Whatsssssss!!!!!!!!!????

Nimempigia simu demu wangu akapokea bwana ake mwingine na kuanza kunihoji:- "wewe ni nani wampigia mpenzi wangu simu???
Nikamjibu:- "Sorry mimi ni Doctor, mpenzi wako alinambiaga niwe namkumbusha kumeza dozi zake za ARV kila muda ukifika"
Yule mwanaume leo tumemzika...!!
Sipendagi ujinga mimi[emoji13] [emoji13]
 
Vibaka wako hivyo, hata akiwa amelazwa na ametundikiwa dripu, hutamani nesi aondoke haraka ili aibe dripu sliyotundikiwa!!
 
Mambo ya Benki...!!
Teller: Hii pesa ni fake.
Mkaka: Shida iko wapi..pesa ni yangu..account pia ni yangu... weka tu!!!
Sipendi mtu kucheza na akili yangu[emoji23]
 
Alex : I love you.
Carol: Lol
Alex : I Need You in my Life.
Carol: Lol
Alex : You're my everything.
Carol: Lol
Alex : iPhone 6 or iPhone 7.
Carol: iPhone 7
Alex : Loooooooooooooool.
Carol: Do you wanna buy it for me?.
Alex : Loooooooooooooool
.
Carol: talk to me.
Alex :Loooooooooooooool
Sipendagi ujinga mimi.!![emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Et jana usiku mwizi kavunja mlango kwangu akaanza kutafuta kitu kila kona ikabidi na mie niamke, namuuliza unatafuta nini??
Ananijibu "Hela...!"
Ndipo nilipoanza na mie kutafuta nae maana hata hela ya kula Jana sikua nayo.
Alichoka zaid nilipomuliza una uhakika uliweka humu?
Sipendagi utani na kitu hela![emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mdada alienda super-market kununua
kuku, bahati mbaya kwenye friji
kulikuwa na kuku mmoja tu.
Muuzaji akamtoa akamuweka kwenye
mzani, akaonekana ana kilo moja na robo.
Mdada akamuuliza muuzaji, ’Huna mkubwa zaidi?’
Muuzaji akamchukua yule kuku na
kujifanya kamrudisha kwenye friji, halafu
akamtoa tena kwenye friji na kumrudisha kwenye mzani, safari hii akagandamiza mzani kwa gumba, kuku akaonekana ana kilo mbili.
Mdada akasema "Duh afadhali huyu
mkubwa kidogo, naomba unifungie
nawachukua wote wawili"[emoji13] [emoji13]
 
Askari wameitwa kwenye nyumba ambayo kuna ugomvi. Wakafika halafu ikabidi waripoti kwa simu yale waliyokuta.
Askari: Mkuu tumekuja hapa tumekuta mama mwenye nyumba amempiga mumewe chuma cha kichwa na kumuumiza sana.
Afande: Kisa na mkasa hata akafanya hivyo?.
Askari: Mama alikua anapiga deki, mumewe akaingia na viatu kabla sakafu haijakauka.
Afande: Mmeshamkamata huyo mama??
Askari: Hapana bado mkuu
Afande: Mnangoja nini sasa??
Askari: Tunangoja sakafu ikauke afande[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kauali 10 MBAYA za Walimu darasani, unakumbuka ipi hapa??
1. Mkimaliza kuongea niambieni niendelee kufundisha.
2. Baba yako kauza Ng’ombe ili alete Ng’ombe mwingine Shule.
3. Kama unajua kuliko mimi njoo ufundishe wewe.
4. Ulikuja peke yako na utaondoka peke yako.
5. Hata msiponisikiliza mshahara wangu upo palepale.
6. Baba yako anahangaika kulipa Ada wew unafanya Utumbo tu.
7. Hata nikeshe nafundisha wengine ni mizigo hawatoki na lolote.
8. Tunavisaidia tu kwani vikifanikiwa mbeleni hata salamu vinatoa?[emoji13]
9. Bichwa kibwa Ubongo Nukta[emoji23] [emoji23] .
10. Wengine hapa wamekuja kukua tu[emoji12]
 
Watu kweli wamezoea vya kuchinja2!!!
WABONGO SINA HAMU NAO...!!
Jamaa alinunua friji jipya, akawaza namna ya kuondokana na lile la zamani, basi akaliweka nje ya nyumba yake na kuandika kibao:-
"ANAYE TAKA KUCHUKUA, ACHUKUE BURE".
Watu wakawa wanapita wanafungua lakini kila mtu akawa anaogopa kuchukua maana hakuna aliyeamini mtu anaweza akagawa friji zima bure.
Baada ya kuona wiki imepita halijachukuliwa, akaandika:-
"FRIJI INAUZWA LAKI 3"
Usiku uleule likaibiwa[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mkuu Supermarket. Asante sana kwa vichekesho hivi. Nime-subscribe kabisa kwenye hii thread na kila nikija sikosi kucheka. Kama unatunga mwenyewe vichekesho hivi basi una kipaji kizuri katika komedia. Mungu Akubariki!
 
Mkuu Supermarket. Asante sana kwa vichekesho hivi. Nime-subscribe kabisa kwenye hii thread na kila nikija sikosi kucheka. Kama unatunga mwenyewe vichekesho hivi basi una kipaji kizuri katika komedia. Mungu Akubariki!
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
WATANZANIA NA MAAMUZI MAGUMU.
1. Huna uhakika wa kula na elfu moja pekee uliyonayo unaamua kuinywa Kiroba - Ni maamuzi magumu.
2. Huna kitanda na unaamua kuoa - Hayo pia ni maamuzi magumu.
3. Huna uwezo wa kumlisha mkeo na unampa ujauzito - Ni maamuzi magumu.
4. Shule haina waalimu unampeleka mwanao - Pia ni maamuzi magumu.
5. Daladala imejaa mpaka mlangoni na unaamua kupanda - Ni maamuzi magumu.
6. Unalipwa laki mbili unamhonga binti laki moja - Hayo ni maamuzi magumu[emoji12]
 
MAJINA KUMI MAGUMU NA YAAJABU TANZANIA...!!
1. Ndugu TAMPERA NGUNAMABWOKO-Mhitimu wa kidato cha sita shule ya sekondari ya wavulana Tabora mwaka 1992.
2. Ndugu GOGOMOKA MISALABA-Mhitimu wa kidato cha sita shule ya sekondari Minaki mwaka 1998.
3. Ndugu ABDALLAH NYUNDO KICHECHE-Mwanafunzi wa kidato cha kwanza shule ya sekondari Minaki mwaka 2002.
4. Ndugu MASANINGA SUMAKU POMBOJOLOWE a.k.a PUMBU-Dereva wa mabasi ya Hood.
5. Koplo RUBYENEKO MUGANYIZI BYOMBARIRWA-Mpi
shi mkuu wa kikosi cha 34 cha Jeshi (34 KJ), Mbeya.
6. Ndugu TAKOTAKO WA PUMBUJE a.k.a AKANANA-Muuza miwa na maji baridi maarufu pale magomeni makutano ya barabara za Rashid Kawawa na Morogoro.
7. Mheshimiwa NJENGAFIBILI MWAIKUNGILE-Jaji wa mahakama kuu ya Tanzania.
9.Ndugu TUNTUFYE MWAIKIMBA a.k.a KIMBA-Fundi majiko maarufu Railway Gerezani Dar es Salaam.
10. Ndugu BENADETTA TYETYETYE-Mhitimu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, mwaka 2001 fani ya sayansi ya jamii (BA)
-KUNA MAJINA MENGINE UNAYAJUA!??[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mvuta Bangi alikwenda kwa Dokta na kumwambia:-
Mvuta Bangi: Mala nyingi huwa nazungumza na watu, lakini cha kushangaza watu hao huwa siwaoni, utanisaidiaje daktari?.
Daktari:- Ni wakati gani huwa inakujia hali kama hiyo?.
Mvuta Bangi:- Mala nyingi pale ninapoongea nao kwa Simu...!!!
Daktari:- Mmm...!![emoji12]
 
WAMBIE WALIMU WAACHE UTANI HATA KAMA MISHAHARA MIDOGO!!
Ona huu mtihan wa terminal:-
1. Rais wa Sasa wa Tanzania ni Kikwe__
a)ta (b)te (c)ti (d)to (e)tu
2. Aliyefanya Tanganyka iwe huru ni Nyere__
a)ra (b)re (c)ri (d)ro (e)ru.
3. Mlima mref kuliko yot Afrika ni Kilima___ro
a)nja (b) nje (c)nji (d)njo (e)nju.
4. Tanzania imepakana na bahari ya hi___
a)nda (b)nde (c)ndi (d)ndo (e)ndu.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Driver:- Kijana naomba unijazie tank yangu.
Petrol attendant:- I only speak English sir, could you please say that in English?...
Driver:- Oh! Ok Good morning,
I currently feel a profound desire to replenish the propellant of my motorized automobile,
therefore I cordially request that you transfer from your subterranean reservoir a sufficient quantity of the combustible fluid of the highest octane rating to fill the appropriate receptacle of the said means of perambullation to the brim.
Petrol attendant:- Mheshimiwa hutaniwi?
Mimi naongea kiswahili tuu!!.[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…