Mitaji sio tatizo mkuu.Ni ukosefu wa mitaji pengine,
IN TIME BE POSITIVE!Mazao ni malighafi na malighafi tunazo nyingi, ishu ni ubora wa bidhaa tunazozalisha kutokana na hizo malighafi.
Je, bidhaa zetu zimekidhi viwango vya kimataifa kiasi cha kuleta ushindani kwenye soko la kimataifa?
Wapinzani hawa wa kutegemea Tungo za mitandaoni hawawezi kufanya lolote zaidi ya kuinyonya na kuirudisha nyuma tanzania hatua zaidi ya 100000. Wasipobadilika kama CCM wanavyojaribu kujibadili wataendelea kutofaa hadi siku ya kiyama.Wewe Chikundi hebu acha kujiabisha kwa hoja za kijinga, unawaharibia CCM zaidi . . , kama huwezi kujadili kacheze mdako . .
Ndio nimekubaliana na Paschal kuwa ccm ni mbovu sana lkn upinzani zaidi hivyo hatuna mbadala kwa sasa .Chikundi,
Unachotaka kuwaaminisha wana JF ni kuwa mtu akiwa ccm, basi regardless yeye ni Bashite type or what , tayari anafaa kuongoza nchi . .? !
Ni lini hao wa vyama mbadala wamepata madaraka ya nchi wakashindwa kazi . . ?!
Ushahidi upo wazi, na ndio maana Paskal ameanzisha mjadala hapa, CCM wameshindwa ku support sekta binafsi kwa ujumla, wachilia mbali kufanya EXPORT . .
Sababu ntazitoa chache . . ,
1. Tanzania kisiasa, tangu tupate Uhuru . . , biashara kwa ujumla haikuwa ni jambo lililokuwa na Sera wezeshi na rafiki kwa watanzania . . Biashara zote zilikuwa zinafanywa na SERIKALI. Mashirika ya UMMA , RTC, BET, BIT, wahindi na wageni, BODI ZA MAZAO, VYAMA VYA USHIRIKA ndio waliokuwa exporters . . Mtanzania (mzawa) alipata taabu sana kufanya biashara nchi hii, nao waliitwa walanguzi tuu . .
2. Tanzania, na hasa ccm, walipoamua kukubali nchi iwe ya vyama vingi . . , bado wakaendelea kungangania Sera zao zilezile za UJAMAA . . , ila kwa HILA wao wakaanza kupora mali za UMMA kwa kisingizio cha UBINAFSISHAJI . .
Kwa sababu ccm walituingiza ktk siasa za kibiashara/kibepari kwa hila, ni wao tuu, viongozi wachache ndio waliokuwa na uelewa wa kuchangamkia fursa za biashara/export . . Walifanya hivyo wakishirikiana na watanzania wenye asili ya ki Asia na wageni wachache . .
3. SIASA ni sababu nyingine inayorudisha nyuma sana watanzania kufanya exports . .
Hata baada ya miaka zaidi ya 50 ya kujitawala, eti mtanzania hawezi kuuza mahindi yake kwa uhuru kabisa hata hapo Kenya tuu . . Kila exports ina cumbersome restrictions, ucheweleshaji wa documents processing for exports na mengi tu ya hovyo . .
Paskali, tatizo ni la CCM by 80% . . , ndio maana ni ngumu kufanya exports nchi hii . .
Jibu hoja acha personal attack hii ni forum ya great thinkers sio dumb thinkers.Wewe Chikundi hebu acha kujiabisha kwa hoja za kijinga, unawaharibia CCM zaidi . . , kama huwezi kujadili kacheze mdako . .
Hii ni hoja inayostahili kujadiliwa kwa kina kitaifa. Nafikiri sababu moja wapo ni ya kihistoria fikiria kuna wakati ilikuwa hata kijijini (baadhi) huruhusiwi kufanya ujasiriamali hata wa mgahawa tu, kila kitu kifanywe na kijiji, ubunifu ulifubazwa. Mazingira ya uthubutu na ubunifu ni hafifu sana kuanzia shule za msingi hadi taifa. Badala ya kuweka kipaumbele katika katika vitu kama mashindano mathalani ya urembo miss so and so ingekuwa mashindano ya ubunifu wa uzalishaji na teknolojia kuanzia kijijini hadi Taifa na Mheshimiwa Rais anatoa tuzo kwa watu au taasisi waliofanya au zilizofanya ubunifu wenye tija kila mwaka. Ni shule chache zinaendesha debate (mambo mbalimbali ikiwemo biashara za ndani na nje) hivyo vijana wanashindwa kuendeleza stadi za kukabiliana na changamoto za kitaifa na kidunia. Udhaifu huu pia unasababisha raia kulalamikia serikali kila siku kwa kila jambo ningefurahi ifike siku serikali ishangae mbona raia sio lialia tena, kila changamoto wanajiongeza kama akili zimehama!Wanabodi,
Tanzania kama nchi, tunakabiliwa na tatizo kubwa la Wafanyabiashra wa Tanzania, kushindwa kuingiza bidhaa zetu kwenye masoko ya kimataifa!, tatizo ni nini?!.
Mifano.
Tanzania ndiye mzalishaji pekee wa madini ya Tanzanite, lakini katika masoko ya kimataifa, nchi inayoongoza kwa kuuza Tanzanite ni India, ikifuatiwa na Afrika Kusini, Lebanon, Kenya halafu ndio sisi wenye Tanzanite zetu. Kwa vile Tanzanite inapatikana Tanzania pekee, data za export market ni zile za cut and polished stones, hii inamaanisha ni Tanzanite nyingi inachimbwa na kuuzwa un cut kuliko ile tunaicharanga wenyewe!.
Tanzania iko kwenye top ten wazalishaji wa korosho. Mnunuzi mkuu wa Korossho ya Tanzania ni India akifuatiwa na Kenya, lakini kwenye urari wa soko la processed nuts, Kenya ana export korosho nyingi zaidi sokoni kuliko Tanzania, huku sisi tukiuza korosho isiyobanguliwa!.
Kwenye nchi za Afrika Mashariki, Kenya ndio inaongoza kwa kuuza vinyago ulaya, na hakuna nchonga vinyago Kenya, vyote wananunua kutoka Tanzania, Kenye ndiye muuzaji mkuu wa unga wa sembe kwenye masoko ya ulaya, lakini mahindi yote wananunua kutoka Tanzania!.
Kwenye fursa za AGOA, Watanzania tumeshindwa kuchangamkia hiyo fursa!, Wakenya wanakuja Tanzania, wananunua bidhaa, na kupeleka Kenya, kule wana process na packing na branding, then zinaingia masoko ya kimataifa as products of Kenya!. What is wrong with sisi Watanzania?!.
Katika kusaidia kwenye hili, Taasisi ya Trademark East Africa, inajaribukutusaidia!.
MICHUZI BLOG: Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.
MATUKIO @ MICHUZI BLOG: Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.
Paskali
I am always truthful and positive!IN TIME BE POSITIVE!
Ndio nimekubaliana na Paschal kuwa ccm ni mbovu sana lkn upinzani zaidi hivyo hatuna mbadala kwa sasa .
Umeuliza Nina ushahidi gani kuwa vyama vya upinzani haviwezi kwa sab havijawahi kushika nchi. Lkn kabla sijajibu kwanini sidhani hata wewe kama unaweza kujibu umejuaje kama upinzani utaweza bali unaamini kutokana na failure ya ccm kwenye nyanja kadhaa bali hujui chama kinavyoendesha mambo yake ni picha tosha ya kukihukumu kama kinaweza kuongoza nchi ama la.
[emoji115]
1.( Tulipopata Uhuru 1961, TANU ilikuwa imeshaendesha Nchi na Serikali gani kabla ya hapo . . ? Wakati huo hatukua na madaktari, wala ma engineers. Hiki ni kisingizio cha kitoto . . )
Tukianza kwenye Mfumo.
Chadema ni chama cha kifamilia ushahidi unaonyesha mwenyekiti wake wake wa kwanza mtei alimuachia uenyekiti Shemeji yake Bob makani kisha akaagiza apewe mkwe wake baada ya Shemeji kufariki na mpk sasa yupo kwa miaka 14.
[emoji115]
2.( Sheria za Nchi haziruhusu vyama vya SIASA kujengwa kwa misingi ya KIDINI, KIUKANDA, KIKABILA, WALA KIFAMILIA .., Msajili wenu wa Vyama vya SIASA ana nguvu ya kufuta chama cha kifamilia kama CHADEMA . . , kwa nini mpaka sasa hajakifuta . . ?! )
Mfumo kama huu lazima utajitokeza pia kwenye utawala wa nchi kitu ambacho ni hatari.
[emoji115]
3.(Kwa jibu langu no 2, hii hoja yako sasa ni ya ki BASHITE . . , Muungano wa vyama vya upinzani, UKAWA, ktk uchaguzi uliopita walipata ushindi wa kura za Uraisi zaidi ya 40% . . , Watanzania milioni 6+, na wewe Chikundi nani ana akili . . ?!)
Tuje kwenye kusimamia katiba
Wameshindwa kusimamia katiba na makubaliano mbali mbali kuanzia chadema mpk ukawa
Wamembrand lowassa kama fisadi nchi nzima kwa miaka minane lkn all of the sudden wakasema ni msafi na kumpa nafasi ya kugombea urais huku wakikiuka katiba yao wenyewe kwani inasema kabla ya mwanachama hajagombea urais lazima afikishe miezi sita chamani lkn lowassa alikaa wiki moja tu chamani akapewa nafasi ya kugombea urais bila mchakato wowote. Hii ikapelekea wakongwe wawili Dr slaa na lipumba kujiengua.
[emoji115]
(Hizi ni POROJO za ccm . . , na ndio maana unaweza kuwasifu Fr Slaa na Lipumba kwa sababu mmefanikiwa kuwanasa kwa njaa zao . ..)
Lkn vyama vilikiuka makubaliano yao kuwa ndani ya ukawa majimboni watoe mgombea mmoja lkn walishindwa kufanya hivyo matokea yake majimbo ya Masasi na ukonga walisimamisha zaidi ya mgombea mmoja.
Nao Cuf baada ya kuvunja sheria ya kujitangazia ushindi wakasusia uchaguzi uamuzi ambao unawatesa wanacuf wa znz mpk Leo kwani wamekosa wawakilishi ambao ni chaguo lao hakuna asiyejua pemba wamekuwa wakiwakilishwa na cuf tokea vyama vingi vianze. Hii yote ni sab ya ubinafsi.
[emoji115]
( Habari ya uchaguzi ZNZ, kila mwananchi mwenye akili yake timamu anajua CUF walishinda, ila ÇCM kama kawaida yenu kufanya WIZI, mkambana Jecha afute matokeo . .)
Hali imejidhihirisha kwa uongozi wake wa juu kugombea ofisi vyeo na ruzuku.
Sasa vyama kama hivi unavipa uongozi wa nchi nzima kwa mazingira gani? Ubunge sawa sio urais.
Hoja imejibiwa kuwa ccm imefeli[emoji115]
SASA, HOJA YA PASKALI KUHUSU EXPORTS HAPA HAIJAJIBIWA, ILA UMEENDELEZA SARAKASI KAMA KAWAIDA YENU CCM.
MMEFILISIKA KIAKILI, NI WIZI TUU . . , NA ROHO MBAYA . . !
TUKIENDELEA NANYI HATUTAWEZA KUFANYA LA MAANA NCHI HII . .
Point mkuu, unakuta huko Duniani kuna makongamano kibao ya biashara ika hutakuta MtanzaniaMwai kibaki aliwahi kutuambia watanzania ni waoga kutoka ndani ya nchi yao.
Badiliko kubwa la haraka na la lazima lifanyike nchi nzima ili bongo zetu ziachane na local mentality
Hivi Paskali hufahamu kuwa Kenya na Tanzania ni nchi mbili tofauti kiuchumi? Tanzania ni nchi ya kijamaa na Kenya ni nchi ya kibepari. Buy/process/pack and sell or manufacture/pack and sell ndiyo mfumo wa kiuchumi Kenya(ubepari). Sisi Tanzania ni Lima/zalisha then mpe dalali auze.(ujamaa). Chukulia mfano zao la chai. Nchi ya Burundi inauza chai kwenye soko la dunia, lakini Tanzania chai wananunu Wakenya na kwenda kuiuza soko la dunia. Akili zetu ni za kidalali tuuWanabodi,
Tanzania kama nchi, tunakabiliwa na tatizo kubwa la Wafanyabiashra wa Tanzania, kushindwa kuingiza bidhaa zetu kwenye masoko ya kimataifa!, tatizo ni nini?!.
Mifano.
Tanzania ndiye mzalishaji pekee wa madini ya Tanzanite, lakini katika masoko ya kimataifa, nchi inayoongoza kwa kuuza Tanzanite ni India, ikifuatiwa na Afrika Kusini, Lebanon, Kenya halafu ndio sisi wenye Tanzanite zetu. Kwa vile Tanzanite inapatikana Tanzania pekee, data za export market ni zile za cut and polished stones, hii inamaanisha ni Tanzanite nyingi inachimbwa na kuuzwa un cut kuliko ile tunaicharanga wenyewe!.
Tanzania iko kwenye top ten wazalishaji wa korosho. Mnunuzi mkuu wa Korossho ya Tanzania ni India akifuatiwa na Kenya, lakini kwenye urari wa soko la processed nuts, Kenya ana export korosho nyingi zaidi sokoni kuliko Tanzania, huku sisi tukiuza korosho isiyobanguliwa!.
Kwenye nchi za Afrika Mashariki, Kenya ndio inaongoza kwa kuuza vinyago ulaya, na hakuna nchonga vinyago Kenya, vyote wananunua kutoka Tanzania, Kenye ndiye muuzaji mkuu wa unga wa sembe kwenye masoko ya ulaya, lakini mahindi yote wananunua kutoka Tanzania!.
Kwenye fursa za AGOA, Watanzania tumeshindwa kuchangamkia hiyo fursa!, Wakenya wanakuja Tanzania, wananunua bidhaa, na kupeleka Kenya, kule wana process na packing na branding, then zinaingia masoko ya kimataifa as products of Kenya!. What is wrong with sisi Watanzania?!.
Katika kusaidia kwenye hili, Taasisi ya Trademark East Africa, inajaribukutusaidia!.
MICHUZI BLOG: Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.
MATUKIO @ MICHUZI BLOG: Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.
Paskali
Mkuu, nadhani hili tatizo ni la kutokua na mwamko wa fulsa za kibiashala za kimataifa akiwemo mtoa mada mwenyewe.Mkuu mimi ninachofahamu, kwanza sisi wenyewe hatuthamini vya kwetu. Hili tuliache kwanza.
Tunawapa wenyewe- faida ya udalali hiyoHizo Tanzanite India inayoongoza kuuza, na Afrika ya Kusini, wanazipata wapi?!. Hivyo vinyago hao Wakenya wanavipata wapi?!. Hayo Mahindi jee?.
Paskali
No, hiyo isue ni ya sisi wananchi, na mfumo wetu wa utawala. Viongozi wetu hawana tofauti na sisi wananchi wa kawaida wote ni madalali tuu. Mwananchi akiamka na kupambana kiuchumi, organs za kiserikali ni kuasidia kutimiza malengo na juhudi za mwananchiKuna taasis za serikali hazijui kazi zake mfano BET
Ishu sio mitaji, ishu ni matangazo ya biashara (marketing) na lugha pia. Alafu Kingine Customers care tupo nyuma sana. Na ndio maana mahotel mengi wanataka kuajiri Wakenya kwa sababu wanafundishwa customers care.Ni ukosefu wa mitaji pengine,
Uko sahihi kabisa tumefeli kwenye eneo hili mfano halisi niliwahi kuomba BET wakati huo nafasi ya kwenda kwenye exhibition ya kazi za mikono Osaka Japan nafasi ambayo serikali ya Japan imewapa bure bileshi Tanzania ili isaidie wafanyabiashara wadogo wa Sanaa za mikono lkn baada ya kupata nafasi hiyo nilitakiwa nilipe ada ya ushiriki(participation fee) niwe na mzigo wa kuonyesha na kuuza niwe na nauli pesa ya kula pesa ya usafiri wa mzigo kutoka Tanzania mpk Japan pesa ya kutolea mzigo Japan hizo pesa zilikuwa nyingi kwa mfanyabiashara mdogo kumudu hivyo nilishindwa.Wanabodi,
Tanzania kama nchi, tunakabiliwa na tatizo kubwa la Wafanyabiashra wa Tanzania, kushindwa kuingiza bidhaa zetu kwenye masoko ya kimataifa!, tatizo ni nini?!.
Mifano.
Tanzania ndiye mzalishaji pekee wa madini ya Tanzanite, lakini katika masoko ya kimataifa, nchi inayoongoza kwa kuuza Tanzanite ni India, ikifuatiwa na Afrika Kusini, Lebanon, Kenya halafu ndio sisi wenye Tanzanite zetu. Kwa vile Tanzanite inapatikana Tanzania pekee, data za export market ni zile za cut and polished stones, hii inamaanisha ni Tanzanite nyingi inachimbwa na kuuzwa un cut kuliko ile tunaicharanga wenyewe!.
Tanzania iko kwenye top ten wazalishaji wa korosho. Mnunuzi mkuu wa Korossho ya Tanzania ni India akifuatiwa na Kenya, lakini kwenye urari wa soko la processed nuts, Kenya ana export korosho nyingi zaidi sokoni kuliko Tanzania, huku sisi tukiuza korosho isiyobanguliwa!.
Kwenye nchi za Afrika Mashariki, Kenya ndio inaongoza kwa kuuza vinyago ulaya, na hakuna nchonga vinyago Kenya, vyote wananunua kutoka Tanzania, Kenye ndiye muuzaji mkuu wa unga wa sembe kwenye masoko ya ulaya, lakini mahindi yote wananunua kutoka Tanzania!.
Kwenye fursa za AGOA, Watanzania tumeshindwa kuchangamkia hiyo fursa!, Wakenya wanakuja Tanzania, wananunua bidhaa, na kupeleka Kenya, kule wana process na packing na branding, then zinaingia masoko ya kimataifa as products of Kenya!. What is wrong with sisi Watanzania?!.
Katika kusaidia kwenye hili, Taasisi ya Trademark East Africa, inajaribukutusaidia!.
MICHUZI BLOG: Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.
MATUKIO @ MICHUZI BLOG: Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.
Paskali
Kwanini wachimbaji wenyewe wasiende kuuza nje hata wamiliki wa migodi?Wanunuzi wengi wa Tanzanite pale Arusha ni wahindi,wakenya,wachina,na apolo kutoka SA. Wafanyabiasahara wakitanzania wachache ndio wanaweza kununua madini na kwenda kuuza nje.
Mtumie imezidi page tanoHiyo mijadala ya maana haina wachangiaji, hata huu wa kwako ukifika hata page 5 leo ni PM namba yako nikutumie pesa ya soda
Maziku haya maswali yako unarudia maswali ya hoja(thread) kuu aliyoleta Paschal(Paskali). Na ndio tunahitaji majibu hapo haujajibu you are just spinning around. Ningeshauri tungejikita ktk kutafuta chanzo cha tatizo kwa namna au lengo la kupata ufumbuzi au njia mbadala kuliko kutafuta wa kumlaumu bila kupata ufumbuzi. Tufanye kama mbinu zinazotumika ku-improve human performance ktk industry ya aviation hasa civil aviation. Kule kukitokea tatizo wanatafuta chanzo nini sio nani, wanatafuta chanzo nani ili kupata historia kabla ya tukio ili kutambua vyanzo vya human errors na mazingira ya kazi kama yalichangia tatizo (i.e. Fatigue and ergonomics or other health and physicological problems). Kwa mfano kama tatizo chama fulani basi ijulikane ni kitu gani hasa wanafanya hao chama A au B kinasababisha hili tatizo, ukikiondoa kile chama bila kujua tatizo lao halisi ni nini kunauwezekano wa kuja chama kingine kikafanya makosa yaleyale lakini ukijua kipi hasa basi chama kingine kikija na huku kinaijua sababu ya kufeli wenzao hawatarudia kosa na hawatabahatisha huenda hiki ndio tatizo kumbe sio.Tangu tumeanza kuzalisha hizo bidhaa, zina mchango gani kwa Tanzania katika soko la kimataifa?