Who created God? Who made him? Where did he come from?

Who created God? Who made him? Where did he come from?

Siwezi kuhadaa ulimwengu kwamba najua majibu ya maswali haya.

Lakini hilo halina maana kwamba nikipewa jibu ambalo si la kweli na lenye mikingamo isiyoafikika, siwezi kulitambua hivyo.

Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hawezi kuwa na viwango vya upendo vilivyo chini ya upendo unaowezekana kibinadamu. Kwa hivyo, kama kweli ana uwezo wote na upendo wote, tungetegemea kuona ulimwengu wake ukiwa mzuri zaidi ya huu wa matetemeko ya ardhi yanayoua kqa mafungu, Ebola isiyotibika kqa watu masikini, mauaji, vita, njaa etc.

Kama mungu angekuwa binadamu mwenye uwezo wote huo anakaa Washington DC, New York, London, Dar au Dodoma, na ana uwezo wa kuzuia hayo yote, lakini hazuii tu, watu qangeandamana kumlaani, na hata kumshtaki mahakama ya The Hague kwa mauaji ya jumuiya.

Sasa inakuwaje huyu mungu mqenye uwezo mkubwa kulimo vyote kwa madai ya wengine, tumuwekee viwango vya chini kabisa vya uwajibikaji?

Huyu mungu yupo kweli au tunajisahaulisha tu kwamba kuna mambo hatuyajui na kila tusilolijua tunamsingizia mungu tusiyemjua?

Kama mungu mwenye uwezo wote na upendo wote yupo, kwa nini mabaya yapo duniani?

Ni kwa sababu sababu anaweza kuzuia ila hataki tu?

Kama ni.hivyo, je, ana upendo.wote kweli?

Au nin kwa sababu anataka kuzuia maovu lakini hawezi?

Kama ni hivyo, je anaweza yote?

Umetaja mabaya unayosema ni mabaya kwa kiwango chako cha kufikiri, hujataja mazuri ambayo Mungu amekuwa akufanya juu yako, uwepo wako duniani ni upendo tosha aliokufanyia Mungu na sidhani km unamlalamikia kuwa kwanini alikufanya uje duniani. Kiranga nilikwambia kwa uwezo wetu wa kufikiri sisi binadamu ni mdogo sn, nilikupa mfano kuwa sisimizi ajifanye kutaka kulingana uwezo wa kufikiri na ww binadamu, hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. Ukimfikiria Mungu in physical matter hutapata jibu, ila ukimfikiria Spiritually utafika mbali na utamuona Mungu
 
Sina chakukujibu coz tayari imani yako imeshashuka
Kwa kweli there is no way useme kwamba Mungu alikuwepo tu since forever.., yaani alitokea tangu milele yote.., its impossible. ngoja nikwambie kwanini.

1.) assuming Mungu ali-exist since forever, na tunaipa forever a value T. Sasa niambie at time (T-1 second) alikuwepo..??!

2.) Na at time (T-1 second) palikuwa na nani.., je ndie aliyefanya uumbaji..?! na je yeye huyo aliekuwepo at time (T-1 Second) kaumbwa na nani na katokea wapi na kwa sababu gani na kwa faida gani na ya nani..??! na ili iweje..??!

3.) Na tukisema Mungu atakuwepo up to forever, na tukaipa hiyo forever a value F, je at time (F + 1 second atakuwa wapi)..??!
 
Hata siku moja hututaweza ku describe kitu ambacho kiko unlimited na fahamu zetu ambazo ziko limited
 
Umetaja mabaya unayosema ni mabaya kwa kiwango chako cha kufikiri, hujataja mazuri ambayo Mungu amekuwa akufanya juu yako, uwepo wako duniani ni upendo tosha aliokufanyia Mungu na sidhani km unamlalamikia kuwa kwanini alikufanya uje duniani. Kiranga nilikwambia kwa uwezo wetu wa kufikiri sisi binadamu ni mdogo sn, nilikupa mfano kuwa sisimizi ajifanye kutaka kulingana uwezo wa kufikiri na ww binadamu, hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. Ukimfikiria Mungu in physical matter hutapata jibu, ila ukimfikiria Spiritually utafika mbali na utamuona Mungu

Hujajibu swali.

Ni kama nakuuliza "kwa nini mama aliyemzaa mwanawe kwa upendo wote aende kumchinjiia mbali wakati ana uwezo na upendo wote wote wa kutomchinja?".

Halafu unanijibu nisiangalie mabaya tu, niangalie kwamba mama kambeba mtoto tumboni na kumnyonyesha.

Swali langu hujalijibu.
 
Thinking beyond perception ni mbaya sana unaeza ukawa kichaa!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
wewe unajua au unaamini mungu hayupo ??

Kutokana na kila tunachokijua hadi sasa kuhusu dunia ama ulimwengu huu hakuna haja ya mungu!na kwa sababu hakuna ushahidi basi hayupo. Kama una ushahidi lete hapa
 
si kila swali lina jibu.

"mimi niko ambaye niko" yeye alikuwako, yuko na ataendelea kuwepo milele yote.

kaa uamini hivyo, ukiendelea kuchunguza utakuwa chizi.
 
Haiingii akilini kabisa. time is real and its here. anything real must adhere to reality such as time.., unless God isn't real.., is it..?!

Time ni mfumo wa kibinaadamu tu. Ukiiliza wazee wako kabla wazungu hawajaja kulikuwa hamna time. Huwezi kupata majibu uliyonayo kichwani kumhusu Mungu usipoweka swala la imani. UKITAKA KUPATA UWEPO WA MUNGU LAZIMA UWE NA IMANI KUMHUSU.
 
Kutokana na kila tunachokijua hadi sasa kuhusu dunia ama ulimwengu huu hakuna haja ya mungu!na kwa sababu hakuna ushahidi basi hayupo. Kama una ushahidi lete hapa

kwa nini hakuna haja ya uwepo wa mungu
haja yako ni nini ili ujue mungu yupo au hayupo ??
 
kwa nini hakuna haja ya uwepo wa mungu

Kwa sababu hakuna kinachohitaji mungu ama uwepo wa mungu ili kiwepo!
haja yako ni nini ili ujue mungu yupo au hayupo ??

Mungu ni idea na sio real figure ama spirit kama mnavoita.Ni idea tu ambayo ipo tu.
Haja yangu ni kwamba ilikuwaje mungu mwenye upendo wote na nguvu zote akashindwa kuepusha maovu katika dunia aliyoiumba na kuipenda kweli?.Kwa nini kama kwel yupo anashindwa kumwangamiza huyo mnaemwita shetani!?.Je shetani anafanya mambo yake kwa mamlaka ya nani?
 
Kwa sababu hakuna kinachohitaji mungu ama uwepo wa mungu ili kiwepo!


Mungu ni idea na sio real figure ama spirit kama mnavoita.Ni idea tu ambayo ipo tu.
Haja yangu ni kwamba ilikuwaje mungu mwenye upendo wote na nguvu zote akashindwa kuepusha maovu katika dunia aliyoiumba na kuipenda kweli?.Kwa nini kama kwel yupo anashindwa kumwangamiza huyo mnaemwita shetani!?.Je shetani anafanya mambo yake kwa mamlaka ya nani?

ulitaka kiwepo nini ili uamini mungu yupo au hayupo ?

Kila kinachotokea ni mipango ya mungu hivyo unavyotafsiri wewe kama maovu labda kwa mungu sio maovu??
Kama binadamu hatuna maana moja ya tafsiri itakuwa wewe na mungu ??
 
Kwa kweli there is no way useme kwamba Mungu alikuwepo tu since forever.., yaani alitokea tangu milele yote.., its impossible. ngoja nikwambie kwanini.

1.) assuming Mungu ali-exist since forever, na tunaipa forever a value T. Sasa niambie at time (T-1 second) alikuwepo..??!

2.) Na at time (T-1 second) palikuwa na nani.., je ndie aliyefanya uumbaji..?! na je yeye huyo aliekuwepo at time (T-1 Second) kaumbwa na nani na katokea wapi na kwa sababu gani na kwa faida gani na ya nani..??! na ili iweje..??!

3.) Na tukisema Mungu atakuwepo up to forever, na tukaipa hiyo forever a value F, je at time (F + 1 second atakuwa wapi)..??!

Je unaweza kuipa infinity (&#8734😉 value ? Naomba jibu la ∞-1.
 
Wakuu mara nyingi nimekuwa nikijiuliza kama kweli niachane na imani za mababu zangu wa kale (bfr colonialism) na kuadopt hizi imani mpya za kikoloni katika suala la kidini. Kitu kinachonipa utata nimegundua kwamba Mungu wa kikoloni (namaanisha imani za kidini zilizoletwa na wageni afrika) be it Allah or Jehovah na Miungu ya kijadi wote wana sifa zifuatazo zinazorandana.

  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wanatumika kuombwa msaada hasa nyakati za shida, hofu au hatari inapomkabili binadamu.
  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wametengewa maeneo maalumu yanayoheshimiwa sana kwa ajili ya kuendeshea ibada, sadaka/makafara mbali mbali mfano misikiti, mahekalu, mipango, milima maalum au miti mikubwa.
  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wanainfluence utamaduni, kasumba au mtindo wa maisha wa binadamu ambao wanawaamini mfano uislamu na tamaduni zake, ukristo na tamaduni zake, upagani na tamaduni zake.
  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wanatumika katika kuongoza binadamu waishi katika misingi inayokubalika ktk jamii kwa hofu ya kupata laana, adhabu za kiroho baada ya kifo au mabalaa mbalimbali ktk jamii.
  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wanahubiri ukuu na ufalme kwamba hakuna kiumbe yoyote mwenye ukuu na ufalme kushinda wao, na hivyo in return mwanadamu inabidi atoe sadaka au kafara kama kuonyesha utii wake kwa mungu husika.
  • KAMA IKO NYINGINE ONGEZEA WEWE

Bado sijaona hasa mungu yupi kati ya hao anamzidi mwenzie na hili swala la kuchanganywa imani liko sana kwa hizi nchi zetu za dunia ya tatu lakini huwezi kuongea kitu kwa wahindi na Hindu religion yao wala wachina na majirani zao na Budha wao (just to mention the few)

Jumatatu kareem
(dont bother with spelling errors just focus on the content)
 
Kwa sababu hakuna kinachohitaji mungu ama uwepo wa mungu ili kiwepo!


Mungu ni idea na sio real figure ama spirit kama mnavoita.Ni idea tu ambayo ipo tu.
Haja yangu ni kwamba ilikuwaje mungu mwenye upendo wote na nguvu zote akashindwa kuepusha maovu katika dunia aliyoiumba na kuipenda kweli?.Kwa nini kama kwel yupo anashindwa kumwangamiza huyo mnaemwita shetani!?.Je shetani anafanya mambo yake kwa mamlaka ya nani?

Swali hili halijapata jibu bado.
 
Kwa sababu hakuna kinachohitaji mungu ama uwepo wa mungu ili kiwepo!


Mungu ni idea na sio real figure ama spirit kama mnavoita.Ni idea tu ambayo ipo tu.
Haja yangu ni kwamba ilikuwaje mungu mwenye upendo wote na nguvu zote akashindwa kuepusha maovu katika dunia aliyoiumba na kuipenda kweli?.Kwa nini kama kwel yupo anashindwa kumwangamiza huyo mnaemwita shetani!?.Je shetani anafanya mambo yake kwa mamlaka ya nani?

Aina hii ya swali linatakiwa liulizwe na mtu ambae anakubali uwepo wa Mungu na Shetani

Unapotengeneza swali kwa ku assume ni tatizo kwakuwa tayari hiyo ni assumption

Kama hukubali uwepo wa Mungu huna haja ya kuhoji kitu kisichokuwepo!
 
Back
Top Bottom