Wenye uzoefu wa kupanda Malori yanayoelekea mikoani, namuomba hapa

Wenye uzoefu wa kupanda Malori yanayoelekea mikoani, namuomba hapa

Ni bado najitafuta , nauli bei ghari mkuu. Ni bora hiyo pesa niitumie nikifika dodoma kwa malazi na chakula
sasa mkuu mabasi kibao unapandaje Lori? huoni utachelewa sana njiani?
 
Za
Njoo nikupe lift kwenye gari ya magazeti upate offer ya kumuona Izraeli mtoa roho upige nae selfie ukaonyeshe mwisho wa safari.
Magazeti huwaga ni maeneo yapi kiongosi ndo location zao mm nipo magomeni mkuu
 
Shida ni PESA WAKUU SHIDA NI PESA , HELA NI NDOGO , NITAFURAHI NIKIPATA. USAFIRI WA 10K MPAJA MKOA DESTINED THEN mengine yatatokea ikiwapo na kuwahi eneo husika
 
Mkuu ni shapanda sana lorry kisa mkwanja umepelea,vya kuzingatia Kuna kuchangia,sio Bure na lazima utoke dar siku 2 au tatu kabla ya interview maana ni malori,kama umezoea shuruba utaona kawaida ila kama mayai mayai jiandae kisaikolojia,good luck
 
Bwa mdogo pole sana km kweli unakosa nauli ya Dar-Dom.
Wako wadau hapa ungewasilisha vizuri hitaji lako Dom unafika bila kutumia senti,mradi uwe na story kibao huko njia mfike salama asilale akakubondabonda huko njiani.
We sema tu naenda Dom sina nauli naomba msaada.
Kesho ushafika.
Na hela ya kula utapewa.
Kuna watu wakarimu sana JF ukijua kujieleza.
 
Ni kweli nilipanda howo nikalipa elfu kumi kwenda dom, kufika moro jamaa kaninunulia msosi na maji ya uhai, shofa alikuwa na story balaa safari ilikuwa fupi mno
Shofa ndio jina lake?
 
Back
Top Bottom