Katika lugha ya Kilatini, neno Apple maana yake ni malum, (evil) lakini baadaye, katika kuhalalisha apple kuwa alama ya mapenzi na thamani, matunda mengi yalijulikana kama apples, kwa mfano, nyanya (tomatoes) na matango (cucumbers) ziliitwa Love apples. What a coincidence of color and shape!
Lakini ilikuwaje lile tunda lililokuwa alama ya uasi na dhambi, ghafla likageuka kuwa alama ya mapenzi?
Sababu iko kwenye swali, uasi na dhambi za Adam na Eva ndizo zilizozaa mapenzi pale walipokula tunda lililokatazwa.
Na kuanzia wakati huo, tunda limekuwa alama ya yote mawili - mapenzi na dhambi, wema na uovu, yote ikitegemea vipi, muda gani [na hata nani na nani] tunda linaliwa.
Ni kwa kula tunda hilo, ndio maana wakazaliwa Abel na Cain - ishara za wema na uovu/uasi na dhammbi, mapenzi na chuki. Cain alipoasi ile amri ya nani amuoe nani kwa ajili ya mapenzi ndio ugomvi ulipoanza na mmoja kumuua mwenzake -dhambi.
Na tokea wakati huo, wana wa Adam na Eva tumekuwa tukiishi hivyo. Kutokana na utamu wa tunda, tunafumba macho na kuona utamu na matunda yake tu (taste, feelings, reprduction) bila ya kujali dhambi zinazotokana nalo pale tunapovunja amri za Muumba, kiasi kwamba leo tunda hili linachukuliwa kuwa ni alama ya mapenzi tu.