What is Wrong with Tanzania?!. Tunashindwa Nini Kufikisha Bidhaa Zetu Kwenye Masoko ya Kimataifa?!.

What is Wrong with Tanzania?!. Tunashindwa Nini Kufikisha Bidhaa Zetu Kwenye Masoko ya Kimataifa?!.

Bila ccm kuondoka madarakani usitarajie jipya!!
Inawezekana ccm wabovu lkn mbadala wa ccm bado hakuna kwa sab waliokuwepo ni wabovu kuliko ccm. Kwa mfano mamvi ndiye ataleta madiliko? Anayetaka urais ili amkomeshe kikwete? Mtu aliyethibitishwa kuwa ni fisadi na chombo chenye mamlaka kikatiba? Au chadema chama cha kifamilia? Au cuf chama chenye makundi? Tanzania upinzani wenye uwezo wa kutawala nchi bado haujatokea.
 
Siku hizi inaitwa TanTrade
Tatizo sio tantrade ni sisi mtanzania mmoja mmoja hatuna mwako wa kutafuta fursa za nje na kutafuta taarifa sahihi kwa watu kama hawa tantrade. Pia ni wavivu linapokuja suala la kukidhi viwango vya kimataifa tunaona kama mzigo mzito maana tunapenda vitu rahisi na njia za mikato. Ndio maana hivi hivi vyetu Wakenya wananunua wanaboresha kukidhi viwango wanauza ulaya
 
Hili ndio jibu mkuu! Hayo mengine hayana maana! Na ndio mpaka sasa tunaendelea kuona uozo na maigizo ya kutosha!! Tutangoja sana! So far nawapongeza sana India na South Africa kwa kuwa wauzaji bora wa tanzanite!
Usirudie kuedit comment yangu plz
 
1. Hatuna mtaji wa kutosha
2. Bidhaa zetu duni/Hatuziongezi thamani kukidhi viwango vya Kimataifa
3. Kizingiti cha lugha/Language barrier(Kizungu hatujui vizuri,kiarabu hatujui vizuri,Kifaransa ndo kabisaa)
4. Hatuna Middle men/women wenye udiriki, wengi wamezoea kutupiga tu humu soko la ndani

BIDHAA TUNAZO...Njombe pale kuna Apple fruits nzuri sana ila zinauzwa na akina mama kwenye mabasi na nyingine zinaoza, Mufindi Muheza kote huko kuna Matunda ya kila aina na kwingineko Tz.
Maua tunayo.
Tukuyu Parachichi mbegu bora zipo ila zinaozea chini
Nyanya Ilula zinazalishwa na eneo linasapoti kila varieties lakini hatuwezi kuuza nje etc...Elimu,Elimu,Elimu
 
1. Hatuna mtaji wa kutosha
2. Bidhaa zetu duni/Hatuziongezi thamani kukidhi viwango vya Kimataifa
3. Kizingiti cha lugha/Language barrier(Kizungu hatujui vizuri,kiarabu hatujui vizuri,Kifaransa ndo kabisaa)
4. Hatuna Middle men/women wenye udiriki, wengi wamezoea kutupiga tu humu soko la ndani

BIDHAA TUNAZO...Njombe pale kuna Apple fruits nzuri sana ila zinauzwa na akina mama kwenye mabasi na nyingine zinaoza, Mufindi Muheza kote huko kuna Matunda ya kila aina na kwingineko Tz.
Maua tunayo.
Tukuyu Parachichi mbegu bora zipo ila zinaozea chini
Nyanya Ilula zinazalishwa na eneo linasapoti kila varieties lakini hatuwezi kuuza nje etc...Elimu,Elimu,Elimu
Hatuna mtaji wa kutosha wakati tunanunua mapangaboi kwa cash??
 
Hakuna sapoti kutoka kwa serikari kwenda kwa mkulima au mfanya biashara, viongozi husika hawajari wakulima/wafanya biashara zaidi ya kumpendelea mgeni kwani kuna pesa wanapata. Mfanya biashara au mkulima ili upeleke bidhaa zako nje kuna vikwazo vingi hasa vya kipesa kwasababu itakubidi utoe sana pesa.
 
Sina cha kujitetea kwakwel,nadhani watanzania tuna upungufu wa taarifa nyingi za muhimu kuhusu hatua mbali mbali za kufanikisha mirad kama hiyo,..watanzania hatupeani motisha,kila mtu anafanya kivyake vyake,wanaojua fursa wanafanya siri etc.pia kukwamishana katika process nzima,mfano mtu unataka kufanya kitu mathalan uchimbaj wa madin haya ya viwandan,unakuta vijij vimepewa mamlaka ya kumiliki haya maeneo sasa unapojitokeza wew kukata lesen na kukamilisha mengne,unashangaa mkutano wa kijij unakuja na kodi ambazo sio elekezi na za juu kwelkwel,kias kwamba mfanyabiashara unakimbia kwan haziko kifaida,plus una kodi ya serikali kuu ambayo ni ya lazima,siikatai ila hizi za vijij znaharib sana harakat,yan inakua kama kijij kinataka shida zao zote uzimalize wew akat wew ndo kwanza unaanza na ni mchimbaj mdogo mdogo,sasa namna hii hatufiki
Hii ni hoja yenye mashiko.
 
Sisi hatuna muda wa kuongelea masuala ya biashara, tunachokiweza ni kufungua M-PESA, GROCERY, MADUKA YA BIDHAA na BAA then tunafanya kazi ya kubeba mikoba ya wanasiasa na kutukana SERIKALI Mitandaoni, KUTUKANA RAIS.
* Tunaangalia MANGE KIMAMBI kaandika nini
* Propaganda gani tuanzishe
* BASHITE
* Tangu serikali ya A5 Imeanza hatuna mjadala wowote wa maana sisi wenyewe zaidi ya kuponda serikali na KUWAZA UCHAGUZI Wakati KENYA ni WAZOEFU WA HIZO KAZI TANGU UKOLONI
Mkuu Mkaruka, anzisha basi huo mjadala wa maana, na sisi tutachangia na kuisifu serikali yetu, badala ya kuiponda!.

Paskali
 
Back
Top Bottom