Whozu ananunua gari baada ya kulipwa Tigo Fiesta..

KWANI HUWA WANALIPWA BEI GANI KWA SHOW MOJA
Hakuna kiwango kwa show, ts about negotiations, Hauwezi ukamlipa fid Q kama unavyomlipa Marioo au whozu, inategemeana una hit songs ngapi na una ushawishi kiasi gani, Ndio maana ninasema just tuangalie factors za nje tu ili kubaini kuwa fiesta inawalipa coz ni vigumu kujua wanalipwa kiasi gani, mikataba iko closed sana.
 
Kasema yeye mwenyewe mimi ninaanza vipi kumbishia. Na kasema alifanya show sehemu zote Fiesta ilikofanyika kasoro mikoa mitatu tu.
Oky, ungemuuliza pia huko alikofanya shows alikuwa analipwa bei gani....
Wengine hapo wanahemewa kisogoni na mijeba yenye hela zao!
 
Oky, ungemuuliza pia huko alikofanya shows alikuwa analipwa bei gani....
Wengine hapo wanahemewa kisogoni na mijeba yenye hela zao!
Be positive, hata haya hakuulizwa kaandika mwenyewe bila kuulizwa siku akijisikia kusema analipwa shilingi ngapi pia atasema bila kuulizwa.
Kwani Mark X hiyo bei gani haizidi hata mls 16, Sasa kwa Shows 13 hata angekuwa analipwa mils 1.5 bado angeinunua tu.
Angeandika kuwa kadhulumiwa huenda usingesema aweke mkataba uone unasemaje, ungewashambulia moja kwa moja anaodai wamemdhulumu.
 
Whozu alizunguka na fiesta mikoa yote Tz mwaka huu

Kama ntakua niko sahihi nadhani ni mikoa zaidi ya 11

Alikua analipwa 1.5mil kwa kila show.Ukipiga mahesabu hapo amekusanya sio chini ya 15m,may 20m

Amenunua gari (asset) la sh 13mil - 16mil...

Hongera kwake kwa kujiongezea matumizi ya maisha (mark x ni jini mafuta kwa mlalahoi kama mimi)

Tusubili mwakani tena Fiesta inayofuata...may be atapata ela ya kujenga anagalau nyumba ya vyumba viwili.
 
Kasema yeye mwenyewe mimi ninaanza vipi kumbishia. Na kasema alifanya show sehemu zote Fiesta ilikofanyika kasoro mikoa mitatu tu.

Hatumbishii mkuu, ila ni vile tu wasanii wana hizi culture za kutuzuga baadhi ya vitu, mfano:

- Diamond aliwahi kuazimwa V8 na pedeshee kitu kama Katunzi (sikumbuki vizuri) akasema kanunua
- Wema aliwahi kuuambia uma nyumba aliyopanga Kijitonyama kainunua, kulikuwa na Range aliazimwa au sijui ilikuwaje, alisema ni take
- Sheta alitutambia na V8 ya kuazima akisema ni ya kwake
- Nay wa Mitego aliwahi kutuonesha nyumba ya around 70mil akasema imemgharimu mil 300
- Kuna kina Giggy na mawigi ya mil 6
Hao ni wasanii na usanii ni kazi yao, hiyo nayo ni sanaa.
 
Hili gari la bei ndogo halifiki hata mls 16 sidhani kama anashindwa kununua kama vijisent vyake vyote alikuwa anvikusanya kutimiza hili.
 
show 13 kati ya 15 alizoperform kaambulia mark x tu.....kweli wasanii wananyonywa
 
Hili gari la bei ndogo halifiki hata mls 16 sidhani kama anashindwa kununua kama vijisent vyake vyote alikuwa anvikusanya kutimiza hili.

Very possible mkuu, ukisoma vizuri andiko langu, sina mahali nakopinga, ila nimeweka all possibilities open.

Msanii na mwanasiasa nawatifautisha kidogo sana, mmoja anaficha idadi ya mali zake (zake anasema si zake), mwingine anakuza idadi ya mali zake (anasema ambazo si zake ni zake).
 
show 13 kati ya 15 alizoperform kaambulia mark x tu.....kweli wasanii wananyonywa
afadhali kaambulia hiyo ndani ya show 13 tena kwa muda usiozidi miezi 3, waajiliwa mbona wanamaliza miaka 40 kwenye ajira halau wanaambulia kiinua mgongo cha mils 84 ambazo nazo hawapewi zote.
Halafu unaweza kukuta unayemcheka mwenzako kila mwisho wa mwezi unapokea mshahara haufiki hata laki 6. Na pia hajasema ela yote kainunua Mark X ila kasema kwa sasa ameanza jitegemea haishi kwa wazazi na kanunua usairi yote ni matunda ya shows alizofanya.
 
Kwenye kuongeza masufuri hapo nawakubari nakumbuka Ommy dimpoz aliponunuaga Mark X kama hii akasema kainunua mls sijui 25
 
Msanii anaona fahari kumiliki gari wakati akiishi maisha ya kuigiza na pengne amepanga!!
 
Hongera sana kwa kuvuta Mark Matusi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…