Wenye Nyumba kaeni kitaalamu: Kama mpangaji wako atakutwa na dawa za kulevya nyumba yako itataifishwa!

Wenye Nyumba kaeni kitaalamu: Kama mpangaji wako atakutwa na dawa za kulevya nyumba yako itataifishwa!

Na hadi leo huyo mbunge hajawahi kutajwa wala kukamatwa.
images - 2024-11-25T125514.479.jpeg
 
Wakuu,

Kama una nyumba sehemu kaa kwa chonjo kuna habari mpya huku kutoka DCEA.

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo, amewahimiza wamiliki wa nyumba za kupangisha kuwa waangalifu na wapangaji wao.

Alieleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara wa dawa za kulevya wamekuwa wakitumia nyumba walizopanga kama maghala ya kuhifadhi dawa hizo, huku wao wakiishi sehemu nyingine.


Soma pia: Makonda: Ukichagua viongozi wa mtaa waaminifu wasiyojihusisha na madawa ya kulevya utaleta chachu katika ngazi hiyo

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Novemba 25, 2024, jijini Dar es Salaam, Kamishna Jenerali Lyimo alisisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria, mali yoyote, kama nyumba au gari, ikikutwa na dawa za kulevya, itataifishwa.

Kamishna huyo amewataka wamiliki wa mali hizo kuhakikisha wanachukua tahadhari na kusimamia vyema mali zao ili kuepuka hasara na kuhusishwa na vitendo haramu.

Source: Wasafi FM

My take:
Mbona kama kuna watu specific wanatafutwa kwa tochi kupitia agizo hili?

1. Mimi kama mwenye nyumba ntajuaje kama mtu anaweka madawa ya kulevya ndani ya nyumba? Niweke CCTV au niwe nafanya doria za kushtukiza?

2. Hiyo nyumba ikishataifishwa inapelekwa kwa nani au taasisi gani?

3. Kama inaenda kwa serikali hamuoni kwamba kuna baadhi ya vigogo serikalini wanaweza wakatumia mwanya huo kupora nyumba za watu iwapo watazipenda?

4. Huo utaratibu wenu wa kutaifisha nyumba ni watanzania pekee au ni utratibu wa kimataifa? Ni mataifa gani yana utaratibu kama huo?

5. Hiyo sheria ya kutaifisha nyumba ambayo sio ya mtuhumiwa ipo kwenye ibara gani kwenye Katiba yru ya inchi?
Na mabasi ya abiria,treni na ndege zitaifishwe pia zitakazo beba abria wenye madawa ya kulevya,
 
Hapo deal ni kuweka hicho kipengele kwenye Mkataba wakati wa kumpangisha mtu.

Mimi niliwahi kuweka kipengele cha kumtaka Mpangaji kueleza kazi ama shughuli aifanyayo kuendesha maisha yake

Hii ilisaidia kutowapangisha watu Wasumbufu kulipa Kodi

Hopefully na hicho kipengele kikiwepo kwenye Mkataba wa kupangisha, kitasaidia kumlinda mwenye nyumba
kwani mkuu mtu anaweza kuwa na kazi moja ya kumuingizia kipato mtu anaweza kuwa na biashara tatu lakini akakutajia moja tu..unajua kuna biashara hazionekani kwenye macho ya wengi lakini zinalipa pesa ndefu
 
Wakuu,

Kama una nyumba sehemu kaa kwa chonjo kuna habari mpya huku kutoka DCEA.

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo, amewahimiza wamiliki wa nyumba za kupangisha kuwa waangalifu na wapangaji wao.

Alieleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara wa dawa za kulevya wamekuwa wakitumia nyumba walizopanga kama maghala ya kuhifadhi dawa hizo, huku wao wakiishi sehemu nyingine.


Soma pia: Makonda: Ukichagua viongozi wa mtaa waaminifu wasiyojihusisha na madawa ya kulevya utaleta chachu katika ngazi hiyo

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Novemba 25, 2024, jijini Dar es Salaam, Kamishna Jenerali Lyimo alisisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria, mali yoyote, kama nyumba au gari, ikikutwa na dawa za kulevya, itataifishwa.

Kamishna huyo amewataka wamiliki wa mali hizo kuhakikisha wanachukua tahadhari na kusimamia vyema mali zao ili kuepuka hasara na kuhusishwa na vitendo haramu.

Source: Wasafi FM

My take:
Mbona kama kuna watu specific wanatafutwa kwa tochi kupitia agizo hili?

1. Mimi kama mwenye nyumba ntajuaje kama mtu anaweka madawa ya kulevya ndani ya nyumba? Niweke CCTV au niwe nafanya doria za kushtukiza?

2. Hiyo nyumba ikishataifishwa inapelekwa kwa nani au taasisi gani?

3. Kama inaenda kwa serikali hamuoni kwamba kuna baadhi ya vigogo serikalini wanaweza wakatumia mwanya huo kupora nyumba za watu iwapo watazipenda?

4. Huo utaratibu wenu wa kutaifisha nyumba ni watanzania pekee au ni utratibu wa kimataifa? Ni mataifa gani yana utaratibu kama huo?

5. Hiyo sheria ya kutaifisha nyumba ambayo sio ya mtuhumiwa ipo kwenye ibara gani kwenye Katiba yru ya inchi?
Ni mambo ya ajabu sana haya, kweli hilo ndio suluhisho la kupambana na dawa za kulevya?

Mfano nina nyumba chanika,boko,kimara, kinondoni, mbezi beach na ubungo, hapo mimi kama mwenye nyumba nitazilinda vipi na watu haujui wanaingia na nini kila siku kwenye hizo nyumba?

Kweli kabisa wao wanaona hii ni rahisi kwa raia wa mtaani tuu kuweza kubaini madawa kirahisi namna hii?

Kama umempata muhusika na dawa zake iweje utaifishe nyumba kitu ambacho hakijahusika na usafirishaji wa dawa hizo?

Kosa la nyumba ni kuhifadhi na si mtu aliyezibeba kutoka huko zilikotoka?


Vipi watu wakifanya hujuma za kutaka nyumba za watu mtawazuia kwa namna ipi?

Ndugu Kamishna tunaomba hili mlitazame kwa undani na mje na plan nyingine ya kudhibiti madawa na si hili la kutaifisha nyumba za watu, nyumba hazina makosa makosa yapo kwa wabebaji, taifisheni vyombo vya usafiri ingawa sijawai kusikia ndege ikitaifishwa kwa kumbeba mtu mwenye madawa ya kulevya.
 
Biashara ya nyumba za kupanga, ni changamoto kwa baadhi ya maeneo na kwa baadhi ya wapangaji wasio waaminifu coz anaweza fanya tukio huko au nyumba yako ikahifadhiwa vitu vibaya kama hilo angalizo.
 
SHERIA ya hovyo kabisa hii... Likikamatwa gari la Serikali inakuwaje!?? Kama zilivyokamatwa ambulances na macruiser ya serikali!? Zikikamatwa kwenye quarters za Serikali!?? Ama kwenye maghorofa ya shirikabla nyumbal la Taifa !??
Mpangaji akipangishwa nyumba mwenye nyumba ana uhuru gani wa kukagua nyumba kila siku!!? Huyu Lyimo atakuwa ni mchaga mjinga wa kwanza.

Hivi DCEA hawamo humu waje watujibu maswali yetu?

Sheria hii itawaumiza wengi sana
 
Back
Top Bottom