Wenye nyumba kupandisha kodi je hii nayo inaenda na kupanda bei za mafuta?

Wenye nyumba kupandisha kodi je hii nayo inaenda na kupanda bei za mafuta?

ommytk

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2015
Posts
520
Reaction score
1,143
Kuna changamoto kwa sasa tunapitia watu kupandisha bei ya vitu kwa taarifa kuwa mafuta yamepanda bei sababu ikiwa vita vya Ukraine, sawa tunakubali ila kuna kama wengine wanafata mkumbo tu, maana jana mwenye nyumba wetu katuambia kodi mwezi ujao itapanda sababu ikiwa gharama za maisha kupanda sasa nyumba ushajenga kuna gharama gani zingine zimepanda naona hii hali ya Ukraine kuna watu wanaotumia kama nafasi kutudhulumu wanyonge.
 
Ila inaweza kuwa sahihi ... huwezi jua kuwa anategemea kodi zenu ili kuendesha maisha yake. Kama Hana chanzo kingine Cha mapato tofauti na kodi
 
Kuna changamoto kwa sasa tunapitia watu kupandisha bei ya vitu kwa taarifa kuwa mafuta yamepanda bei sababu ikiwa vita vya Ukraine sawa tunakubali ila kuna kama wengine wanafata mkumbo tu maana Jana mwenye nyumba wetu katuambia kodi mwezi ujao itapanda sababu ikiwa gharama za maisha kupanda sasa nyumba ushajenga kuna gharama gani zingine zimepanda naona hii hali ya Ukraine kuna watu wanaotumia kama nafasi kutudhukumu wanyonge

Kujenga nyumba sio jambo dogo, mwenye nyumba angeweka pesa zake huko leo angekuwa anapambana na mfumuko wa bei, lakini kajenga nyumba, kakupangisha wewe, na hiyo nyumba ndio chanzo chake cha mapato. Sasa kama anaona akiongeza kodi ndio atapata nafasi ya kujikinga na mfumuko wa bei, wewe mwambie tu nahama. Au simamia kwenye mkataba wenu wa upangaji.
 
Ndio mfumuko wa bei huo mkuu, mafuta yanaendesha uchumi wote hasa usafirishaji wa bidhaa. Ili aweze kununua maandazi yaliyopanda bei inabidi chanzo cha mapato kiongezeke. Kwenye uchumi tunaangalia sasa, hiyo nyumba angeijenga sasa gharama zingeongezeka..

Mafuta yanakuja kuleta mfumuko wa bei, kila mtu kwenye kamba yake ataongeza urefu kupambana na uhalisia..
 
Leo kkoo 1.5sqm wire tulikua tunanunua kwa 45,000/- leo ni 48,000/-, 75,000/- ya 2.5sqm ni 78k,
Vitu vimepanda bei mazee
 
Na Bado! Ngoja tumalizie Usajili wa Makazi tuanze kuwaonesha Rangi za Dunia.
 
Kuna jamaa jana kaniuzia paka nikamwambia apunguze bei anasema paka bei juu kisa vita ya Ukraine na Russia!
Samahani mkuu, wewe ni shabiki wa simba? Maana hivi karibuni wana mechi za Kimataifa. Sasa ulivyosema umetoka kuuziwa paka, nimepatwa na mshtuko wa ghafla.
 
Kuna gharama za matengenezo madogo madogo ambayo yanahitaji pesa, ukiharibu kifaa cha umeme, kifaa cha maji, ukijaza choo, ukiharibu ukuta kwa kuuchora chora,...n.k, tuzidi kuombea Amani tu
 
Back
Top Bottom