Wema unaofanya ukiwa Arusha kamwe hautafunika uovu uliofanya ukiwa Dar es Salaam!

Wema unaofanya ukiwa Arusha kamwe hautafunika uovu uliofanya ukiwa Dar es Salaam!

Watu wa Kolomije tunasema Amina kwa kila jambo.Kwamba Albert anajaribu kufanya kitubio akiwa Arusha lakini bado toba yake haikubaliki? basi itabidi afanye kuendeleza kufanya matendo mema Mungu atapokea toba yake
 
Ndio unasamehewa lakini matokeo ya ubaya uliotenda lazima uubebe ndio msalaba wako...

Mfano umengonoka ovyo uko ukapata ukimwi afu urudi kuomba toba,, ndio unasamehewa na Mungu but ukimwi utaishi nao mpaka ukuue.
Sio kila baya limpatalo mwanadamu ni matokeo ya dhambi alizotenda.
 
Imeandikwa; dhambi zenu zijapokuwa nyekundu kama damu mkitubu zitasafishwa ziwe nyeupe kama theluji! Muhimu hapo ni toba ya kweli kutoka moyoni.
Sisi wakatoliki tunadundishwa ukimkosea Mungu na wanadamu lazima.utubu kwa Mungu na wanadamu. Kujifanya unacheza mziki eti unapotezea haisaidii utacheza segere zote ila raha hutaipata.

Ni kwa mujibu wa Askofu Paul Ruzoka wa Jimbo Kuu la Tabora.
 
Ndio unasamehewa lakini matokeo ya ubaya uliotenda lazima uubebe ndio msalaba wako...

Mfano umengonoka ovyo uko ukapata ukimwi afu urudi kuomba toba,, ndio unasamehewa na Mungu but ukimwi utaishi nao mpaka ukuue.
We jamaa huu mfano umeeleweka sana.

Kama yule jamaa ambaye amezana kwenda Gym baada ya kufukuliwa kwa miaka mingi. Mungu atamsamehe kwa ushoga wake ila sio kwa madhara yale ataishi nayo milele
 
Ametubu,lakini haisaidia........................mkuu kwani mtu anapotubia kuna sauti inatoka mbinguni kuja duniani kuwambaia kuwa toba yake imekubalika au haijakubalika ?
 
Huyu bwana ni wazi anasumbuliwa sana na uovu aliofanya Dar es Salaam, ambao ulitia ndani kuteka na kuua watu. Sasa hili linamchanganya sana kiakili, na huenda anapata ndoto na maono yanayomvuruga kichwa kutokana na damu alizomwaga moja kwa moja au kuratibu mipango ya damu hizo kumwaga.

Amejaribu sana kwenda kutubia kwa mapadri, lakini haijamsaidia. Amejaribu sana kuwaomba wachungaji na hata mashehe wamuombee japo yeye si mwislamu, lakini bado haisaidii.

Kuna wakati taswira za uovu aliofanya zikimjia analia kama mtoto. Anajitahidi kwa kila njia kushiriki mambo ya kidini, lakini haisaidii. Damu alizomwaga zinazidi kumwandama tu. Akiona watu ambao ni kama wazazi, wake, au watoto, anakumbuka kuna mtu alishiriki kumwaga damu yake na kuwanyima hao watu huduma na msaada kutoka kwa huyo mtu. Inamchanganya sana, na kutaka kuwasaidia kama namna ya kupunguza uzito wa maumivi ya mambo aliyofanya. Kuna wengine hata ameanza kuwaita rafiki zake, akijua wazi ilikuwa awafutilie mbali.

Sasa amekuwa na fikra kwamba akiwafanyia wema kina baba na kina mama ambao ni kama wazazi wa wale aliomwaga damu zao, au wale ambao ni kama wake wa aliomwaga damu zao, labda atapata unafuu fulani, kwamba wema huo utasaidia kufunika uovu aliofanya akiwa Dar es Salaam. Kuna wakati mambo yalimzidi hadi ikaamuliwa apumzike kwa muda.

Nataka nimwambie wazi, damu alizoshiriki kumwaga akiwa Dar es Salaam zitamwandama siku zote, na hakuna kuombewa na wachungaji wala mashehe kutakakomsaidia. Wala hakuna wingi wa wema atakaofanya utafunika uovu aliotenda huko nyuma. Kuna kila dalili kwamba anavurugikiwa akili, na nimwambie wazi, hizo ni dalili za mwisho mbaya unaomsubiri. Jambo moja tu litakalomtoa katika kuchanganyikiwa aliko nako ni kukiri hadharani na kwa familia alizoziathiri kwa uovu wa aliyotenda na kuomba msamaha, ikibidi hata aende jela. Akifanya hiyo toba ya kweli ndipo Mungu anaemtafuta kwa bidii atakuwa tayari kumpokea. La sivyo tatizo la afya ya akili linamnyemelea, na huenda wengine wakahisi ni bora apotezewe kabla hajaanza kutoa siri.
Uzi mzuri sana.
 
Huna tofauti na nyumbu ambao wataona mwenzao analiwa na simba na kuangalia tu kwa kushangaa, kisha wakaendelea kula, kama vile kusema mwacheni simba aendelee kula, na kusahau kuna siku itakuwa zamu yao kuliwa!
Endapo Ni Kweli Alifanya Mabaya (Maana hakuna uthibitisho) na Sasa anafanya Mema, Basi Tuhesabu Mema yake.
Utusamehe kama na sisi tunavyosamehe waliotukosea..

Yona aliona wivu kwa Watu Wa Ninawi kufanya toba na kusameheea mahali alipodhani wangehukumiwa.

Mbinguni malaika wote hufurahi mwenye dhambi mmoja anapotubu.
 
Ametubu,lakini haisaidia........................mkuu kwani mtu anapotubia kuna sauti inatoka mbinguni kuja duniani kuwambaia kuwa toba yake imekubalika au haijakubalika ?
Jamaa anajipa Umungu. Wa kupokea na kukataa toba.Hakuna mwanadamu asiyekosea.Kutubu ni dalili kwamba anayetubu anajua yeye ni mwanadamu na anakosea.Huyu "malaika" anayeendelea kushutumu na kuhukumu aendelee na kazi yake ya kujua wanaosamehewa na wasiosamehewa.
 
Endapo Ni Kweli Alifanya Mabaya (Maana hakuna uthibitisho) na Sasa anafanya Mema, Basi Tuhesabu Mema yake.
Utusamehe kama na sisi tunavyosamehe waliotukosea..

Yona aliona wivu kwa Watu Wa Ninawi kufanya toba na kusameheea mahali alipodhani wangehukumiwa.

Mbinguni malaika wote hufurahi mwenye dhambi mmoja anapotubu.
Wewe ubaya wake ulikuathiri vipi? Kwa nini uwe mwepesi wa kuongelea kusamehe kwa mambo ambayo hayakukuumiza binafsi? Wewe angekuwa ni mume, au kaka au mtoto aliemdurumu haki ya kuishi ungesema haya unayosema hapa?
 
Jamaa anajipa Umungu. Wa kupokea na kukataa toba.Hakuna mwanadamu asiyekosea.Kutubu ni dalili kwamba anayetubu anajua yeye ni mwanadamu na anakosea.Huyu "malaika" anayeendelea kushutumu na kuhukumu aendelee na kazi yake ya kujua wanaosamehewa na wasiosamehewa.
Acha uongo
 
Jamaa anajipa Umungu. Wa kupokea na kukataa toba.Hakuna mwanadamu asiyekosea.Kutubu ni dalili kwamba anayetubu anajua yeye ni mwanadamu na anakosea.Huyu "malaika" anayeendelea kushutumu na kuhukumu aendelee na kazi yake ya kujua wanaosamehewa na wasiosamehewa.
Hujamwelewa. Anachomaanisha ni kwamba ametubu kwa mapadri, kaomba aombewe na wachungaji na mashehe, nk, lakini haijasaidia kumtuliza akili. Haimwondolei sense ya kuwa guilty na kumwaga damu za watu, ndio maana bado analia lia tu kama mtoto
 
Back
Top Bottom