahidi sio hear say za kimtaani
 
MAKONDA NGOJA KWANZA......


tuachane na habari za hao dagaa wa ngada

hebu zungumzia matokeo ya kidato cha NNE kwa mkoa wako mheshimiwa rais wa dalisalama
 
Hivi hawa watu ambao wanatuhumiwa kila mara na huyu mwanadada waliahawahi hata kuchunguzwa kweli??
Kwani ye nani mpaka amkisema jambo lenye ukakasi lichunguzwe
 
kwa mantiki hiyo majambazi wanaokamatwa na silaha nao wasitangazwe kwakuwa hawajawa proven/hukumiwa na mahakama kuwa ni majambazi.... kutaja sio kosa ndugu.... na watuhumiwa sio wahukumiwa na ndio maana kawaita kukutana nao kituo cha polisi

Majambazi umesema ni red handed.
Hawa wengine hakuna ushahid at hand...sio njia nzuri kuwachafua watu kwenye media....
Ingekua yeye ametangazwa na raia anahusika unadhani huyo mtu angepona...
 
Pia mi nadhani huyu jamaa kaanza emu tumpe muda tuone atakapoishia....Mungu yu mwema hata mbuyu ulianza kama mchicha....
Mimi kanifurahisha kwa hao akina makomeo na swai,hao maafande wamekuwa wakionea sana wanyonge mitaa ya kinondoni
 
Embu afanyie kazi swala la elimu hususan shule za gavoo maana sio kwa kiwango hiki cha kufeli,arudishe hadhi za akina jangwani azania
Atarudishaje wakati ampo tayali kupokea mabadiliko zaidi ya kukosoa
 
Stori hizi mrangi huwa zinamhusu sana hapa, je hawa waliokamatwa au wanaotuhumiwa ndio tuliokuwa tukiwajadili miaka yoteeee............hapa JF?Ikiwa kwenye orodha wale tuliokuwa tukiwajadili hapa hawapo je wameshaacha?
 
I hope jamaa ana ushahidi sio hear say za kimtaani
Kuna wale wapakistan walikamatwa na kilo za kutosha tu as ushahidi, na wakaachiwa hadi leo hakuna aliyewajibishwa.Ukimkamata TID ukawaachia wapakistani walioingiza hapo hupambani na unga.Na hadi leo hakuna mtu aliyetiwa hatiani kwa uzembe ule wa wale wapakistani KUTOROSHWA,hawakupaa angani wale wamepita kwenye entry ya kawaida tu
 
Safi saana makonda...kwa hili nitakusifu milele
 
Kila kitu haramu huwa haramu pale unapokamatwa nacho lkn kama haujakamatwa nacho basi bado ni halali,sasa kati ya hao waliotajwa mpaka kuthibitisha hatia yao mpaka kipatikane kidhibiti
 
Wengi naona mnawatetea sijui mpaka wakutwe na vidhibiti ndo watiwe hatiani. Ila hao kumbukueni ni watumiaji, na kama ni watumiaji those stuffs zipo damuni so vidhibiti wanatembea navyo miilini mwao. Ni swala la kuwapeleka hospital na kuwapima, kingine ni kumuweka under supervision kwa saa 48 ama zaidi. Kama ni mtumiaji, hawezi kaa saa 48 bila kuwa high.

Ila swala hapa naona halitatuliwi kwa ukubwa wake. Kuna list ipo ikulu wayback ya wafanyabiashara wa hii kitu. Ni kwenda kuifukua na kuanza kudeal nao. Naamini sifa mojawapo ya serikali ni mkono mrefu, haishindwi jambo ikiamua kutumia mikono yake mirefu. Sema tuu mashaka yaliyopo ni kama je kweli wana nia ya dhati kutokomeza tatizo kwa kudeal na watumiaji badala ya waingizaji.? Ngoja tuone hatima ya hili jambo.

Kusema ukweli vyombo vya ulinzi vinafahamu namna hii biashara inavyofanyika. Kama haifahamu kuna haja ya kujitathmini namna vinavyofanya inteligence gathering. Haiingii akilini tones of heroine ziingie nchini zisifahamike.

Way back, nadhani ni 2014 kuna shehena kubwa sana ilikuwa inazagaa mitaa ya pangani baada ya kuwa umetoswa na kutelekezwa baharini, kwa jinsi trend ilivyokuwa ile shehena yaweza pata hata tani moja ama zaidi. But ile issue ilienda kimyakimya na hakuna hata aliyekamatwa, which means mzigo wote uliwafikia walaji mitaani. Gari binafsi zilikuwa zinatiririka pangani kwa kipindi hicho kufuata mzigo kuliko kipindi chochote kile.
 
Sure sio issue ndogo hii
 
Naunga mkono hoja ya mh makonda kwa asilimia miamoja ni mwanzo mzuri wa kupambana na hili genge la waharifu na ikiwezekana aombe tu kwa mh raisi tu adopt strategy za bwana mkubwa wa ufilipino bwana Rody" Roa Duterte
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…