WhatsApp imeanza kuweka mfumo wa Channels

WhatsApp imeanza kuweka mfumo wa Channels

Sasa nilikua naipenda kwakua ilinilia bando kiduchu sasa wakileta hayo mafeatures itakuawaje??

Status tu zinamaliza gb nzima, nimekimbia twitter, nimekimbia insta wananifata mpaka whatsapp.
 
Hakuna cha marketing strategy hapo, kuingiza hizo features ni swala la kiutaalam zaidi so inategemea una watu gani ktk kitengo, pia SERA za kampuni/Mtandao zinasemaje? Ndio maana Google kila siku wanabadiri sera za matumizi ya Huduma zao hasa upande wa Youtube au huwa husomi?
Mmh ko Telegram ndo wanajua intergration zaid au sio. Pooor.

Uweke kila kitu kwa wakti mmoja what nrw utakachokuwa nacho uko mbele.

Mfano unaona wanachokifanya Apple na Matoleo yao ya simu. What if wakeweka kila kitu kwenye tole la kwanza
 
Hakuna cha marketing strategy hapo, kuingiza hizo features ni swala la kiutaalam zaidi so inategemea una watu gani ktk kitengo, pia SERA za kampuni/Mtandao zinasemaje? Ndio maana Google kila siku wanabadiri sera za matumizi ya Huduma zao hasa upande wa Youtube au huwa husomi?
Wamarekani wanawapiku wengine kwenye Techolojia sio kwamba wanajua sana ila kwenye namna ya kujimarket tu na kujibrand.

Mfano izo feuture unazosema eti ni mgumu kuzifanya jiulize kwann izo wssap ambazo sio official kama FM wasap na Gb walikuwa wanatoa matoleo ambayo huenda yanavuja wao wanakuwa wako Mbele ndo maana wasap wanaziban izo GB wasap maana wale ni kama wanaiba zile feuture ambazo bado wasap hawajazirelease ko wao unakuta wako mbele. Mfano Kuhide Chat, GB wasap tayar walikuwa nayo saiv ndo official wasap wanaiweka

Wasap wao wanaenda kwa matoleo ili wasap iendelee kubaki kwenye soko na iendelee kuwa Mpya kila kukicha

Ukitaka kujua ilo Jiulize kwann Telegram haivumi sana kama ilivo kwa wasap
 
Whatsapp inawafaa wenye akili ndogo, Telegram inawafaa wenye akili kubwa (Intelligence-based people) nina mwaka wa tano sasa whatsapp naisikia kwenye mabomba yao tu situmii upuuzi.
ID yako inasapoti upuuzi ulioongea.
 
Mmh ko Telegram ndo wanajua intergration zaid au sio. Pooor.

Uweke kila kitu kwa wakti mmoja what nrw utakachokuwa nacho uko mbele.

Mfano unaona wanachokifanya Apple na Matoleo yao ya simu. What if wakeweka kila kitu kwenye tole la kwanza
Unataka kusema telegram haipo developed since kuwekwa hizo features hapo mwanzo?

Kwanza unapaswa ujue recently Telegram kaingiza feature ya Groups ndani ya Group. Sijui kama umeliona hili? Kama ww ni mtu wa kuangalia makalio huko TG huwez nielewa naongelea nini.

Telegram ni low key mno ndio maana huwez kuta Ads za wao kujitangaza wala huwezi kuta wameingia ktk mizozo ya kibiashara.
 
wanaziban izo GB wasap maana wale ni kama wanaiba zile feuture ambazo bado wasap hawajazirelease ko wao unakuta wako mbele. Mfano Kuhide Chat, GB wasap tayar walikuwa nayo saiv ndo official wasap wanaiweka

Kwa uandishi huu wa hii Paragraph sina haja ya kuendelea na huu Mjadala.

Ila wacha nikuelimishe.

Gb whatsapp na zingine mfnao FM whatsapp etc zote hizo kitaalam tunaita (Modded Apps)..

Niende kitaalam zaidi.

Database structure ya whatsapp ipo open kupokea mabadiriko ya kimfumo kulingana na nini kimesukwa ktk (Backend). hao wanao clone whatsapp na kuinject features nyingi zaidi ni manipulation ya syntax za Database kuu. Ndio maana nasisitiza whatsapp haipo end to end encrypted kama inavyojinasibu.

Mwanzo nilikuuliza kama unasoma Policy and guidelines za huduma unazopewa hasa za Google au hao Meta (Whatsapp)? Hukunijibu inaonesha kichwani ni mweupe ktk haya mambo unakaa unashikilia bango la Marketing strategy.

Wao wanasera zao za uendeshaji wa huduma, pia kaa ukijua Telegram ni open source hivyo ni rahisi sana kuendelea kitech kuliko hiyo whatsapp.

Telegram ipo mbele miaka 10 kitech kulinganisha na Whatsapp si kwa security si kwa muonekano si kwa Storage.

Mwisho.

Endelea kushikilia Bango la Marketing strategy etc wakati hutaki kusoma ni vipi huduma za whatsapp zinatakiwa zitolewe kwa kuzingatia nini na kwa nani. Soma Policy documents and user agreements alafu urudi.
 
Kwa uandishi huu wa hii Paragraph sina haja ya kuendelea na huu Mjadala.

Ila wacha nikuelimishe.

Gb whatsapp na zingine mfnao FM whatsapp etc zote hizo kitaalam tunaita (Modded Apps)..

Niende kitaalam zaidi.

Database structure ya whatsapp ipo open kupokea mabadiriko ya kimfumo kukingana na nini kimesukwa ktk (Backend). hao wanao clone whatsapp na kuinject features nyingi zaidi ni manipulation ya syntax za Database kuu. Ndio maana nasisitiza whatsapp haipo end to end encrypted kama inavyojinasibu.

Mwanzo nilikuuliza kama unasoma Policy and guidelines za huduma unazopewa hasa za Google au hao Meta (Whatsapp)? Hukunijibu inaonesha kichwani ni mweupe ktk haya mambo unakaa unashikilia bango la Marketing strategy.

Wao wanasera zao za uendeshaji wa huduma, pia kaa ukijua Telegram ni open source hivyo ni rahisi sana kuendelea kitech kuliko hiyo whatsapp.

Telegram ipo mbele miaka 10 kitech kulinganisha na Whatsapp si kwa security si kwa muonekano si kwa Storage.

Mwisho.

Endelea kushikilia Bango la Marketing strategy etc wakati hutaki kusoma ni vipi huduma za whatsapp zinatakiwa zitolewe kwa kuzingatia nini na kwa nani. Soma Policy documents and user agreements alafu urudi.
Mm ni mweupe sijui Tech na sipo Kubishana Mkuu maana Matech wa Bongo kwa Kubishana na kujikutana mnaijua mifumo hamjambo Mtafikkr mshawai develop ata Mfumo mmoja wa maana.


Ila Nashukuru kwa elimu yako Mimi Natamani tu Telegram iwe na watumiaji wengi bongo kama ilivo kwa wasap maana Nina Channel yangu kule ina Subscribers Elfu 20 walijoin kipind Fulani ivi nilikuwa natoa huduma fulan nikawa nawaforce watu wajiunge kwenye Channel yangu ili kuipata iyo huduma ko nikavuna Subscriber elfu 20 ila sasa saivi walioko online ni wachache tofaut na ilivo kwa Makundi yangu ya Wasap.

Ko licha ya Telegram kuwa na future nzur lkn bado bongo imeshia kuwa chaka la watafuta porno na movies tu
 
Mm ni mweupe sijui Tech na sipo Kubishana Mkuu maana Matech wa Bongo kwa Kubishana na kujikutana mnaijua mifumo hamjambo Mtafikkr mshawai develop ata Mfumo mmoja wa maana.


Ila Nashukuru kwa elimu yako Mimi Natamani tu Telegram iwe na watumiaji wengi bongo kama ilivo kwa wasap maana Nina Channel yangu kule ina Subscribers Elfu 20 walijoin kipind Fulani ivi nilikuwa natoa huduma fulan nikawa nawaforce watu wajiunge kwenye Channel yangu ili kuipata iyo huduma ko nikavuna Subscriber elfu 20 ila sasa saivi walioko online ni wachache tofaut na ilivo kwa Makundi yangu ya Wasap.

Ko licha ya Telegram kuwa na future nzur lkn bado bongo imeshia kuwa chaka la watafuta porno na movies tu
Iuze hiyo Channel, alafu ununue nyingine yenye active users.

Kumbe unajua Wabongo wanataka nini? Wawekee hizo Porn na Movies. Hicho ndio wanapenda au ww unawawekea mistari ya biblia? Ukishausoma mchezo watu fulani wanataka nini basi wape wanachotaka.
 
Wale chawa wa "yunaitedi steti ofu amerika" wanaiongelea telegram kwa makasiriko sana sababu tu ilianzisha na warusi.
20230613_090304.jpg
 
Iuze hiyo Channel, alafu ununue nyingine yenye active users.

Kumbe unajua Wabongo wanataka nini? Wawekee hizo Porn na Movies. Hicho ndio wanapenda au ww unawawekea mistari ya biblia? Ukishausoma mchezo watu fulani wanataka nini basi wape wanachotaka.
Mm kwenye porno siwez wala Biashara ya movies siwez ila nachokijua Channel za Wasap zitakuja kuwa active kuliko izo za Telegram

Nimewekeza majeshi uku saiv Makundi Wasap yanabeba watu wengi Telegram inaendelea kukosa soko View attachment 2655705
 
Via Telegram unaweza fanya direct monetary transactions kwa kupita modded bots zilizokuwa developed through various API's

Via Telegram unaweza kutunza files za ukubwa mbalimbali kwa muda mrefu hili huwez fanya kwa whatsapp wala social media yoyote. 10gb +

Hauna haja ya kudownload media, media zipo live 24/7 kutokana na server zao kuwa kubwa Unawez access kila kitu in a matter of seconds.

Kupita Bots unaweza trade chap through Telegram..

Kupitia Telegram kila kitu unachotaka unapata (Like a Darkweb thing) kuna jinsi ya kudeal na BOTS wakuletee unachotaka.


Kupitia Telegram unaweza cheza games.. unaweza tengeneza Chat Bot lako na kuendesha mijadala.

Unaweza kuwa na Multiple accounts bila hata kuwa na number..

Aisee ni mambo mengi ila somo linatakiwa libase ktk matumizi ya BOTS ambayo kwa Whatsapp walifeli.. bot pekee lilikuwa la Michezo na limefeli
Mkuu hapo kwenye dark web hebu kazia basi.
 
Kwa nini telegram ni underdog kwenye social media mbali na hayo uliyoyataja , ?? Najua jibu unalo , ulimwengu wa sasa unahtaji vtu simple , hayo mambo ya BOTS too complicated Kwa watu wenye mambo mengi, kitu kilichovutia watu na kuifanya iwe popular ni ule uwezo wa kuhold watu wengi per once , ndo maana umekuwa mtandao maarufu Kwa maswala ya group za malaya n.k .....!! Yes leta feature mpya but iwe simple and friendly , Tiktok sio wajinga ,
Nakuapia ndani ya miaka mitatu ijayo Telegram ataiuza Kwa META ,
Kama Meta atainunua telegram maana yake telegram ni bora kuliko whatsap yake.Jambo lingine unatakiwa ujue watumiaji wa tekegram wako dunia nzima.sasa huo wingi wewe umeupimaje ili kujua whatsap ina watumiaji wengi zaidi.Labda kama unazungumzia tanzania tu.
 
Unaweza kuedit msg whatsapp toka huko vichochoroni ulipo updates zitakufikia. 5B WhatsApp, 1B Telegram downloads. Numbers speak for themselves. Kama watanzania wanafika 5B haya.

View attachment 2651531
Hapo kuna marehem wakutosha.Kwa umri wa whatsap toka imeanzishwa kufikisha hao watu waliodownlod inawezekana.ila kwenye matumiz worldwide telegram inakuja kwa kasi na ni mdogo sana kwa whatsap.
 
Mm kwenye porno siwez wala Biashara ya movies siwez ila nachokijua Channel za Wasap zitakuja kuwa active kuliko izo za Telegram

Nimewekeza majeshi uku saiv Makundi Wasap yanabeba watu wengi Telegram inaendelea kukosa soko View attachment 2655705
Yako active kwasababu mengi ni magroup ya harusi,familia na maeneo ya kazi.Ila telegram unaweza kujiunga magroup ya watu wengi toka nchi mbali mbali ambao hamjuani na maisha yakaenda.Whatsap anafaida ya ukongwe ila sio ubora.
 
Namna ambavyo watumiaji wa WhatsApp wanaitumi app ya WhatsApp; itabadilika na soon WhatsApp itakuwa ni mtandao wa tofauti zaidi. Itakuwa ni sehemu ambayo sio lazima ukimaliza kuchat na rafiki yako kwenye WhatsApp, unafunga app ya WhatsApp na kufungua app ya Instagram ili kufahamu habari zinazoendelea mjini. Itakuwa unaweza kupata taarifa zote kupitia app ya Instagram bila kulazimika kwenda kwenye apps nyingine.

Kampuni ya Meta imekuwa ikifanya majaribio ya kuweka mfumo wa Channels. Mfumo huu utawezesha makampuni, content creators, wataalam na brands mbalimbali kutengeneza Channels ambazo zitakuwa zinatoa updates na taarifa mbalimbali ndani ya mtandao wa WhatsApp.

View attachment 2650207

Mambo ambayo yatakwepo katika Channels za WhatsApp​

  • WhatsApp itakuwa na channels za news, team za mpira, vyombo vya habari, content creators, wasanii, brands mbalimbali, channels za kiserikali na aina mbalimbali ya channels ambazo zitakuwa zinatoa updates kwa watumiaji.
  • Channels zitakuwa na button ya “Follow
  • Ukitaka kujitoa kwenye Channel, itakwepo option ya “Leave
  • Channels zitakwepo kwenye tab mpya ya “Updates” ambayo itakwepo kwenye tab ya Status.
  • Message za kwenye Channels zitakuwa zinafutika baada ya Siku 30
  • Admins watakuwa na uhuru wa kuzuia Screenshot zisifanye kazi kwenye Channels.
  • Hautaweza kuona orodha ya watu ambao wame-follow channel.
  • Hautaweza kuona namba za admins wa Channel
  • Admin atakuwa na uhuru Channel iwe huru kwa kila mtu kujiunga au kuzuia isipatikane kwa watumiaji wote.
  • Message za Channels sio encrypted hivyo WhatsApp inaweza kuziona. WhatsApp imesema inafanyia kazi mfumo wa encryption ambao utasaidia kuboresha usalama wa chats
  • Status na Channels zitakaa pamoja na zitakwepo kwenye tab ambayo itaitwa “Updates”. Utaweza kuona Status za marafiki na kuangalia updates za Channels ambazo umejiunga nazo kwa pamoja. Tab ya Updates itakuwa na Channels na WhatsApp Status kwa pamoja.
  • Meta imetangaza mfumo wa Channels utaanza rasmi kwa watumiaji wa WhatsApp na utaanza kwa watumiaji wa nchi za Colombia na Singapore.
  • Itakuwa ni njia rahisi ya kutuma habari, na taarifa mbalimbali kwenye WhatsApp. Watumiaji hawatalazimika kutumia Instagram, Facebook au Twitter kufahamu nini ambacho kinaendelea.
  • Itakuwa njia salama kwa sababu hauwezi kuona namba za admin na watu ambao wamejiunga kwenye channel.
  • Channels zitarahisisha kwa wafanyabiashara kutangaza bidhaa zao na biashara.


Mabadiliko haya yataleta utaratibu mpya wa kufuatilia habari, na taarifa mbalimbali moja kwa moja ndani ya WhatsApp; badala ya kwenda Twitter, Instagram na Facebook ili kupata taarifa mbalimbali kama vile habari. Itaathiri soko la Telegram, ambayo inafanya vizuri kwa kuwa na Channels nyingi na kuanzisha mfumo wa Channels kabla ya app nyingine hazijaanza kuwa na Channels.

View attachment 2650211View attachment 2650212
View attachment 2650213View attachment 2650214

Mwamba wee ni nomaa
 
Back
Top Bottom