Wenye "madingi" wakali tukutane hapa

Wenye "madingi" wakali tukutane hapa

bado yupo hai kweli maana hafai hata kidogo
ni kati ya watu wa maana sana kwangu asee alifariki 96...kwetu mpaka leo hamna t.v kuna santuri na shelfu la vitabu..alikua mtu wa haki sana sema adhabu zake si za nchi hii...kadri siku zinavyoenda huwa natamani sana kuwa kama yeye but siwezi..ila kaka yangu hakuwahi kumpenda mpaka na sidhan kama hata anamkumbukaga
 
Nimelelewa na Baba mdogo ila mtata kinoma,kuna siku alisafiri huku nyuma mi nkaacha kwenda chuo(madrasa),mama akiniambia niende chuo namwambia 'kausha' basi siku aliorudi akaambiwa taarifa zangu,mzee akaniita akiwa na gunia la bakora,akaniambia nivue nguo zote,baada ya kusaula alinipa kichapo ambacho siwez sahau,baada ya kunichapa sana akawa ananizungusha mtaani mm mbele yeye nyuma huku akiniteremshia mvua ya bakora tena akawa ananiambia niwe naimba hv,mm cna akili,mm mwehu,mm kichaa nisiependa chuo,basi alinikimbisha mchaka mchaka wa bakora mtaa mzima,nilvyoona hali mbaya na yeye hana dalili za kuniacha nkakimbilia msikitini maana ilikua mida km ya saa 2 hv usiku,mzee nkajitosa msikitini mzima mzima nliwakuta na wanakimu kwa ajili ya kuaza swala,hapo ndo ikawa ponea yangu maana wazee wa msikiti walimuona anisamehe japo alikua mgumu kunisamehe lkn mwisho akakubali kunisamehe,yy alitaka aendelee na lile zoezi usiku kucha,basi asubuhi yake nkaamka nkiwa na vidonda vya haja,alafu mtaan ikawa gumzo kila nnapopita nachekwa tena hadi na madem zangu,alafu pale mwanzo alipokua ananiamuru nivue nguo ile chupi nkawa cjaiweka chini,maana nlipovua chupi tu kichapo kikaanza kwa hiyo nkakosa nafasi ya kuiweka chini,hivyo mda wote wa mchaka mchaka wa mateso ile chupi nlikua nayo mkononi,(tena kipindi nakimbizwa na fimbo kulikua na kundi la watoto walikua wameunga ule mchakamchaka huku wakishangilia mm nnavyoadhirika) sasa baada ya kuingia msikitini wale mashekhe wakanitoa nje ili waongee na mdingi ili anisamehe,sasa mdingi alivyofika tu akanichapa bakora ya mkono tena ule mkono nlioishika ile chupi,kutokana na mshituko ile chupi ikaniluka na ckujua imelukia wapi kwa wakat huo,kumbe ile chupi ilirukia juu ya paa la msikiti,asubuhi yake watu(hasa watoto wenzangu) wakaiona juu ya bati basi ikawa stori tena kila nkipita nachekwa na kukejeliwa juu ya kile kichapo na chupi yangu kuwa juu ya paa la msikiti,ile chupi ilifanya tukio langu lisisahaulike haraka halafu ikanishangaza ilikua haianguki hata mvua iminyesha kias gani,ilikaa zaidi ya mwezi mmoja pale juu hadi ilipodondoka ndo nkaanza kua na amani maana watu wakaanza kusahau kile kipondo changu,hadi leo nmebaki na makovu km kumbukumbu ya lile tukio,USIOMBE YAKUKUTE
hahahahahhaha mada nzima chupi na sio dingi tena hahahahah
 
Ni ukweli usiopingika Wazee wa zama zile wengi wao walikuwa wakali hatari,walikuwa hawataki mchezo na wakiwepo full heshima yaani mpaka raha;na kipindi hicho vijana weng walikuwa na sifa ya ukorofi acha hawa wa siku hizi;Mzee akiwepo Nyumbani ni kimya na wala hakuna kutangatanga,kuropoka au kulala lala ovyo bila kazi,na masister walikuwa hawabebi mimba wakiwa Nyumbani maana mziki wake wanaujua ila Wazee wa siku hizi jina tu,madada wanazaa ovyo ovyo na vijana nao wapo huru kufanya watakayo,kiufupi mambo yamebadilika kwa sasa,Wazee wa miaka ile walikuwa Wakoloni kwwl
 
hao wazee wote mnaiwataja hapa hamna kitu asee nakumbuka mwaka 84 ilikua jumamosi mzee akatuagiza majani ya kuku tulikua na kuku wengi sana yeye akaenda kazini ..tulivyoenda tulikaa mpaka saa nane au tisa hivi ndo tukarudi na mizigo yetu ya majani ya kuku watu wa arusha wanayafahamu majani ya sungura..bwana kumbe mzee alikua amesharudi na ameenda kutafuta chakula cha kuku mwenyewe....kwakuanzia tuliambiwa kila mtu ale mzigo wake coz tuna njaa na kuku wameshakula hamna pa kuyapeleka...kwa jinsi alivyokua tukaanza kupiga mdogo mdogo tulikua watatu...kaka yangu akaleta ukorofi mzee alimtia kwenye gunia la kuhifadhia kahawa akalifunga kwa juu asee alimtia fimbo zisizo na idadi ..akamtoa kwenye gunia akamtia fimbo kavu kavu mpaka vijiti vikamwingia kama miba then akamfingia kwenye mti wa mlimao kwa minyororo kwa siku 3 day and 9t tulikua tunampelekea msosi kwa siri usiku na alivyotoka hapo ni kumuuguza na kumtoa vijiti mwilini......

pia nakumbua dada yetu mkubwa aliwahi kumpiga mdogo wake mama akamsemea mzee alimpiga then akampeleka kwe ng'ombe zizini akamwambia akae huko siku saba kwasababu anatabia za ng'ombe...kuna matukio mengi sana mfano akikupangia kazi usipifanya mfano ya shamba akirudi hata kama ni saa nne usiku utaenda kulima ...alikua anaogopwa mpaka na mabosi wake
Khaaa huyu alikuwa zaidi ya mkali
 
Nakumbuka nilikuwa napenda sana kutengeneza manati.sasa kama mnavyojua manati yanatakiwa yawe na like kingozi cha kushikia jiwe,na lazima kiwe kilaini.sasa bwana huku na huku nikatafuta ngozi bila mafanikio.akili ikanituma nikakate kiatu cha baba anachokipenda kuliko vyote.kilichotokea alivyorudi huwa ctak kukumbuka maana alinipa kichapo kiwango cha lami.
Hapa huwezi kusema baba yako ni mkali
 
Nimelelewa na Baba mdogo ila mtata kinoma,kuna siku alisafiri huku nyuma mi nkaacha kwenda chuo(madrasa),mama akiniambia niende chuo namwambia 'kausha' basi siku aliorudi akaambiwa taarifa zangu,mzee akaniita akiwa na gunia la bakora,akaniambia nivue nguo zote,baada ya kusaula alinipa kichapo ambacho siwez sahau,baada ya kunichapa sana akawa ananizungusha mtaani mm mbele yeye nyuma huku akiniteremshia mvua ya bakora tena akawa ananiambia niwe naimba hv,mm cna akili,mm mwehu,mm kichaa nisiependa chuo,basi alinikimbisha mchaka mchaka wa bakora mtaa mzima,nilvyoona hali mbaya na yeye hana dalili za kuniacha nkakimbilia msikitini maana ilikua mida km ya saa 2 hv usiku,mzee nkajitosa msikitini mzima mzima nliwakuta na wanakimu kwa ajili ya kuaza swala,hapo ndo ikawa ponea yangu maana wazee wa msikiti walimuona anisamehe japo alikua mgumu kunisamehe lkn mwisho akakubali kunisamehe,yy alitaka aendelee na lile zoezi usiku kucha,basi asubuhi yake nkaamka nkiwa na vidonda vya haja,alafu mtaan ikawa gumzo kila nnapopita nachekwa tena hadi na madem zangu,alafu pale mwanzo alipokua ananiamuru nivue nguo ile chupi nkawa cjaiweka chini,maana nlipovua chupi tu kichapo kikaanza kwa hiyo nkakosa nafasi ya kuiweka chini,hivyo mda wote wa mchaka mchaka wa mateso ile chupi nlikua nayo mkononi,(tena kipindi nakimbizwa na fimbo kulikua na kundi la watoto walikua wameunga ule mchakamchaka huku wakishangilia mm nnavyoadhirika) sasa baada ya kuingia msikitini wale mashekhe wakanitoa nje ili waongee na mdingi ili anisamehe,sasa mdingi alivyofika tu akanichapa bakora ya mkono tena ule mkono nlioishika ile chupi,kutokana na mshituko ile chupi ikaniluka na ckujua imelukia wapi kwa wakat huo,kumbe ile chupi ilirukia juu ya paa la msikiti,asubuhi yake watu(hasa watoto wenzangu) wakaiona juu ya bati basi ikawa stori tena kila nkipita nachekwa na kukejeliwa juu ya kile kichapo na chupi yangu kuwa juu ya paa la msikiti,ile chupi ilifanya tukio langu lisisahaulike haraka halafu ikanishangaza ilikua haianguki hata mvua iminyesha kias gani,ilikaa zaidi ya mwezi mmoja pale juu hadi ilipodondoka ndo nkaanza kua na amani maana watu wakaanza kusahau kile kipondo changu,hadi leo nmebaki na makovu km kumbukumbu ya lile tukio,USIOMBE YAKUKUTE
mkuu ilikuwa wapi hyoo???

umenikumbusha kitambo sana

mie nakumbuka enzi hizo kuna siku sikuenda madrasa mda wa jioni asee mdingi kurudi si akapata taarifa kwamba dogo sijaenda madrasa dooooohhhh..

nlikaa nje tangu saa tatu usiku mpaka mda usiofahamika mpaka kuna jirani yetu akanionea huruma akanichukua nikaenda kulala kwake mpaka asubuhi ...

mzee alikuwa hataki mchezo kabisa aseee
 
Mzee alikua anasema kama unajiona upo vizuri njoo tuzipange.

Alikua hapendi mtu anyoe kipara, kaka yangu akawa mbishi siku hiyo karudi home na kipara. Mzee akamwambia kimbia ukiona upo mbali sema tayari.

Jamaa akakimbia mzee anaona mdau anasogea tu hasemi tayari, akamuungia. Dakika kadhaa mbele tunaona kaka anarudishwa kabebwa begani.
Kufika home akaambiwa tuzipange, ghafla jamaa kapiga magoti analia anaomba msamaha.

Mzee akamwambia adhabu yako utakua unapaka kiwi kichwa hadi nywele ziote.
Dah Mzee mbabe sana
 
Daaah,maisha haya!!
Mkuu umenikumbusha maisha yangu ya utotoni.

Kwa asilimia kubwa mzee alikuwa huko job mwanza, lakini kila weekend alikuwa anarudi home.

Huyu mzee alikuwa mkali na mbabe haswaa!!

Kwanza tulikuwa tumenunuliwa saa za mkononi,inatakiwa saa kumi na mbili jioni uwe umesharudi home,ukichelewa hata dakika moja utakula kichapo kikali sana.

Kaka yetu mkubwa kwa sasa ni marehemu,alichelewa kurudi home,mzee akazama kitaani kumtafuta mwenyewe,aliporudi nae akajifungia nae ndani,brother alikula kichapo heavy mpaka akachanganyikiwa, mzee akawa anamuuliza nimekukuta wapi?Bro,anajibu nimesahau uliponikutia!!

Mungu amjaalie umri mrefu sana,kwa sasa ana miaka 70 lakini hadi wajukuu wakizingua wanachezea kichapo.


Mimi mwenyewe siwezi kumjibu nikiwa karibu,akiwa anakuuliza ukikaa kimya ni kichapo unadharau,halafu ukimjibu unapigwa vibao kwa sababu ni kiburi kumjibu.

Sio mzungumzaji sana lakini ukiongea nae akikwambi,unyamaze imetosha!!unapaswa kunyamaza,ukiendelea kuongea una hamu ya kukandwa
 
Daaah,maisha haya!!
Mkuu umenikumbusha maisha yangu ya utotoni.

Kwa asilimia kubwa mzee alikuwa huko job mwanza, lakini kila weekend alikuwa anarudi home.

Huyu mzee alikuwa mkali na mbabe haswaa!!

Kwanza tulikuwa tumenunuliwa saa za mkononi,inatakiwa saa kumi na mbili jioni uwe umesharudi home,ukichelewa hata dakika moja utakula kichapo kikali sana.

Kaka yetu mkubwa kwa sasa ni marehemu,alichelewa kurudi home,mzee akazama kitaani kumtafuta mwenyewe,aliporudi nae akajifungia nae ndani,brother alikula kichapo heavy mpaka akachanganyikiwa, mzee akawa anamuuliza nimekukuta wapi?Bro,anajibu nimesahau uliponikutia!!

Mungu amjaalie umri mrefu sana,kwa sasa ana miaka 70 lakini hadi wajukuu wakizingua wanachezea kichapo.


Mimi mwenyewe siwezi kumjibu nikiwa karibu,akiwa anakuuliza ukikaa kimya ni kichapo unadharau,halafu ukimjibu unapigwa vibao kwa sababu ni kiburi kumjibu.

Sio mzungumzaji sana lakini ukiongea nae akikwambi,unyamaze imetosha!!unapaswa kunyamaza,ukiendelea kuongea una hamu ya kukandwa
Hahahaa kama nawaona mlivyokuwa mnatamani kurudisha siku nyuma weekend isifike
 
We jamaa unaongelea kuchapwa na waya za umeme??....me nlichapwa na hizo waya, mipira ya maji mzee akaona hii bado nunda...basi akatafuta kipande cha waya unaoshikilia nguzo za simu (steel wire).....daahh ilikua shughuli, nlipigwa tatu tu ila ziligonga hadi mifupa!!!
 
mkuu ilikuwa wapi hyoo???

umenikumbusha kitambo sana

mie nakumbuka enzi hizo kuna siku sikuenda madrasa mda wa jioni asee mdingi kurudi si akapata taarifa kwamba dogo sijaenda madrasa dooooohhhh..

nlikaa nje tangu saa tatu usiku mpaka mda usiofahamika mpaka kuna jirani yetu akanionea huruma akanichukua nikaenda kulala kwake mpaka asubuhi ...

mzee alikuwa hataki mchezo kabisa aseee
Hahahah
 
Back
Top Bottom