Wenye "madingi" wakali tukutane hapa

Wenye "madingi" wakali tukutane hapa

Hakuna mtu alikuwa na dingi mkali kanda ya kati kama mimi.

Yani Tabora, Dodoma na Singida nna uhakika mzee wangu ndio alikuwa mzee mkali kuanzia miaka ya 1976 mpaka alipofariki mwaka 1997.

Mzee alikuwa fundi umeme, ndani alikuwa na nyaya za umeme za kutosha siku ukifanya kosa anachukua nyaya anaikunja mara mbili anaanza kukupa kichapo. Ukishika umefuta

Maumivu ya nyaya ya umeme yasikie ndugu, ya mkanda yanasubiri sana. Maumivu ya nyaya nadhani ilibaki kidogo yafikie kwenye maumivu ya mapenzi (hahaha, joke)

Tulikuwa na choo na majani, siku moja nikawa nachezea kibiriti nikachoma choo then moto ukaenda kugusa kenchi za nyumba ashukuriwe Mungu majirani waliwahi kabla moto haujapamba lakini aliporudi mzee chamoto nilikiona, nilikuwa siwezi kukaa wiki nzima mfululizo kalio zimevimba balaa.

Pamoja na yote lakini nakukumbuka sana mzee wangu (RIP).

We mzee wako alikuwa mkali? tupe story
Kwa nini alikuwa mkali?
 
Nakumbuka nilikuwa napenda sana kutengeneza manati.sasa kama mnavyojua manati yanatakiwa yawe na like kingozi cha kushikia jiwe,na lazima kiwe kilaini.sasa bwana huku na huku nikatafuta ngozi bila mafanikio.akili ikanituma nikakate kiatu cha baba anachokipenda kuliko vyote.kilichotokea alivyorudi huwa ctak kukumbuka maana alinipa kichapo kiwango cha lami.
 
Mzee wangu alikua mtata ila hamzidi kaka yake ambae ni baba mkubwa aisee kwanza nililijua jina halisi la baba mkubwa nikiwa umri umeenda ila nilijua jina la baba mkali alikua akija kusalimia home yeye ndo anakua kama baba mwenye nyumba anapiga mkwala mpk mdgo wake aisee kile kchwa balaa watoto wake walikuwa mamenyooka kama nguo ya kamanda siro kwake kulikua na taratibu ambazo kamwe hazivunjwi aisee apumzike kwa amani
 
Mkuu Raphael wa Ureno, nimecheka sana, najua ushapoa sasa hakuna haja ya pole.

Kibishi tu sasa hivi nikimtazama huwa naona kama Bro wangu hana noma, Mara ya Mwisho ananipiga ilikuwa niko Darasa la nne, alikuwa yupo safarini ila asubuhi aliniita chumbani akanipa majukumu ya kufanya, Nimeamka tu nikaenda kusakata kabumbu nikijidai Maradona hadi saa 12 jioni ndipo Maradona anarudi nyumbani akamkuta baba yake kafika hakuna kazi yeyote iliyotendeka.

Kipigo cha Kufa Mbwa kikamhusu Maradona, Kilichoniokoa niliona nikiendelea kulia na kupiga kelele nitakufa kwa ngumi na makofi ya Baba yake Maradona basi Nikajidai nimezima anapiga sitikisiki wala kugeuka kapiga kama dakika 1 kashituka, akajua Maradona Kafariki, alikuwa na buti moja chini limeandikwa Base akanikanyaga nalo duh maumivu yale yalimtoa chini Maradona akasepa mwendo wa Kimondo kuelekea kusikojulikana.

Tangu Siku hiyo hakunipiga tena.
 
Nimelelewa na Baba mdogo ila mtata kinoma,kuna siku alisafiri huku nyuma mi nkaacha kwenda chuo(madrasa),mama akiniambia niende chuo namwambia 'kausha' basi siku aliorudi akaambiwa taarifa zangu,mzee akaniita akiwa na gunia la bakora,akaniambia nivue nguo zote,baada ya kusaula alinipa kichapo ambacho siwez sahau,baada ya kunichapa sana akawa ananizungusha mtaani mm mbele yeye nyuma huku akiniteremshia mvua ya bakora tena akawa ananiambia niwe naimba hv,mm cna akili,mm mwehu,mm kichaa nisiependa chuo,basi alinikimbisha mchaka mchaka wa bakora mtaa mzima,nilvyoona hali mbaya na yeye hana dalili za kuniacha nkakimbilia msikitini maana ilikua mida km ya saa 2 hv usiku,mzee nkajitosa msikitini mzima mzima nliwakuta na wanakimu kwa ajili ya kuaza swala,hapo ndo ikawa ponea yangu maana wazee wa msikiti walimuona anisamehe japo alikua mgumu kunisamehe lkn mwisho akakubali kunisamehe,yy alitaka aendelee na lile zoezi usiku kucha,basi asubuhi yake nkaamka nkiwa na vidonda vya haja,alafu mtaan ikawa gumzo kila nnapopita nachekwa tena hadi na madem zangu,alafu pale mwanzo alipokua ananiamuru nivue nguo ile chupi nkawa cjaiweka chini,maana nlipovua chupi tu kichapo kikaanza kwa hiyo nkakosa nafasi ya kuiweka chini,hivyo mda wote wa mchaka mchaka wa mateso ile chupi nlikua nayo mkononi,(tena kipindi nakimbizwa na fimbo kulikua na kundi la watoto walikua wameunga ule mchakamchaka huku wakishangilia mm nnavyoadhirika) sasa baada ya kuingia msikitini wale mashekhe wakanitoa nje ili waongee na mdingi ili anisamehe,sasa mdingi alivyofika tu akanichapa bakora ya mkono tena ule mkono nlioishika ile chupi,kutokana na mshituko ile chupi ikaniluka na ckujua imelukia wapi kwa wakat huo,kumbe ile chupi ilirukia juu ya paa la msikiti,asubuhi yake watu(hasa watoto wenzangu) wakaiona juu ya bati basi ikawa stori tena kila nkipita nachekwa na kukejeliwa juu ya kile kichapo na chupi yangu kuwa juu ya paa la msikiti,ile chupi ilifanya tukio langu lisisahaulike haraka halafu ikanishangaza ilikua haianguki hata mvua iminyesha kias gani,ilikaa zaidi ya mwezi mmoja pale juu hadi ilipodondoka ndo nkaanza kua na amani maana watu wakaanza kusahau kile kipondo changu,hadi leo nmebaki na makovu km kumbukumbu ya lile tukio,USIOMBE YAKUKUTE
 
Mshua alinichapaga viboko mbele ya demu wangu alikuja kusuka.
Dingi amekuja mchana kula chakula akakuta hakuna maji hata ya kunawa mikono, kubabake alinichapa sticki hizo.
Demu wangu alikua nje anasukwa na dada yangu, dingi ananichapia sebuleni.
Kwa kuwa nilikua sitaki demu wangu ajue kama nachapwa, nikawa najikaza sipigi kelele.
Dingi akajua viboko havini umizi, akaanza kunipiga na mavibao, kubabake nilivimbaga mikononi.
Mara Paaaap nikatoka na mindoo kwenda kuchota maji, mialama ya viboko kwenye matako, mgongoni, mikononi.
2001 hiyo Kiloleni Tabora
Mzee wako alikuwa msala... Mm kuna jirani yangu alikuwa ni mtata sana, alikuwa anadaka madogo anawafungia kwenye mfuko ile ya kamba za katani anawapandishia darini la jikoni halafu anatafuta kuni zinazo toa moshi mwingi anawafukiza wakiwa huko darini hahaha
 
Mzee alikua anasema kama unajiona upo vizuri njoo tuzipange.

Alikua hapendi mtu anyoe kipara, kaka yangu akawa mbishi siku hiyo karudi home na kipara. Mzee akamwambia kimbia ukiona upo mbali sema tayari.

Jamaa akakimbia mzee anaona mdau anasogea tu hasemi tayari, akamuungia. Dakika kadhaa mbele tunaona kaka anarudishwa kabebwa begani.
Kufika home akaambiwa tuzipange, ghafla jamaa kapiga magoti analia anaomba msamaha.

Mzee akamwambia adhabu yako utakua unapaka kiwi kichwa hadi nywele ziote.
Mzee kwel alikuwa hatari"kimbia ukiwa mbali sema tayari"
 
Enzi hizo nasoma form six nimerudi likizo! Kuna demu mmoja alikuwa anapenda kupita pita mitaa ya nyumbani ili aninase....basi kumbe jana yake kwenda kutazama mechi za eufa kumbe wadogo zangu nao walitoka pale nyumbani kukawa hakuna mtu wa kufungua geti! Basi mzee alivyorudi alipiga honi alivyoona hakuna response yoyote akaamua ashuke na kufungua geti mwenyewe! Basi bwana kesho yake si ndio akanifuma namaliza na yule demu ili niokoe mzigo. Duh kilichotokea pale siwezi kukisimulia ila ni zaidi ya fedheha.
Malizia mkuu hamna tatizo just fun
 
Mzee alikua anasema kama unajiona upo vizuri njoo tuzipange.

Alikua hapendi mtu anyoe kipara, kaka yangu akawa mbishi siku hiyo karudi home na kipara. Mzee akamwambia kimbia ukiona upo mbali sema tayari.

Jamaa akakimbia mzee anaona mdau anasogea tu hasemi tayari, akamuungia. Dakika kadhaa mbele tunaona kaka anarudishwa kabebwa begani.
Kufika home akaambiwa tuzipange, ghafla jamaa kapiga magoti analia anaomba msamaha.

Mzee akamwambia adhabu yako utakua unapaka kiwi kichwa hadi nywele ziote.
Yaaani Nimecheka mpka nimejamba.
 
hao wazee wote mnaiwataja hapa hamna kitu asee nakumbuka mwaka 84 ilikua jumamosi mzee akatuagiza majani ya kuku tulikua na kuku wengi sana yeye akaenda kazini ..tulivyoenda tulikaa mpaka saa nane au tisa hivi ndo tukarudi na mizigo yetu ya majani ya kuku watu wa arusha wanayafahamu majani ya sungura..bwana kumbe mzee alikua amesharudi na ameenda kutafuta chakula cha kuku mwenyewe....kwakuanzia tuliambiwa kila mtu ale mzigo wake coz tuna njaa na kuku wameshakula hamna pa kuyapeleka...kwa jinsi alivyokua tukaanza kupiga mdogo mdogo tulikua watatu...kaka yangu akaleta ukorofi mzee alimtia kwenye gunia la kuhifadhia kahawa akalifunga kwa juu asee alimtia fimbo zisizo na idadi ..akamtoa kwenye gunia akamtia fimbo kavu kavu mpaka vijiti vikamwingia kama miba then akamfingia kwenye mti wa mlimao kwa minyororo kwa siku 3 day and 9t tulikua tunampelekea msosi kwa siri usiku na alivyotoka hapo ni kumuuguza na kumtoa vijiti mwilini......

pia nakumbua dada yetu mkubwa aliwahi kumpiga mdogo wake mama akamsemea mzee alimpiga then akampeleka kwe ng'ombe zizini akamwambia akae huko siku saba kwasababu anatabia za ng'ombe...kuna matukio mengi sana mfano akikupangia kazi usipifanya mfano ya shamba akirudi hata kama ni saa nne usiku utaenda kulima ...alikua anaogopwa mpaka na mabosi wake
bado yupo hai kweli maana hafai hata kidogo
 
Mzee wangu alikua mtata ila hamzidi kaka yake ambae ni baba mkubwa aisee kwanza nililijua jina halisi la baba mkubwa nikiwa umri umeenda ila nilijua jina la baba mkali alikua akija kusalimia home yeye ndo anakua kama baba mwenye nyumba anapiga mkwala mpk mdgo wake aisee kile kchwa balaa watoto wake walikuwa mamenyooka kama nguo ya kamanda siro kwake kulikua na taratibu ambazo kamwe hazivunjwi aisee apumzike kwa amani
hahahahaha izo taratibu sasa ivi zinavunjwa tu
 
Kibishi tu sasa hivi nikimtazama huwa naona kama Bro wangu hana noma, Mara ya Mwisho ananipiga ilikuwa niko Darasa la nne, alikuwa yupo safarini ila asubuhi aliniita chumbani akanipa majukumu ya kufanya, Nimeamka tu nikaenda kusakata kabumbu nikijidai Maradona hadi saa 12 jioni ndipo Maradona anarudi nyumbani akamkuta baba yake kafika hakuna kazi yeyote iliyotendeka.

Kipigo cha Kufa Mbwa kikamhusu Maradona, Kilichoniokoa niliona nikiendelea kulia na kupiga kelele nitakufa kwa ngumi na makofi ya Baba yake Maradona basi Nikajidai nimezima anapiga sitikisiki wala kugeuka kapiga kama dakika 1 kashituka, akajua Maradona Kafariki, alikuwa na buti moja chini limeandikwa Base akanikanyaga nalo duh maumivu yale yalimtoa chini Maradona akasepa mwendo wa Kimondo kuelekea kusikojulikana.

Tangu Siku hiyo hakunipiga tena.
hahahahaha hafai kwa jamii huyo
 
Back
Top Bottom