Wenye magari pitieni hapa kuepuka kupigwa vituo vya mafuta

Wenye magari pitieni hapa kuepuka kupigwa vituo vya mafuta

Singida ndio home

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2012
Posts
3,188
Reaction score
3,370
foto28493.jpg


Mafuta ni kitu muhimu kwenye gari, Ni mara kwa mara tunayajaza haya mafuta lakini tukumbuke pia unaweza kupigwa mchana kweupe.

Hakikisha kabla hujajaza mafuta ile pump ya kujazia imerudishwa kikamilifu kwenye mashine, Pump inaporudishwa lazima mashine isome 0.00, ila endapo pump ikategeshwa ionekane kwamba imerudishwa haitasome 0.00 hapo utakuwa umepigwa.

Hakikisha kwamba ukiweka mafuta basi kiasi kamili kiwekwe bila kuunga unga, mfano ukiwaambia wakuwekee mafuta ya elf 10 wasiweke ya elfu mbili alafu kwenye mashine waongezee ya elfu nane bila kurudisha pump ili isome 0.0, kitachotokea ni kwamba watakuingizia ya elfu mbili tu hayo ya elfu 8 hayatoki itatoka hewa tu.

Mwenzako wa mbele anapojaziwa sisitiza sana pump ipachikwe kwenye mashine ili isome 0;00 usiruhusu mwenzako wa mbele ajaziwe na wewe ujaziwe mafuta bila pump kurudishwa kwenye mashine ili ianze upya.

Hakikisha unaangalia kwenye kioo wameingiza pump kwenye gari yako, ukiwa mzembe wanaweza wanaweza kujijazia kwenye vigaloni.

Omba risiti na uhakikishe ni ya pump waliyokujazia na muda uendane na ulipojaza, nakumbuka niliwahi kupewa risiti ya saa tatu asubuhi wakati nimejaza jioni.

Muhimu: Kwa hizi njia anayeiba sio sheli ni mtu. Usipumbazwe na sheli fulani kusifiwa.

zamani watu wakihisi wanapigwa walikua wanaenda na vidumu vyeupe vile vinavyoonesha ujazo ila Tangu mwaka 2009 EWURA ilipopiga marufuku unaweza kukataliwa kujaziwa, ukitaka kujaziwa uende kirafiki usiende kwa nia ya kuhisi wanakuibiaga.

 
Kuibiwa mara nyingi hutokea wakati wanaojaza mafuta wako wengi. Na anayeibiwa hapo ni mteja na siyo boss !

Mbinu za wizi:

1. Wakati anakuulizia kiasi cha mafuta unachotaka kuweka, pump anakuwa kaiegesha kwenye dumu ( anaweka mafuta ).
Ukishampa pesa, anahamishia tu pump kwako bila kureset. Hapo ushapigwa.

2. Upo kwenye foleni: Boda Boda, Wewe, Dala Dala, Roli.

Hapo mfano: Kama Boda Boda anaweka ya elfu 10, anakuwa wa kwanza kuwekewa. Wakati anawekewa wewe unaulizwa unaweka ya kiasi gani ?

Kama ni Let's Say Tsh 30,000 Pump inahamishwa directly kutoka kwa Boda Boda kuja kwako bila resetting.
Hapo Tsh 10,000 ya Boda Boda inawekwa pembenii
 
Mi huwa nikifika tu sheli hali yote ya ukali unatawala hlo bit hapo huwa wanajikut mbinu zimeisha zote kwanza kwa mkwala lazma nishuke kwenye gari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Somo kabisa hili


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Siku hizi wizi wa kijinga haupo maana pump ikisharudi tu risiti yatoka

Sent using Jamii Forums mobile app
Gari ambalo nilikuwa mbele yako kama lijaziwa mafuta ya elf 10 na dereva hakuchukua risiti na wewe ukajaza ya elfu 10 unaweza kichezewa michezo niliyoitaja ukapigwa na ukapewa risiti ya elf 10
 
Back
Top Bottom