econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 20,189
- 29,663
Huyu Wenje amejidhihirisha kuwa ana kazi Maalum ndani ya CHADEMA.
Kwanza yeye ndiye kamleta Abdul CHADEMA. Mivurugano yote unayoiona kwa Sasa imeletwa na Wenje baada ya pesa za Abdul kuingia kwenye chama. Leo kiburi Cha Kambi ya Wenje ni kwamba Kuna pesa walizonazo ndizo Kinga yao. Na pesa za Abdul ndizo zitakazo saidia kuwashawishi wajumbe wa mpigie kura Wenje na Mwenyekiti wake. Wenje asingemleta Abdul kwenye chama yote haya yasingetokea.
Pili, Wenje alitaka kumuingiza Lissu kwenye mtego wa Abdul. Tukumbuke ya kwamba Wenje ndiye aliyempeleka Abdul kwa Lissu. Maana nyingine ni kwamba, Lissu angekubali kuchukua pesa za Abdul Leo hii akina Wenje wangeitumia Kama silaha ya kummaliza kisiasa Lissu. Jiulize Kama kweli Wenje hajui protocali za serikali kuhusu malipo mpaka akaongee na mtoto wa Rais?. Tuwe wakweli. Cha msingi ni kwamba Lissu aliepuka huo mtego la sivyo Leo akina Wenje wangekuja Hadi na video za maongezi au stakabadhi za malipo. Yani Lissu alitumia akili Sana la sivyo wangemmaliza.
Tatu, Wenje yupo kumtoa Lissu kwenye reli. Baada tu ya kuchafuliwa kuwa mwenyekiti ya Kanda ya Victoria , ni Wenje huyo huyo alitangaza kugombea Umakamu Wenyekiti wa CHADEMA. Pamoja kwamba ni haki yake ya kichama, ila ilizua swali kwanini asijielekeze kwanza kwenye Kanda aliyochaguliwa ila anakimbilia kwenye umakamu uenyekiti?. Je ametumwa ili atumie fedha za Abdul kuhonga wajumbe ili afanikiwe kumtoa Lissu. Lissu kwa kujuaa mipango ya Wenje akajitoa kugombea umakamu uenyekiti na kugombea Uenyekiti. Sasa hapo ndipo kelele zikaanza.
Mwisho, Wenje anatumika kumtoa Pambalu kwenye reli. Pambalu alipotangaza kugombea Uenyekiti wa Kanda ya Victoria , Wenje akaibuka naye kutaka kugombea. Kama haitoshi, Wenje kamvamia Pambalu Nyamagana kutaka kugombea ubunge mwaka 2025. Yote ni kumtoa Pambalu kwenye reli na amefanikiwa kwa hilo.
Niwe mkweli, kitendo Cha WanaCHADEMA kuogopa kuchukua fomu za umakamu uenyekiti kisa kumuogopa Wenje na pesa Abdul, kinaonesha jinsi CHADEMA inavyoharibiwa na vibaraka wa CCM.
Kwanza yeye ndiye kamleta Abdul CHADEMA. Mivurugano yote unayoiona kwa Sasa imeletwa na Wenje baada ya pesa za Abdul kuingia kwenye chama. Leo kiburi Cha Kambi ya Wenje ni kwamba Kuna pesa walizonazo ndizo Kinga yao. Na pesa za Abdul ndizo zitakazo saidia kuwashawishi wajumbe wa mpigie kura Wenje na Mwenyekiti wake. Wenje asingemleta Abdul kwenye chama yote haya yasingetokea.
Pili, Wenje alitaka kumuingiza Lissu kwenye mtego wa Abdul. Tukumbuke ya kwamba Wenje ndiye aliyempeleka Abdul kwa Lissu. Maana nyingine ni kwamba, Lissu angekubali kuchukua pesa za Abdul Leo hii akina Wenje wangeitumia Kama silaha ya kummaliza kisiasa Lissu. Jiulize Kama kweli Wenje hajui protocali za serikali kuhusu malipo mpaka akaongee na mtoto wa Rais?. Tuwe wakweli. Cha msingi ni kwamba Lissu aliepuka huo mtego la sivyo Leo akina Wenje wangekuja Hadi na video za maongezi au stakabadhi za malipo. Yani Lissu alitumia akili Sana la sivyo wangemmaliza.
Tatu, Wenje yupo kumtoa Lissu kwenye reli. Baada tu ya kuchafuliwa kuwa mwenyekiti ya Kanda ya Victoria , ni Wenje huyo huyo alitangaza kugombea Umakamu Wenyekiti wa CHADEMA. Pamoja kwamba ni haki yake ya kichama, ila ilizua swali kwanini asijielekeze kwanza kwenye Kanda aliyochaguliwa ila anakimbilia kwenye umakamu uenyekiti?. Je ametumwa ili atumie fedha za Abdul kuhonga wajumbe ili afanikiwe kumtoa Lissu. Lissu kwa kujuaa mipango ya Wenje akajitoa kugombea umakamu uenyekiti na kugombea Uenyekiti. Sasa hapo ndipo kelele zikaanza.
Mwisho, Wenje anatumika kumtoa Pambalu kwenye reli. Pambalu alipotangaza kugombea Uenyekiti wa Kanda ya Victoria , Wenje akaibuka naye kutaka kugombea. Kama haitoshi, Wenje kamvamia Pambalu Nyamagana kutaka kugombea ubunge mwaka 2025. Yote ni kumtoa Pambalu kwenye reli na amefanikiwa kwa hilo.
Niwe mkweli, kitendo Cha WanaCHADEMA kuogopa kuchukua fomu za umakamu uenyekiti kisa kumuogopa Wenje na pesa Abdul, kinaonesha jinsi CHADEMA inavyoharibiwa na vibaraka wa CCM.