What is the Point........................

What is the Point........................

MwanajamiiOne

Platinum Member
Joined
Jul 24, 2008
Posts
10,470
Reaction score
6,580
Dear WanaJF............
Habari zenu?

Katika hizi siku za karibuni kuna matukio yaliyojitokeza ambayo yamenifanya niwaze na kujiuliza maswali mengi sana. Hasa hili suala la Mainfii ambao wamezaa na waume za watu.............. kwa nini wengi hujitokeza kumreveal mtoto alozaa na baba flani pale ambapo mhusika mkuu amefariki? Yaani anaposikia tu infidelator ambaye ni mume wa mtu amefariki au anaumwa sana ndo anakuja kuclaim kuwa amezaa na marehemu?? Nina maswali makuu manne katika hili jambo.....
1. Huwa wanapata wapi nguvu na ujasiri wa kujitokeza kuwa nimezaa na mume wa mtu (Nazungumzia wale ambao watoto husika huwa wamezaliwa wakati jamaa yuko ndoani- yaani kithibitisho cha kuinfidelate--- mtoto ni mdogo zaidi ya umri wa ndoa halali)?
2. What is the point... nini hasa matazamio (Mhusika ameshafariki wewe kama infidelatee ambaye umezaa na marehemu- unakuwa unatarget nini wakati unapojireveal/mreveal mtoto wakati babake ameshafariki?
3. Je kuna tofauti ya kujireveal kati ya mwanamke ambaye anajimudu kimaisha yeye na mwanaye (ambaye ameamua tu kuzaa na mume wa mtu for the sake ya kuzaa) na mwanamke ambaye bado ni tegemezi (let say mwanafunzi au kina Eliza)?? na
4. Kuna wanaume wanaojitokeza kudai watoto iwapo wanajua kabisa (na wana ushahidi ) wa kuzaa na mke wa mtu??

Sina majibu ya haya maswali waungwana ninaomba mnisaidie.
Aksanteni
( Teamo, please usikwesheni muda wa kurushwa kwa sredi- just spare me)
 
Wanataka mgao wa urithi!!!

Aksante LIZZY huoni kama wanafanya gambling??.....waht is the point of them having the babies?? what if wao ndo watatangulia kufa?? Haimake sense


But if that is the case kuna namna tunawezakuwacategorise kuwa wanawake wa aina hii huwa wanaexpect this therefore tuwaavoid?.....hii ingewasaidia sana kaka zetu katika kumake decision on how to choose.......kama wale ambao ni tegemezi ndo the onces who are likely to make "noise" wao wakishakufa basi wachague watu wa kuinfidelate ao au kama ni wale wanaoclaim kuwa independent.............ili wasijicommit
 
Aksante LIZZY huoni kama wanafanya gambling??.....waht is the point of them having the babies?? what if wao ndo watatangulia kufa?? Haimake sense


But if that is the case kuna namna tunawezakuwacategorise kuwa wanawake wa aina hii huwa wanaexpect this therefore tuwaavoid?.....hii ingewasaidia sana kaka zetu katika kumake decision on how to choose.......kama wale ambao ni tegemezi ndo the onces who are likely to make "noise" wao wakishakufa basi wachague watu wa kuinfidelate ao au kama ni wale wanaoclaim kuwa independent.............ili wasijicommit


Sidhani kwamba hua wanapanga ila inapotokea anaona oportunity ile pale anaamua kuichukua!!!

Tatizo hawa kaka zetu nao wakati mwingine wala hua hawaangalii.....wanachukua tu!!

Ila kusema ukweli wapo ambao unakuta hawahitaji chochote zaidi ya kwenda kujionyesha tu huko...na kumwonyesha mama mwenye nyumba kiburi na kumuongezea uchungu!!!Wengine utasikia eti nataka awajue ndugu zake....utadhani siku zote hakuona umuhimu huo mpaka itokee mwenye mtoto hayupo kumzuia tena!!!

Binafsi hua nashindwa kuelewa mtu anapata raha gani kua na mtoto na mtu ambae hata kumtambulisha huyo mtoto kwao hataki!!!:twitch:
 
Mh mie nakumbuka mwaka juzi.....mjombaangu alikuwa hoi taabani anapumulia mipira....and there she came.....ajabu mwanaye huyo alikuwa ni mkubwa kuliko mtoto wa kwanza wa mjomba na shangazi (RIP)........I was shocked yaani niko Agakhan natafakari litakalijiri (hasa baada ya kuiona hali ya mjomba) anakuja mtu ananiambia unajua mie nina damu yenu........nilitamani nimmeze na nguo zake..............but we thank GOD shangazi yangu ni mwelewa......shez an angel who lives in this planet................
 
inawezekana wakati wa uhai wa jamaa huyo
bibie anaona huruma kuja mtambulisha mtoto asije
akamzushia soo "mzazi mwenzake". sasa maadamu
jamaa ametangulia mbele za haki anaona hilo
soo halitakuwepo kwa "mzazi mwenzake"
 
Mwanamke yeyote mwenye jeuri tu ya kuwa na uhusiano na mume wa mtu muogope kama si kumheshimu.....kajitoa mhanga,yaani liwalo na liwe,so sishangai akija kudai mali mwanaume akifa....na lazima awe na guts anazopewa na mwanaume mwenye mkewe na pengine uwezo wa kuzaa anao au hata watoto,kumuacha mkewe kwenda kwake,hapo ndo jeuri yao inatoka

Wengi wa infii ni tegemezi kwahiyo mume anapofariki,wanataka matunzo ya mtoto na at the same time ya kwao,so kwa kujitambulisha kwa familia anategemea msaada,wale ambao ni infi by choice na wana uwezo hupenda tu heshima,kwamba mtoto ajue ndugu wa baba yake......

Tofauti ya kuji-reveal ipo,wanaolia shida na wanaokuja na confidence lao hawafanani ujio wala namna wanavyopokelewa kwa familia ya baba aliofariki,kina Eliza tabu kweli vikao vingi but mwenye nazo kwanza pengine marehemu anakuwa ashasema nina mtoto nje.......

Wapo wanaume wanaojitokeza kudai watoto,nimeshuhudia zaidi ya mara nne wanaume wenye ndoa wanakuja na kudai watoto ni wao na kutaka watoto wawatambue kama baba na wanatimiza majukumu yao..........
 
Mi najiuliza... ikitokea mama ndo amefariki? Mtoto c atalazimika kulelewa na baba yake? Hilo soo...dah ngoja nilale....
 
umuhimu wa mtoto kumjua baba yake halisi ni mkubwa mno

kuliko swala la jamii kuona ulizini au ulitembea na mume wa mtu.....

suppose mtoto ana magonjwa ya kurithi aumatatizo mengine kama blood group au hata
wenye asili ya mashetani......

vyovyote vile iwe sawa si sawa kutembea na mtu mwenye ndoa yake......

lakini umuhimu wa mtoto kujua asili yake na ndugu zake wa damu ni mkubwa mno....

watoto wengine huwa na tabia za ajabu ukichunguza ni za asili huko kwao...
labda babu yake alikua hivyo hivyo.....
 
kuna mambo mengi yanayochangia haya kutokea
1.inaweza ikawa kabisa hawa walikubaliana lakini sababu tu mume anamuelewa mkewe atajaribu kuficha siri awezavo lakini anahudumia mtoto.
2.wengine huzaa bila matakwa ya hawa wanaume na chance pekee watayopata ni pale huyu baba anapofariki kumtambulisha mtoto.
3.tunajua kabisa kiburi cha wamama tulio na ndoa mara nyingi huwa tunatoa adhabu zisizostahili kwa hawa viumbe amabo hawana makosa kwaiyo mume anaona bora akae kimya kuliko kumpa mateso huyu mtoto.
4.bado wanandoa wengi tunaishi maisha yasiyotazama ukweli wa yale yanayoendelea kwenye dunia yetu ndo pale unapomkuta mdada mume anaongea tu story kuhusu mwanamke mwingine tayari mama analianzisha wiki nzima haongei.tujifunze kuelewa kusoma saikolojia ya jinsia nyingine itatupa sana amani na kupunguza mambo meni tunayolalamikia so far alishakupenda akakuoa amini ivo na uendelee kujiamini.

wapo wanaume nao huwa wanadai watoto wao nimeshashuhudia viburi,ujuaji mwingi kutojali ni chanzo cha matatizo mengi ndani ya ndoa tujifunze kuwa wa wazi kwa wenzi wetu unalowaza ,unachotamani mshirikishe mwenzako na tujitahidi kuwa na positive thoughts itatusaidia sana kupunguza hii migogoro.
 
Ni makosa makubwa sana haya tunayafanya ila sasa ndio hivyo tena dunia yetu hii mtihani.
 
Back
Top Bottom