#COVID19 WHO yasema haina taarifa za COVID-19 kutoka Tanzania

#COVID19 WHO yasema haina taarifa za COVID-19 kutoka Tanzania

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Ulimwenguni, Tedros Adhanom Ghebreyesus, amesema WHO haijapokea taarifa yoyote kutoka Tanzania juu ya hatua zinazochukuliwa na serikali kuhusiana na janga la corona.

Tedros amesema kwenye taarifa yake kwamba hali hiyo inatia wasiwasi na ameitolea mwito serikali ya Tanzania kuanza kuratibu maambukizi ya corona na kutoa data kuhusiana na COVID-19 nchini humo.

Mkurugenzi mkuu huyo wa Shirika la Afya Ulimwenguni amesema, mwishoni mwa mwezi Januari alishirikiana na mkuu wa shirika la WHO barani Afrika Matshidiso Moeti, katika kuihimiza Tanzania kuongeza jitihada kwenye hatua za kiafya dhidi ya COVID-19 na kujiandaa na mikakati ya kutoa chanjo.

Ameitaka Tanzania kuchukua hatua za kuwalinda raia wake na watu wengine ndani na nje ya nchi hiyo.


DW swahili
 
Hawa WHO wanahela na wanahaha pa kuisafisha, yaani Tanzania tukikubali leo hela iliyobakia yote wataileta hapa kisha wakubwa watafahamiana waTZ changamkieni dili hilo.
 
Namba inazidi kupanda Tu.
Hao WHO BURE KABISA
Kwanza WHO wangetuambia hizo hatua wanazotaka tuchukue zimesaidiaje hao waliozichukua ili nasi tushawishike
Screenshot_20210221-092923.jpg
 
Kwani WHO ikipata taarifa za takwimu za COVID-19 kutoka tz wanasaidiaje? Mbona vifo vimezidi hata huko nchi za ng'ambo?
Hivi kwanza WHO ina maana gani na kazi zake ni zipi?

Nadhani ungejua hilo / ukishajua hilo nadhani usingeuliza hili, By the way Tanzania pia inatengeneza hio WHO yaani ni kama chain ambayo is as strong as its weakest link
 
China ilipoanzia corona.kuna wagonjwa wapya 423.
TUNAANZA UPYAAA.
Screenshot_20210221-093308.jpg
Screenshot_20210221-093317.jpg
 
Kwanza WHO wangetuambia hizo hatua wanazotaka tuchukue zimesaidiaje hao waliozichukua ili nasi tushawishike
Huwezi kufanya maamuzi kabla ya kujua ukubwa wa tatizo. Wenzetu vifo vimeanza kupunguza baada ya kuchukua hatua stahiki.
 
Back
Top Bottom