Wewe ni Mvulana au Mwanaume.?
Kuna ukweli mchungu inapokuja kwenye kubadirika kutoka
Mvulana kwenda
Mwanaume na umri hauhusiani na hilo.
Ni ngumu katika kubadirika kutoka
Mvulana na kuwa
Mwanaume. Lakini pia jamii ya sasa inafanya hili kuwa ni ngumu zaidi.
Jamii ya sasa inajaribu kuwabadirisha wavulana mapema kuwa na tabia za kike,
Huenda na wewe pia ukawa ni mwenye kuoshwa ubongo na jamii ya sasa na matokeo yake kukupelekea wewe kuwa
dhaifu na mwenye utoto katika uanaume wako.
Huenda likakuijia wazo la kuwa
wanaume wanatakiwa kuwa wa kike zaidi na kuwa na
Uanaume ni
SUMU
Fikiria kuhusu hili;
Tangu upo kijana mdogo ulikuwa ukiambiwa tabia zako za kiume ni mbaya, yaani kuwa wa
kiume ni dalili za tabia mbovu.
Wengi wa walimu wako kama sio wote walikuwa ni wanawake.
Na kama ulikuwa huwezi kukaa kama watoto wa kike darasani basi ulikuwa unaonekana na tabia mbaya na mbovu.
Kama kijana wa
kiume, ikiwa ulikuwa na
ushindani,
kutafuta changamoto na
kuwa na nguvu nyingi ulikuwa unapata aibu na kudhalauliwa kwa hicho "Eti kanajifanya kanaume".
Wakati muda huo huo ili
mwanaume aweze
kutawala,
kusaidia na
kulinda, Mbinu hizi kiuhalisia huwa ni lazima.
Kama umekuwa ukikandamiza asili yako ya
kiume! kwa muda ambao hata ukumbuki ulianza lini kujikandamiza, Njia ya kutakasa ubongo wako haitakuwa rahisi.
Lakini itafaa Niamini.
Tuendelee.....
Sasa hata kama hukuangukia kwenye uongo wa jamii ya sasa, hii haikutoshi kukubadirisha kutoka
Mvulana kuwa M
wanaume.
Waschana hugeuka wanawake kwa kufikia ukomavu wa kimwili.
Lakini
wavulana wanatakiwa kushinda mtihani. Mwisho wa yote, Wanaume hubeba mzigo wa Utendaji.
Kama hufanyi kazi katika kipengele chochote cha maisha yako kama
mwanaume. Dunia itakuona kama mtu wa daraja la chini asiye na thamani.
Mwanamke anaweza kuwa mrembo, na dunia inaweza kumfanya kama Almasi,Utadhani kuna thamani katika urembo wake (
No offence).
Kwa
mwanaume hivi sivyo ilivyo, Ni lazima utajituma kwenye kazi ili uweze kutengeneza thamani yako mwenyewe.
Huu ni ukweli Mchungu kwa
wavulana.
Vyovyote vile, Unatakiwa utizame hili kama kitu kizuri, Maana yake haijarishi wewe ni nani, Unaweza kujijenga na kujiweka mwanaume mwenye thamani kubwa.
Andika chini wanaume unaowaheshimu sana katika maisha yako.
- Kipi kinakufanya uwaheshimu?
- Uwezo wao wa kuondosha matatizo?
- Uwezo wao wa kutatua shida?
- Ujasiri?
- Nguvu?
- Nidhamu? au Uongozi?
Chochote kinachokufanya uwaheshimu kama
wanaume hakina mahusiano na umri.
Tujadili mambo 4 (manne) ambayo yatamgeuza MVULANA kuwa MWANAUME,
1: Majukumu
Wavulana:
hufanya chochote wanachotaka au wanachohisi na huwalaumu watu wengine kwa yanayowatokea kwenye maisha yao.
Badala ya kufanya majukumu yao, wao hulaumu kuhusu matatizo yanayotokea. Na hujiona wao ni wenye kuonewa katika hali na hupenda kutukana kwa maandishi hata simu utaona hawapendi kuongea zaidi wao hutumia ujumbe.
Wanaume:
huelewa ya kwamba siku zote kuna umiliki wa kuchukua sehemu. Hata kama mtu mwingine kawakosea au kavuruga mambo yao.
Bado kuna sehemu yao ya kumiliki wao hujua ipo tu na huamua kutukana kwa mafanikio na hata mawasiliano yao ni maongezi.
Kwa mfano;
Unaweza kuamua kupuuza HATARI. Asilimia 90 katika 100 ya maisha sisi sio wenye kuonewa na mazingira. Bali ni fikra zetu wenyewe.
Kwa kukubali
majukumu yako, utasimamia matatizo yako na utasimamia maisha yako.
Tupo sehemu ambayo tupo katika maisha yetu sio kwa sababu ya watu wengine, isipokuwa ni kwa sababu yetu sisi wenyewe.
2: Kufanya badala ya Kuongea
Sote tunamjua
Mvulana haijarishi umri wake anaeongea sana kwa kujigamba.
Mara zote yeye hujisifu ni wanawake wangapi kalala nao, pesa kiasi gani anatengeneza, na uwezo wake wa kupambana.
Huyu mtu mara nyingi huwa na story nzuri ambazo huenda na majigambo, Mwisho wa siku yote huwa ni maneno tu.
Kuwa
mwanaume wa wanawake au mwenye kutumia pesa au mwenye kupambana vema, inataka Kazi.
Wavulana huchukua mbinu rahisi na kujaribu kutaka kufikia hadhi wanayoitaka na hufanya hivyo kwa kujigamba. Hadhi ya hivi sio ya kweli.
Na hali yoyote ya kweli ikitokea kumtaka athibitishe majigambo yake hufichua siri yake.
Wanaume wanajua kuongea ni Rahisi sana na
matendo huongea zaidi kuliko maneno.
- Jua ni muda gani wa kufunga mdomo wako?
- Jua ni muda gani wa kuinamisha kichwa chako?
Na fanya kazi zako na ujitume kimya bila kulalamika hata kidogo
Wanaume huangalia zaidi katika vitendo kuliko maneno.
3: Hili ni gumu kwa wanaume wengi.
Acha kucheza magemu na acha kupiga punyeto
Kucheza magemu inaweza kuwa ni raha yenye kuvutia sana Isipokuwa unatakiwa ufahamu kwamba yametengenezwa safi kwa ajili ya tamaa zako za ndani kama
mwanaume.
Unafikiria ni nini kinachowafanya
wavulana na
wanaume ambao ni wapuuzi wanakuwa na uraibu wa kucheza magemu?
- Changamoto
- Ushindani
- Hadhi
- Utawala
- Ushindi
Magemu mengi yenye kuuza sana ni yale yaliyotengenezwa kwa ajili ya kuchezesha maisha ya
Uanaume na tamaa zake,
Mafanikio haya kwenye magemu ni
Fake.
Na ukilewea kwenye michezo ya magemu basi umejitupa kutoka katika Tamaa yako ya mafanikio na nguvu ya maisha katika ulimwengu wa kweli.
Njia nyingine ya kujipoteza kwenye uhalisia wa
Uanaume wako ni
KUPIGA PUNYETO kutokana na video za ngono mtandaoni. Huu ni Ushindi bandia.
Unachoangalia ni watu wengine huna uwezo wa kumfuata mwenza jinsia tofauti na yako pia utashindwa kufanya tendo wewe mwenyewe elewa hili.
Na ukweli ni kwamba wanaume wengi wenye matatizo ya nguvu za kiume sababu yake ni hii.
4: Tawala Hisia zako
Wavulana mara nyingi hufanya chochote wanachojihisi,
Wanaume hufanya wanachotakiwa kufanya Ikiwa watajihisi kukifanya au hawajihisi kufanya.
Tunaishi katika jamii inayojaribu kwa nguvu sana kuwafanya
wanaume wawe kama
wanawake.
Jamii hujaribu kuwaambia
wavulana na
wanaume kujielezea hisia zao na kuwa wawazi kihisia.
Muhula wa kukaza na kuwa
mwanaume thabiti unaonekana kama
SUMU.
Na hapo ndipo mambo huanza kugeuka.
Wanaume na wanawake huelezea hisia zao katika njia tofauti;
WANAWAKE:
Unapowaambia mwanamke wafunguke na waache kujizuia hisia zao. wao huongelea hisia zao na wanaweza kulia.
WANAUME:
Unapowaambia wanaume wafunguke na waache kujizuia hisia zao. Na wasikilize hisia zao wanaweza kuwa wakatili sana.
Unaweza kumtandika mtu barabarani kwa sababu tu unasikiliza hisia zako badala ya kuzitawala
Utawala wa kihisia ni moja kati ya Msingi wa
Kiume.
Asilimia 99 ya watoto watukutu Africa hutokea katika malezi ya Nyumba yenye Mama asiye na mume.
Baba huweka na kulazimisha misingi ya heshima, adabu na amri ndani ya Nyumba.
Ikiwa hakuna malezi ya
Ubaba basi utaona Jamii inawalazimu
wavulana kusikiliza hisia zao.
Na hapo ndipo Mambo mabaya hutokea upesi sana,
Hii haimaanishi kwamba kila kitu lazima Ukifunge katika kifua chako kama mwanaume.
Kama kuna jambo la kutaka umakini sana. Unatakiwa kuongea na kaka zako au Rafiki yako sehemu ya mazoezi.
Kwanza kabisa unatakiwa kujitoa kwenye Jambo hilo kisha ulitizame kwa ukamilifu. Mara nyingi mambo huwa sio makubwa au mazito sana kama tunavyo yachukulia.
Wanaume bora utakao kutana nao ni wenye kuweza kutawala hisia zao.
Hisia sio mbaya, Hisia zinazotumika vibaya, Ni mbaya.
Wanaume wengi huanza kwenda Gym na kutengeneza Nguvu katika miili yao kwa sababu ya Hasira,
Wengi wao walishawahi kunyanyaswa.
Huu ni mfano mzuri wa kuongoza hisia zako. Na kuutumia katika faida. Ukilijua hili katika akili yako. Utashangazwa na uwezo kiasi gani ulionao kama
mwanaume.
Rakims