Whistleblower: Kashfa nzito suala la sukari, wamo vigogo wazito

Whistleblower: Kashfa nzito suala la sukari, wamo vigogo wazito

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
BARUA KWA RAIS SAMIA SULUHU KUHUSU UFISADI KWENYE SUKARI

11 December 2021


Mheshimiwa Rais nakusalimu kwa Jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini ningependa badala ya kusema kazi Iendelee basi uitikie haki, ustawi wa watu na uhuru wa kweli.

Mheshimiwa Rais nina mengi ya kukueleza kuhusu nchi yetu lakini leo ningependa kukueleza moja ambalo ni maombi yangu kwamba utalifanyia kazi ili kuitoa nchi yetu katika uchafu huu mkubwa. Jambo hili ni ulanguzi katika bei ya sukari na ufisadi mkubwa uliopo katika eneo la bidhaa muhimu (nipatapo wasaa nitakuandikia barua zaidi kuhusu bidhaa nyingine kama mafuta ya kula). Nakiri kwamba bei ya bidhaa hizi inachangiwa na mwenendo wa bei ya soko la dunia lakini pia inachangiwa na ufisadi uliopo katika soko la ndani.

Kwenye sukari tuna kundi dogo la wazalishaji nchini na hawa wana kikundi chao ambacho kisheria si sahihi (cartel). Kikundi hiki kiko chini ya Seif Ally Seif ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Superdoll (wamiliki wa Mtibwa na Kagera Sugar). Bei za sukari zinaweza kupandishwa kwa namna mbili, kwanza kwa kuamua kiasi gani cha sukari viwanda vya ndani vizalishe, maana yake hapa unaamua kiasi gani cha sukari kiwe kwenye maghala.

Ukishaamua kiasi basi bei itapanda kuendana na kiasi. Maana yake ukiamua sukari uzalishe kidogo basi bei itapaa sababu bidhaa inakuwa chache na wahitaji ni wengi. Namna ya pili ni kushirikiana na watendaji walio serikalini kuhakikisha kwamba unapobana uzalishaji soko la ndani ili kuwe na uhaba na bei iwe juu basi serikali haitoi vibali kwa watu kuingiza sukari nchini sababu kwa kufanya hivyo uhaba hautakuwepo na bei unayotaka wewe itavurugika. Huo ndio mchezo unaochezwa Tanzania.

Ilikuwaje?

Endelea kusoma HAPA
 
Halafu wanatuletea stori za legacy sijui hero! Kumbe mtesi wa wananchi! Kama ni kweli na alaaniwe! CCM imefika mahali kila adhaniwaye ni msafi kumbe ananuka kuliko mwenzie! Chama kimefika hatua kinatumia vyombo vya dola (bunge, jeshi, mahakama, ofisi za serikali - DPP, DCI, Polisi, etc.) kujihalalishia uchafu wao; ni hatari sana.
 
Ni jambo jema!

Nasubiri andiko lako kuhusu Mbowe.

Hayo ya ufisadi nawaachia akina Muhuni na Kiroboto!
Mada zingine weka upumbavu wako mfukoni mwako, hii mada it got nothing to do with politics, ni issue inayoongolea kuhusu watanzania wote regardless itikadi zao, well done my whistleblower maana mpo wachache sana, kama ni kweli uliyoyaandika hapa Imani yako itakujibu, umenikimbusha uandishi wa gazeti la Rai (sio la sasa) na gazeti la mfanyakazi; shame on us kwa kuyafanya maisha ya mtanzania wa kawaida kuwa hovyo kabisa.
 
Mada zingine weka upumbavu wako mfukoni mwako,hii mada it got nothing to do with politics ,ni issue inayoongolea kuhusu watanzania wote regardless itikadi zao,welldone my whistleblower maana mpo wachache sana,kama ni kweli uliyoyaandika hapa Imani yako itakujibu,umenikimbusha uandishi wa gazeti la Rai(sio la sasa)na gazeti la mfanyakazi;shame on us kwa kuyafanya maisha ya mtanzania wa kawaida kuwa hovyo kabisa.
Manka umeshavurugika!
 
Halafu wanatuletea stori za legacy sijui hero! Kumbe mtesi wa wananchi! Kama ni kweli na alaaniwe! CCM imefika mahali kila adhaniwaye ni msafi kumbe ananuka kuliko mwenzie! Chama kimefika hatua kinatumia vyombo vya dola (bunge, jeshi, mahakama, ofisi za serikali - DPP, DCI, Polisi, etc.) kujihalalishia uchafu wao; ni hatari sana.
Mwambie huyo mchambuzi alete ushahidi wa maelezo yake. Mbona Hutaki Unaacha alikuwa anatupa hata na account namba za benki pesa zilipopita, siku hata saa na nani alipokea hizo fedha!? Watu watoe tuhuma kwa ushahidi usiotiliwa shaka. Vinginevyo, huku ni kuchafuana kwa maslahi binafsi.
 
... halafu wanatuletea stori za legacy sijui hero! Kumbe mtesi wa wananchi! Kama ni kweli na alaaniwe! CCM imefika mahali kila adhaniwaye ni msafi kumbe ananuka kuliko mwenzie! Chama kimefika hatua kinatumia vyombo vya dola (bunge, jeshi, mahakama, ofisi za serikali - DPP, DCI, Polisi, etc.) kujihalalishia uchafu wao; ni hatari sana.
Hujamuelewa mleta uzi. Ni kuwa yeye mleta uzi katumwa na genge la wezi na mafisadi. Prof. Mkenda alifafanua vizuri sana. Nyie mafisadi hamuwezi kutudanganya hata iweje. Dkt Magufuli alikuwa mzalendo alifanya vitu vyenye tija na faida kwa taifa.

Acheni uhuni wa kutunga. Maana unaposema eti wanaamua wazalishe kiasi gani wakati waziri aliwahi kusema na inajulikana capacity ya viwanda vyetu ni ndogo. Halafu mnavyotaka vibali vitolewe ili mlete na sukari oliyo isha muda ili watanzania wafe? Kipindi cha JK watu walikula bidhaa za ovyo ovyo cheki watu wanavyokufa na cancer. Kwa ufupi huo mlango wa ufisadi hautafunguliwa!
 
Sijawahi wala sitakaa nimfikirie Majaliwa kama mtu mwema kwa hili Taifa na watu wake. Mungu anisamehe ila namuona Majaliwa kama mtu mwenye roho mbaya, mnafiki, mzandiki na mwenye tamaa. Hajawahi kuwa mkweli kwa Taifa.

Hata sasa namuona ndie masta mind wa anguko la Mama. Ana jionyesha kwake kama mtu mwema lakini hafai. Muda utaongea. Nani alijua yeye na Jenister ndio wako nyuma ya sakata la sukari? Bado ikija ya mafuta ya kula na mafuta ya gari utamkuta Majaliwa.

Tulimpigia Mama kelele aanze na safu yake akaona watu wana mfundisha kazi. Akabeba uchafu wa mwenda kuzimu. Sasa wazimu una mkuta. Amebaki kusema hato kubali wakati amesha kubali. Hata madudu yaliyopo bandarini ukifuatilia mkono wa Majaliwa upo. Makesi ya hovyo mahakamani Majaliwa yupo. Say all evils lazima yupo.
 
Back
Top Bottom