Wenye Dhamana watathmini changamoto za sensa na kutoa miongozo mipya

Wenye Dhamana watathmini changamoto za sensa na kutoa miongozo mipya

ego

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2013
Posts
1,620
Reaction score
1,407
Kwa mtizamo wangu zoezi la sensa limekuwa na "poor planning"

Mitaani watu wengi inaonekana hawajafikiwa na zoezi hili katika siku ya kwanza ya 23/08/2022.

Siku hii ndiyo ya mapumziko, watu wameshinda nyumbani na makarani hawakuonekana. kuanzia tarehe 24, kila mtu atakuwa kwenye shughuli zake na nyumbani zipo nyumba hakuna anayebaki nyumbani, nyingine wanabaki watoto au mtu wa kazi na nyingine anaweza kuwepo mzazi mmoja.

Tumeambiwa zoezi linaendelea kwa siku 7,

Je, tunafuatwa wapi? nyumbani au kwenye shughuli zetu?

Karani akimkuta mtoto mdogo au mfanyakazi atafanikisha sensa kweli?

Kama tunataka zoezi lipate takwimu halisi na si watu kufikia hatua wakaanza kuandika chochote ilimradi waonekane wamefanya kazi, basi ni lazima tufanye tathmini ya zoezi lilivyoanza na kutoa dira ya nini kifanyike
 
Mitaa ipi mpaka saa 12 jioni hawajapitiwa?

Mi wamepita asubuhi na mapema na wameniambia wenye mageti wengi hawafungui.nikaona ni kweli watu wanamageti n a hawajaweka kengele .so unaita na kugonga kimya.
 
Kwa mawazo yangu Mimi naona zoezi la sensa linaweza kufanikiwa sana kama wangetumika wajumbe wa nyumba kumi wa maeneo yote nchini maana wanawatambua wakazi wao kwa majina na makazi pia upatikani wao.
Watu nje ya wajumbe ya nyumba kumi ni wizi mtupu, hakuna kinachofanyika.
 
Kwa mawazo yangu Mimi naona zoezi la sensa linaweza kufanikiwa sana kama wangetumika wajumbe wa nyumba kumi wa maeneo yote nchini maana wanawatambua wakazi wao kwa majina na makazi pia upatikani wao.
Watu nje ya wajumbe ya nyumba kumi ni wizi mtupu, hakuna kinachofanyika.
Mbona unalazimisha wajumbe wa nyumba kumi?wanajua kutumia simu janja?wajumbe wengi ni wazee hii teknolojia wangechemka.Sensa sio kama kuhesabu namba.
 
Mbona unalazimisha wajumbe wa nyumba kumi?wanajua kutumia simu janja?wajumbe wengi ni wazee hii teknolojia wangechemka.Sensa sio kama kuhesabu namba.
Wanafundishika naamini, hawa ndio wanaojua wakazi wao wote nje ndani.
 
"Hili nalo muende mkalitizame,Mwanangu Dkt Albina Chuwa na Dada yangu Anneh Makinda"
 
Back
Top Bottom