Wenye Akili tuliandika mno Kupinga Ujenzi wa hovyo wa 'Fremu Lugalo' tukapuuzwa, sasa hata Mama nae Boss wao 'wamekerwa' nao

Wenye Akili tuliandika mno Kupinga Ujenzi wa hovyo wa 'Fremu Lugalo' tukapuuzwa, sasa hata Mama nae Boss wao 'wamekerwa' nao

Kwani JWTZ wanashid gani hadi waruhusu fremu kujengwa Lugalo? Kwani pangebaki palivyo wangepungukiwa nn? Hivi hata wakienda mafunzo huko nje ya nchi hawaoni kambi za wenzao zilivyo?

Kwa hiyo wanataka wawe na groceries karibu na kambi?
 
Hazijakaa vizuri na pia nahisi kila mtu alijijengea Kwa utashi wake, hakuna designs
Na ni kwanini unajisi kambi ya Jeshi kiasi kile... Hao viongozi hawajawai tembelea ma-barracks ya wenzetu huko nje...hata hapo Rwanda wanatusginda...Barracks zina nidhamu na muonekano wake... leo hii mavikosi mengi ya jeshi yamejaa mabaa na mafrem... aibu tupu
 
Kuna vitu lazima viwepo kwenye nchi ya kistaarabu, haijalishi kama kuna 'watumiaji'. Na maeneo ya Mbezi kwenda Boko, wasomi wapo, watapata tu 'wateja'.

Wangejenga hata maktaba ya kuonyesha shughuli na kumbukumbu za mambo ya jeshi.
Ah kabisa,sisi wengine wakati wetu licha na kuwa na elimu ya kuungaunga
Lakini tulikuwa hatukosi kujichanganya maktaba ya taifa pale
Na American library mara umeenda kujiongeza British Council lkn yote kuongeza mbolea kwenye ubongo
Ila sahv watoto,vijana library hawana habari nazo,we waambie bongo fleva au kufatiia mambo ya wasanii ndiyo #1

Ova
 
Mabibo jeshin hazikuwa zikimilikiwa na jeshi, ni nyumba za NHC Kama za magomeni
Wajeshi walipewa kukaa miaka hiyo baadae ziliuzwa na aliyepewa nafasi ya kununua ni mpangaji aliyekaa muda mrefu zaidi, awe mjeshi au hawara wa mjeshi.
Kule sio makao ya wajeshi tena...labda tuwe tunatofautiana eneo tunalozungumzia ila ni hii mabibo ya kuingilia via soko la ndizi toka Moro road ama luhanga toka Mandela road
Hapa inaongelewa kambi ya jeshi iliyopo njia ya kwenda Kisukuru sio zile nyumba walizokuwa wanaishi wanajeshi kule Mabibo mwisho.
 
Back
Top Bottom