Wengi hawajaielewa kauli ya Dkt. Ally Bashiru kuhusu CCM kutumia faida ya kuwa na dola kuendelea kubaki madarakani

mwana wa Tanzania, Wewe unafikiri kwanini Ali Bashir, Magufuli, Makonda, Profesa Majalala na Polepole huwa hawaeleweki mara moja wakiongea, hadi walazimike kila wakati kutolea ufafanuzi kuropoka kwao?

Maana yake Jamaa wanaoongoza dola kwa sasa ni Vilazer wa kutupwa
 
Incumbent ni neno la kiingereza neno la kawaida kabisa huyu aliyekufundisha jalalani aliposema wanategemea/kutumia Dola kubaki madarakani alimaanisha Polisi, Jwtz, TISS, kugawa vyeo kwa wastaafu wa hivyi vyombo kuvitumia kuumiza wapinzani kukamata kuua kama unataka utuaminishe kwamba CCM, wanatumia dola kama USA, lakini ukigundulika unakuwa impeached kama Trump, basi wewe utakuwa ni kilaza haswa kutoka jalalani

Kwa nchi za Africa ukisikia kutumia Dola maana yake Ni Lisasi kibao kwa Lisu, Kesi zisizo isha kwa wapinzani, kupotezwa kwa Ben Saanne, Mauaji ya Robert Ouko Kenya na hivi karibuni mauaji ya mkuu wa usalama wa ofisi ya makamu wa raisi Kenya

Hayo ndio matumizi ya Dola.

Pls do not insult our intelligence,usitake kutuaminisha kwamba hii demokrasia ya kwetu ni ya haki kama USA,Uk,
Unless unatafuta kuteuliwa,maana hizi njaa za vijana hatari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mwana wa Tanzania,
Mkuu usihangaike, akili ya Mbowe haiwezi kutafsiri logic za kisomi kama hawa,
Mbowe ni tapeli wa kisiasa ni wa kupuuzwa tu.
 
mwana wa Tanzania,
Kiongozi walio tafsiri kauli ya bashiru na mada yako hakuna utofauti, kipengele muhimu hapa ni matumizi ya dola katika kushinda ama kuendelea kubaki madarakani. Ni bahati mbaya sana hata we mwenyewe umekubali kwamba dola inatumika pamoja na tasisi nyingine za umma. Ingekuwa vizuri kama unge tuwekea na hivyo vifungu vya kanuni, taratibu na katiba vinavyo ruhusu matumizi ya dola kushinda ama kuendelea kubaki madarakani.
 
Mwanafunzi kasoma kafundishwa kingereza na mbaya zaidi kasoma Art ambayo msingi wake ni lugha. Mwalimu kamwambia "DOLA" au "STATE (organs)", yeye anajifanya kasikia INCUMBENCY.

Masikio ya mjinga ni hatari kwa ustawi wa jamii.
 
Sijui mchungaji Bagonza ufafanuzi wako atauona? Maana, anahitaji hili somo haswa? Usually his comments lacks political science elements!
Acha upuuzi. DOLA siyo INCUMBENCY. Dola ni state (kwa maana ya mamlaka za dola kama majeshi, polisi, watumishi wa uma, bajeti ya serikali nk.).
 
Hii inasidia kupata uelewa wa pamoja na haiwezi kubadili walio amua kuelewa kwa fikra hasi au chanya.Makundi yote mawili yapo sawa kutegemeana na upande wanaousadiki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Bila kamusi toka kwa wanafunzi Wake, Bashiru hotuba zake hakuna anayezielewa. Hata wamujini n a wasomi hawamuelewi, vipi huko kijijini?

Baada ya hotuba ni lazima watokee watafsiri, wakianza na neno :Nyie hamkumuelewa; ufafanuzi unafuatwa, Kazi kweli kweli..........
 
Wasomi wetu wanaonyesha udhaifu mkubwa wa kutambua mambo, wale wenye elimu ya chini au wasio na elimu rasmi wamekuwa waelewa kuliko wasomi wengi. Argument za wasomi zimekuwa za ajabu mno kuliko za watu wa kawaida. Shida iko wapi, tumekwama wapi au ni tamaa ya nafasi za uteuzi zinatesa wasomi wetu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukweli utabaki Kama ulivyo chama chochote kilichoko madarakani lazima kitumie Dola hasa kwa nchi za afrika
 
mwana wa Tanzania, Ni ngumu sana kuleta tafsiri uchwara ili kuwadanganya watu kwenye dunia ya leo.
Hizo ngebe zako zilifanywa enzi za mwalimu na watazama tv.

Tangu lini wanachama wa CCM wakawa na akili kutafsiri. CCM mna kichwa kimoja tu cha kutafsi mambo ambacho ni mwenyekiti wengine ni kusikiliza tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu mrundi bado anatumia dola kubaki?
 
Mpaka sasa haamini nguvu za Mungu alivyopindua meza haamini asipoangalia lazima apigwe stroke .maana haamini anaona kama anaota...na bado jeuri ya kuchezea pesa za walipakodi imeishaaa
 
Kwanza usimlishe Bashiru maneno. Alichosema Bashiru ni matmizi ya vyombo vya Dola kubakiza Serikali (siyo Chama) madarakani. Pili, umeibuka na kuwafanya wa-Tanzania wendawazimu wasioelewa chochote hata walichokisikia kwa masikio yao. Siku ingine uje na hoja zako zenye mashiko humu siyo kudandia kwa mbele gari iliyokwishanza safari mapema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…