Wenye Nyumba kaeni kitaalamu: Kama mpangaji wako atakutwa na dawa za kulevya nyumba yako itataifishwa!

kwani mkuu mtu anaweza kuwa na kazi moja ya kumuingizia kipato mtu anaweza kuwa na biashara tatu lakini akakutajia moja tu..unajua kuna biashara hazionekani kwenye macho ya wengi lakini zinalipa pesa ndefu
Ni kweli usemacho, lakini pale kwenye Mkataba atasema kazi yake Moja halali

Kwahiyo akikamatwa na ishue ya madawa itakuwa ni suala lake binafsi kwahiyo nyumba yako haiwezi kuwa kwenye risk ya kutaifishwa
 
Hii sheria imepitishwa na watanzania wenye akili timamu kabisa wenye bachekor degree kabisa ya miaka mitatu/minne?
 
Umeweka kipengele mpangaji ameona na amesaini
Then anakutwa na Unga
Kipengele kitasaidia nini?
Mimi nadhani hii kitu kuna mtu anatafutwa na asipokuwa makini ataingia kwenye mfumo
 
Nyumba zangu za kupangisha Kuna kupengele Mali ya mpangaji ni yake haisiani na mwenye nyumba hata ulinzi WA Mali zake ni juu ya mpangaji mwenyewe,Sheria ya Lyimo inakinzana na masharti ya wapangaji wangu
daah! lakini mkuu sheria zako binafsi na wapangaji wako haziwezi kuwa juu ya sheria za kitaifa za wenye mamlaka walioshika mpini si unajua mfumo wa hii nchi unavyotenda kazi zake itabidi uwe mpole tu..
 
Umeweka kipengele mpangaji ameona na amesaini
Then anakutwa na Unga
Kipengele kitasaidia nini?
Mimi nadhani hii kitu kuna mtu anatafutwa na asipokuwa makini ataingia kwenye mfumo
Hicho kipengele kitamlinda mwenye nyumba, kwamaana hatowajibishwa Kwa makosa yasiyo yake
 
Hata kama ya msikiti au kanisa?
 
Na mabasi ya abiria,treni na ndege zitaifishwe pia zitakazo beba abria wenye madawa ya kulevya,

Wamejilinda kwa maandishi madogo yenye kanuni, sheria na masharti.

Hivyo wenye nyumba mikataba iwe na kanuni, masharti na vigezo katika maandishi ili kujikinga na usumbufu au utapeli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…