Mkuu Chonya Wa Chilonwa kama nlivyotangulia hapo juu kusema, hongera sana kwa kuwa na malengo ya kusoma engineering!!! na hongera pia kwa kutumia muda wako kufanya research kuhusu fields mbali mbali za engineering!!! sijapata hakika sana kama umepanga kusomea huko huko france au utakuja bongo kusoma, whatever the case...haya ni mawazo yangu...
kama nilivyoahidi....
1)Civil engineering
Kwa hapa nyumbani (tanzania) hii kiasi flani ina upana sana katika kujiajiri na kuajiriwa. Ukianzia katika sekta za serikali na binafsi, mashirika mbali mbali ya research yanahitaji hawa watu!! most likely ukisomea hii kozi uta specialize katika moja hizi fields structural,transport engineering na baadhi ya vyuo wameongeza irrigation na water resources!! changamoto kubwa ya hii field ni tenda nyingi kupewa watu wa nje(wachina na wengineo), kuwepo kwa wataalam feki na kutokuwepo kwa capital hasa mainjinia wazawa!! mkuu simaanishi kwamba huwezi ajiriwa au kujiajiri, uwanja upo mkubwa sana!! japo umesema hujai feel ila unaweza ukaifikiria tena hii field...
2) Mechanical engineering
Kwa maoni yangu hii inafwatia kwa ubora hapa kwetu!! kama utasomea hii kozi unaweza specialize kwenye energy production, au general... popote ambapo civil engineer yupo huyu lazima awepo!! kazi zao ni katika ujenzi, migodini bila kusahau secta za binafsi na serikali!! uzalishaji wa mashine mbali mbali na kudesign mara nyingi ndio kazi zao!!
3) Electrical and electonics engineering au electrical engineering.
Sasa hii ntamwomba
Maganga Mkweli ,
Sinziga
King'asti Horseshoe Arch Consultant na wengine waje watie neno hapa!! japo wengi wanasema iko so limited nikimaanisha wao waafanya kazi tanesco tu, hii sio kweli!! hakuna project ambayo inaanzishwa bila hawa watu kuwepo!! migodini, ujezi wa nyumba, bara bara, uzaishaji umeme and so forth kote huko wanapatikana!! na kama ukisomea hii most likely unaweza specialize kwenye power generation, micro computer, au general electrical!! kwa hapa tanzania bado sana inalipa na ina future nzuri kama utafaulu na kuipenda!! katika hii kozi kama nlivyosema unaweza pia kusomea mambo ya computer kama ukiambua kuspecilize huko..inawezekana!!
4)Petrolium engineering
Hakuna ubishi kwamba gesi imevumbuliwa hapa nyumbani, na kwa msisitizo hii kozi imeanza fundishwa kwenye vyuo kama UDSM(imeanza mwaka huu) na UDOM!! ni kozi nzuri na future yake ni nzuri, ila kama unataka kujiajiri nadhani haitakua rahisi kiasi flani na mara kwa mara unaweza ajiriwa na serikali!! changamoto nyingine ni kwamba, katika field hii ya gesi hasa hapa bongo makampuni mengi yenye tenda ni ya nje na mara nyingi wanakuja na wataalamu wao(simaanishi wataalam wa ndani hawaajiriwi), sasa hapa mbongo kupata kazi kiasi flani inaweza kua ngumu!!
5)Agriculture engineering
Kwa hapa nyumbani hii kozi inatolewa chuo kimoja tu, nchi sasa imeweka mkazo sana kwenye mambo ya kilimo, na kama unavyoona watu hawa kiasi fulani wapo wachache sana, kama unataka kujiajiri ni rahisi sana na kama kuajiriwa pia haisumbui!! makampuni ya uzalishaji hasa kilimo wanahitaji sana hawa watu, kwenye viwanda nako hawa watu fiti..
6)Chemical engineering
Mara nyingi hawa watu wanabase sana kwenye viwanda na uzalishaji(processing) kwa ujumla. na kwa hapa tanzania inatolewa na vyuo kama viwili kama sikosei(UDSM na SUA), bado hawa watu wanahitajika sana na ni choice nzuri. Kwa mtazamo wangu hawa watu ni ngumu kidogo kujiajiri(simaanishi haiwezekani kijiajiri), labda kama unauwezo ukaanzisha kiwanda chako...
7) Computer engineering, Software engineering
Kuliko ukasomee computer science(kama unataka kusomea engineering) ni bora ukasomea moja ya hizo mbili. kwa hapa bongo inakaugumu flai kupata kazi katika serikali ila ni rahisi sana kujiajiri hasa kama consultant engineer. tukianza na compurer engineering wana deal sana na hardware na kiasi flani computer science imemezwa na hii, na kwa baadh ya vyuo ukifika mwaka wa tatu unaweza ukaspecilize katika software engineering!! software engineering, on the other hand, kwa hapa tz inatolea na UDOM pekee, bado sana watu wake wanahitajika sana katika sekta binafsi na serikali!!
8)Irrigation engineering
Kwa hapa kwetu inatolewa na vyuo vitatu tu (SUA na arusha tech,instutute of water dar), hii kozi ni subset ya civil engineering na kwa baadhi ya vyuo wanaijumisha na water resources engineering!! hamna mtu ambaye hajui mabadiliko ya hali ya hewa duniani!! wataalamu wa umwagiliaji wanahitajika sana duniani hasa na makampuni binafsi, bila kusahau kama unataka kuajiriwa na serikali ni rahisi mno na nirahisi kujiari!!
9)Architecture
Japo inaonekana kama sio field ya engineering, ila believe me hamana project inafanywa bila uwepo wa architect na yeye mara nyingi ndiye anadesign let say nyumba then anamkabidhi structural engineer, wataalamu wake wapo wachache hilo halina ubishi, kama unajiamini ni mbunifu(and ofcoz to be an engineer you must be creative) hii field nzuri sana hasa kwa hapa bongo!! ni rahisi sana kujiajiri na inasemekana hata ukiwa mwanafunzi hasa mwaka wa nne na tano unaweza ukawa unapiga pesa mtaani kama uko smart enough!!!
USHAURI
Hamna kitu kizuri kama kufanya kazi au kitu unachopenda toka moyoni mwako bila kulazimishwa na mtu!! kwa field yoyote utayoenda hakikisha unaenda sio kwa sababu inalipa ua utapata tittle mtaani ila kwa sababu unaipenda toka moyoni!! kumbuka changamoto zipo anzia shuleni(sup) mpaka makazini...ila kama umeenda kwasababu unaipenda kamwe hutatishwa na changamoto hizo!!! Kumbuka hamna kitu kizuri kama kutimiza ndoto zako maishani!! Ukifanikiwa maliza usisahau kujisajili kama proffesional engineer ili utambulike ndani na nje....na kama unaswali usisite kuuliza..
Karibu sana uhandisini mkuu, na kila heri...