Wenye viwanda vya khanga mfikirie kuongeza ukubwa wa khanga

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011


Dunia imebadilika na idadi ya wanaovaa extra size imeongezeka, ukubwa wa khanga umebakia ule ule.

Unanunua khanga hata bila kuikata unapinda zote mbili lakini bado ni ndogo. Mbona vitenge tunauziwa piece tatu? Wenzenu walishaona umuhimu wa super size.

Kuna mitandio inatoka Karachi Pakistan, huwa na ukubwa wa kuridhisha, kama khanga zingekuwa size ile ingependeza.

Wekeni khanga za vipande vitatu, sisi mabonge tutanunua, soko la sasa hivi halikidhi mahitaji yetu.
 
Naunga mkono hoja
 
Umefikiria nje ya box, kweli kuna shida, nimeishuhudia especially kwa wale waliojaaliwa neema za Allah.
 
Tafuta khanga za Mombasa ni kubwa na zitakidhi mahitaji yako

Nilimnunulia wife na mama angu kwa kweli ni kubwa sana halafu hazina maandishi,so ata ukishona nguo zinawapendeza
Hizi khanga za Nida ni biashara tu, khanga imekuwa kama kitambaa cha kichwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…