Wengi mpaka leo hatujui kiliongelewa nini kwenye Ngangari ya Gangwe Mobb, mliojua tunaomba mtusaidie

Nilielrwaga kipindi hicho, sasa nimesahau.
Nyimbo nyingi na kazi za sanaa kwa ujumla hueleweka kwa wakati uliopo 1
 
Aisee nimetoka kapa.

Ila Gangwe Moh ilikuwa ni Musiclub matata sana.
 
Inspector Harun alitupiga sana kamba hata kwenye" mtoto geti kali" anakuambia " mtoto white,softy,black beauty,maji ya kunde ,chotara,uso usio na chunusi.

Sasa imagine huyo mrembo ana rangi gani au anakuwa anabadilibadili make up

Inspector style yake anapenda kurudia neno moja kwa misemo tofauti tofauti.

Mara vikaanza viboko ,bakora ,stick ,michalazo - Heka Heka za teacher.

Mtoto kila kitu kwao stock ,Beef Cow Kitimoto Pork - Mtoto wa Geti kali.

Kwenye friji ,friza vimiminika vya kumwagililu mpaka kusaza - Geti kali.

Chechela Segedansi Nondo Gereza ,inside ,Ndichi ,Ngome ,Lupango Kunapotekeza - Wanaoenda Jela ft LWP
 
Ila yeye na Nature inaonekana walikuwa wa uswahilini sana
 
Inspector Harun alitupiga sana kamba hata kwenye" mtoto geti kali" anakuambia " mtoto white,softy,black beauty,maji ya kunde ,chotara,uso usio na chunusi.

Sasa imagine huyo mrembo ana rangi gani au anakuwa anabadilibadili make up
mambo ya sanaa, mtoto mkali hadi kamtia kiwewe 😀
 
Utofauti wa rap katuni na rap zingine nini mkuu
Rap Nyingine Kila Mtu Anaweza Kuielewa InachoongeleA
Rap Katuni Ni Kwa Watu Maalum/Waliokusudiwa Tu
Hasa Wakazi Wa Temeke Mikoroshini, Mwembeyanga, Tandika
 
Oho ohoooo .
Maafande ndani ya track 1 huku Luteni huku Inspector angalia Lugha zao Sasa.
 
Rap Katuni,cha ajabu kipindi kile navuta nilikua naelewa kila kitu kilichoimbwa,ila sasa hivi ndio nagundua bangi ilikua inanidanganya😅
 
Inspector Harun alitupiga sana kamba hata kwenye" mtoto geti kali" anakuambia " mtoto white,softy,black beauty,maji ya kunde ,chotara,uso usio na chunusi.

Sasa imagine huyo mrembo ana rangi gani au anakuwa anabadilibadili make up
Vipi Nature alivyotupiga kwenye "inaniuma sana"
Na wenye kuhonga twelve million or six dollars..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…