#COVID19 WHO: Nchi 16 Afrika zimekumbwa na kirusi kipya cha Delta

#COVID19 WHO: Nchi 16 Afrika zimekumbwa na kirusi kipya cha Delta

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
INDIA
Wimbi la tatu la janga la COVID-19 kwa kirusi cha Delta linasambaa kwa kasi barani Afrika na mpaka sasa nchi 16 za bara hilo zimebainika kukumbwa na kirusi hicho.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya duniani (WHO), kirusi hicho kinasambaa kwa kasi zaidi barani Afrika kuliko wakati wowote ukilinganisha na idadi ya wagonjwa waliobainika juma lililopita.

Mkurugezi wa WHO kanda ya Afrika, Dokta Matshidiso Moeti amesema, kuongezeka kwa kasi ya kusambaa kwa kirusi hicho kwenye wimbi la tatu la janga la COVID- 19 ni tishio kwa bara Afrika.

Visa vya wagojwa waliobainika kuwa na virusi vya Delta vimeogezeka zaidi karibu katika wiki sita mfululizo.

Kwa mujibu wa takwimu mpya, wimbi hilo la Delta limebainika kwa asilimia 97% na 79% katika nchi ya Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.

Wakati visa vya Delta vikiendelea kuongezeka na watu kulazwa, WHO inakadiria kwamba mahitaji ya oksijen barani Afrika sasa ni asilimia 50% zaidi kuliko ilivyokuwa waka jana lilipoibuka wimbi la kwanza.
 
Kongo?

Duuuh!

Serikali yetu ADHIMU iharakishe kuuleta mzigo wa CHANJO.

Nimeshalitayarisha BEGA LANGU kupata hizo CHANJO MBILI.

Hali si hali kwa Kweli.

Yaani iko hapo jirani KONGO?

#ChanjoIje
 
Tukisimama na Mungu tena tutashinda.

Ni jukumu letu sote kila mmoja kwa imani yake tumwombe Mungu atuepushe na janga hili.
Ni vile dunia nzima Mungu anatusikiliza sana waTanzania, ngoja tusimame nae sisi si ndio taifa takatifu pekeee duniani!! [emoji848][emoji848][emoji848]

Kwanza hata haja ya kujikinga haipo, tusivae barakoa wala tusifuate tahadhari zote za kitaalamu, sisi si wa Mungu bhana!
 
Ukisikia bendera chuma mlingot chuma ndo hii sasa apa sasa cha muhimu ni maombi tu kwa muumba wetu.
 
Jiwe angekuwepo angetupitisha salama, ila sasa hivi hata sielewi naona mapichapicha tu. Ila freshi tu kufa au kuishi yote kheri tu watu hawajaanza kufa jana.
 
Ni vile dunia nzima Mungu anatusikiliza sana waTanzania, ngoja tusimame nae sisi si ndio taifa takatifu pekeee duniani!! [emoji848][emoji848][emoji848]
Kwanza hata haja ya kujikinga haipo, tusivae barakoa wala tusifuate tahadhari zote za kitaalamu, sisi si wa Mungu bhana!
Lini tulivaa barakoa kwani? 😂😂
 
Hili dubwana kuna waqt kama nalielewa hivi khalafu pana waqt silielewi kabisa waqt maambukizi yanatoka ng 'ambo walibashiri afrika wiki mbili za kwanza wangedondoka watu robo bilioni kutokana na mfumo wetu masikini wa afya matokeo yake kweli watu walifariki lakini sio kwa rate ya wabashiri wetu hii kitu wazungu inawachanganya sana wanajiuliza hawa kima mbona hawadondoki kwa kasi?

Waqt wa mazishi ya raisi kutokana na nyomi ile wakasema hapa sasa matokeo yake kweli watu wanafariki lakini sio kwa kasi ya kuku wa mdondo.

Tuendelea kumuomba mungu na pia hizi tahadhali zetu za ujanja ujanja tuendelea kuzichukua. Kuna waqt hufikiria labda linatulia timing kisha litupe sucker punch ndo maana nasema silielewi.
 
Hili dubwana kuna waqt kama nalielewa hivi khalafu pana waqt silielewi kabisa waqt maambukizi yanatoka ng 'ambo walibashiri afrika wiki mbili za kwanza wangedondoka watu robo bilioni kutokana na mfumo wetu masikini wa afya matokeo yake kweli watu walifariki lakini sio kwa rate ya wabashiri wetu hii kitu wazungu inawachanganya sana wanajiuliza hawa kima mbona hawadondoki kwa kasi? ...
Sasa wamewatengenezea chenu special. Za mwanzo mlichomoka sasa wanatimiza lengo lao.
 
Back
Top Bottom