Wenye "madingi" wakali tukutane hapa

Binafsi huwa sielewi kwanini awa wazee wetu walikuwa wakitufanyia ukatilii kwa kisingizio cha kukosa kwani walishindwaje kutumia kauli nzuri tu za kufundisha watoto yan ata kwa kutumia hekima za kidini.Nimelelewa na mzee wangu katika maisha ayo na kunifanyia matendo ya kikatilii imenipelekea kuwa mtu mwenye hasira sana nilipata ahueni ya mateso pale tu nilipofaulu form 6 kwenda chuo.
 
Me Mzee wangu sio mkalii ilaa Kila mmoja wetu alishawahii pigwaa Kipigoo Kimojaa tuu yanii ilikuwaa Ni kipigo cha maishaaa.... Ilaa mazaa alikuwa na vipigo vya rejarejaa aiseee Haipiti siku sijalaa vibaoo au kifinyooo.. Ila nlipofika Form One akaacha...!! Siku hizi sijui washazeeka Huwa tunaonywa kwa maneno tuu... Noo vipigo tenaa...
 
Huu ukatili ukipitiliza kiwango mm hadi leo nina kovu kichwani alinipiga na kitu kizito nilizirai na kupoteza damu tena hapo kwa msaada wa dada yangu aliweka mkono wake kichwani kwangu kunikinga lakini haikufua dafu, huwa najiuliza alidhamiria nn ile in zaidi adhabu kiukweli, mby zaidi alikuwa anamzingua maza sana, ila nilipofika tu 18 years tu nilimpa tabu sana na yeye ukatili wote aliweka mfukoni
 
Wamekulia maisha ya ukoloni na survival for fittest so ile colonial legacy ilikuwa kubwa sana plus jkt walikopitia,hata tuliosoma shule za zamani za bweni hali hiyo ilikuwepo kwa madent hadi walimu..ilikuwa hatari sana
 
Nimepitia hii thread ila nachoweza sema ni kwamba kwa kizazi cha watoto waliozaliwa miaka ya kati ya 1978-1995 wamekutana na shuruba za mababa wakatili na washenzi hicho ndo naweza kusema. Ni kweli tuliwaita baba zetu ila kwa jinsi nilivosoma hii thread wengi wa mababa walikuwa ni waonevu na walikuwa hawajui namna ya kumuadhibu mtoto.

Binafsi mi niseme tu baba yangu hakuwa mkali kabisa ingawa kuchapwa na mkanda kulikuwepo tena mara chache sana na sababu kubwa ilikuwa ni kukojoa kitandani ingekuwa sio hiyo sababu inawezekana maisha yangu ya utotoni yangekuwa ya raha mstarehe maana hata na hivo nilikuwa mpole sana.
 
Awa wazee wetu yani wao kupiga mtoto ni sifa kubwa kwao tena utakuta wanakaa kwenye vijiwe vyao wanaadithiana kwamba wanajua kupiga .Haya mambo yakupigwa pigwa ovyo bila sababu yalinijenga kuwa na tabia ya uwoga,hasira na roho ya chuki (nashukuru Mungu nilijtambua nkazpinga izo roho) kwn mzee alkua anapenda kuogopeka kuliko kuheshimika.Mbali na kupgwa wazee wanakuaga na kauli mbaya sana juu yetu tukiwa wadogo utakuta mzee anakuambia yan ww ata ukisoma vp hutokuja fanikiwa maishani na stokuja kula ata shiling yako halafu baadae anakuja kukulia eti uyu ndio mwanangu mpendwa msomi.
 
Sasa nyie vidingi vya miaka ya Leo eti mnapiga selfie na vitoto vyenu ndo maana vinaishia kuwa vishoga na vimalaya uchwara,mm lazima nimuenz mdingi alikuwa hatar sana ntasimulia simu nyingine
izo tabia za ushoga na umalaya ni hurka na pengine wazazi walishindwa kuwaandaa watoto kimalezi vizuri.unajua hakuna kitu kizuri km baba kuwa rafiki kwa watoto wako utaweza jua tabia zao kiundani toka wakiwa wadogo na hii itawakuza mpk wakiwa watu wazima watakua na upendo ule wa dhati kwako
 
Wamekulia maisha ya ukoloni na survival for fittest so ile colonial legacy ilikuwa kubwa sana plus jkt walikopitia,hata tuliosoma shule za zamani za bweni hali hiyo ilikuwepo kwa madent hadi walimu..ilikuwa hatari sana
yea kweli ilo nimeliona mwenyewe
 
Hizi ni hadithi za miaka hii,mbona die wengine wazazi wetu walikuwa ni wakali sana lakini Tania zetu walizifahamu na kizidhibiti bila kuwa na mazoea ya kijinga jinga
 
Hahahaa dah
 
Wazee wazamani walikua hawana tofauti na wakoloni asee
 
Hizi ni hadithi za miaka hii,mbona die wengine wazazi wetu walikuwa ni wakali sana lakini Tania zetu walizifahamu na kizidhibiti bila kuwa na mazoea ya kijinga jinga
Mkuu kuna ule ukali wa kawaida tu ambao ata kwny dini unaelezewa ,huu unaoelezewa apa na wadau kwa kiasi kikubwa ni ukatili huwezi mpiga mtoto mpaka anazimia afu unasema ni fundisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…