Uchaguzi 2020 Why Bernard Membe is not a presidential material, at all!

Uchaguzi 2020 Why Bernard Membe is not a presidential material, at all!

pia nashauri mods waiondoe thread hii kwa vile inapandikiza chuki kwa viongozi(Membe vs Magufuli) wakati hawa si maadui ,kama ni propaganda zenu "mumebugi men"

greenstar hivi unaweza kujieleza kwa umombo maana naona hata mada hujaielewa kabisa magufuli na membe kugonganishwa na hii mada wapi na wapi?...............au unataka tujenge utamaduni wa kusifiana tu kiunafikinafiki hivi?
 
Last edited by a moderator:
Huyu ni January Makamba undercover. Hizi ni aina za speech mbofu mbofu alizokuwa anamwandikia JK; anatumia maneno ya ajabu ajabu ya kiingereza kunogesha hotuba bila kujali hoja ya hotuba yenyewe.

[MENTION]UgonjwaUkimwi[/MENTION]......hivi Makamba anaweza kuyaandika haya au basi hata anayaelewa? Huu ukimwi wako huo kaa nao tu ndugu yangu miye nauogopa hivi..............
 
umemu-attack personally kuliko hoja alizotoa, mfano aliongelea 'how to break a poverty circle' na akasema ni kwa kufanya 'rular transformation' ndo tunaweza kutoka kwenye hii circle....do you agree with him?, why? and you have to give yours too...tukupime...ulichofanya ni kumu-attack personally kama mtu anayesaka uraisi na sio hoja muhimu kwa taifa alizozitoa...ni hatari kwa taifa kuwa na watu 7 selfish kama wewe, nenda kasome 'LEVIATHAN' ya Thomas Hobbes na urudi na mawazo mazuri.

Az 89..rural transformation? If you believe this nonsense then you will believe anything.................huo ni msamiati tu hauna uhusiano wowote ule na uwezo wa kuyatatua matatizo ya nchi hii. Kilichoshindikana kuwa na hiyo "rrural transformation" wakati huu ambao yeye ni waziri tena wa mambo ya kigeni ni nini? Kama siyo gheresha zake mbaya zaidi hata hakujibu maswali ya how, why, when....................and in particular why did he not initiate them in 2005? Zaidi ya kutetea ufisadi wa radar?
 
Last edited by a moderator:
quote_icon.png
By Rutashubanyuma

Vonix kutofaa haiamaanishi hatakuwa Raisi..............JK hafai lakini tuko naye na suti zake
At least umenifurahisha

Az 89 Kwa hiyo unachekelea bora liende? Au bora kiongozi kulikoni kiongozi bora?
 
Last edited by a moderator:
This Rutashubanyuma's post presents an opportunity for me to recirculate what I wrote about the same aspirant some years ago. Enjoy it!


Katika orodha ya wanaotajwa kuwania uteuzi wa ccm kwa nafasi ya urais wa JMT-2015, namba mbili (2) katika nisio shawishika nao ni Mh. Bernard Membe. Mh. Membe hanishawishi kuwa anastahili nafasi hiyo kwa sababu zifuatazo:


  1. 1. Historia halisi ya utendaji wake kama Mbunge na Waziri haina matokeo yanayosimama kumshuhudia Mh.Membe kama mtu wa kuleta mabadiliko chanya au maendeleo.

Asiyeweza katika dogo, ataweza katika makubwa? Mbele ya wapigakura wa Jimbo la Mtama, Mh. Membe anaonekana kama mtu aliyeshindwa kutimiza ahadi zake za muhula wa kwanza (2005-2010). Na walio wengi hawaoni umuhimu/mchango wa ukaribu wake na serikali katika kuwaletea mabadiliko. Ndo maana Mh. Membe alipata wakati mgumu sana kutoka kwa mgombea wa TLP, mtu ambaye hakuwa na jina, mali wala pesa bali support ya wananchi. Lakini kwa kutumia utaalamu aliojaaliwa, Mh. Membe aliweza "kumshughulikia" na kumdhibiti mpinzani huyu pekee na kuhakikisha wapiga kura wanakosa chaguo mbadala wakati wa uchaguzi. Ninashawishika kufikiri kuwa hata mpinzani mmoja angepenya na kusimama, matokeo ya Jimbo la Mtama yangekuwa sawa na ya Nyamagana.

Kuna jambo moja ambalo Mh. Membe ameshiriki na watu wasio na kumbukumbu nzuri au wafupi katika kuchambua mambo wanaweza kusema kalifanikisha. Ni suala la kurejeshwa kwa fedha za rada kupitia serikali badala ya NGOs kama wezi walivyotaka. Hii haiwezi kuhesabika kama jitihada ya Mh. Membe wala serikali ya Tanzania. Hili silielezi kwa ufasaha ili watu wajadili……………………..


  1. 2. Misingi ya mbinu anazotumia Mh. Membe katika kusaka kuungwa mkono na makundi yenye ushawishi mkubwa katika jamii haina maslahi kwa Taifa na inatengeneza viporo vya uporaji wa rasilimali za nchi na migogoro mikubwa ya kijamii hapo baadae.
Mathalani, katika suala la serikali kuanzisha na kuendesha Mahakama ya Kadhi na serikali ya JMT kujiunga na OIC, Mh. Membe akiwa mbele ya waandishi wa habari amekuwa akiwaondoa hofu wahusika kuwa haya mambo hayana shida na serikali iko katika hatua mbalimbali za kuyatekeleza. Mara tu upande wa pili wakianza kupaza sauti za kupinga, Mh. Membe hu-haha na hukimbia kimya kimya kwenda kwa viongozi wakuu wa upande wa pili "kutuliza mambo" kwa kificho. Katika hili, Mh. Membe anataka kuuma na kupuliza na ni ndumila kuwili. Ni vema, si kwa Mh. Membe tu, bali wanasiasa wote kuimarisha msingi wa msimamo ambao umekwishafikiwa na serikali katika suala hili nyeti.

Mh. Membe anasimama miongoni mwa viongozi wa Bara la Afrika waliosimama kidete kuomboleza kifo cha Shujaa wetu Mummar Gadaff. Lakini nyuma ya kilio na maombolezo ya msiba huu, kumefunikwa giza totoro la vitendawili juu ya nini haswa "majonzi" ya Mh. Membe? Wako wanaotoa nuru ili kutegua vitendawili kwa hadithi tofauti tofauti ambazo kwa ujumla wake ukizikusanya kwa ushambuzi makini unapata picha pana juu ya makubaliano/fadhila za utawala uliongushwa Libya kwa mgombea mtarajiwa. Watanzania tunapaswa kuwa tumejifunza madhara ya wagombea wetu kufadhiliwa na matajiri (nchi au mtu binafsi). Tutumie 2015 kuepuka kurudi chini ya utawala wa waliofadhili wagombea katika chaguzi kuu.

Mh. Membe anapigania uraia wa nchi mbili. Kwa faida ya nani? Binafsi sioni kama hili jambo lina tija kwa Taifa lenye uchumi unaomilikiwa na asilimia mbili (2%) ya wananchi wake na ndio asilimia tisini na nane (98%) ya hao hao tayari wana uraia wa nchi zaidi ya mbili. Hapa Mh. Membe hasimami kutetea rasilimali watu za Watanzania walioko nje bali kutafuta kuongeza wigo wa kuungwa mkono na watu wasiokuwa na uchungu wa nchi hii. Hawa tunaowaita "Watanzania wenye asilia ya Kihindi" ambao ndo wanashawishi sana suala hili tayari wanao uraia Uswizi, Canada, Marekani na hapa kwetu kutokana na udhaifu wa idara zetu za uhamiaji wanaishi na kufanya wanalotaka kwa jeuri ya pesa yao.

Nahitaji kushawishiwa kwa historia na utendaji upi Mh. Membe anastahili kuomba ridhaa ya kubeba bendera ya ccm katika uchaguzi mkuu 2015. Michango yenu ikiwemo matusi na dhihaka vinakaribishwa. Na kuwa na hakika, nitavipokea vyote kama vilivyo. Kwa namna ya pekee nausubiri mchango wa MBOPO, mtu ambaye mara nyingi hujitahidi kujibu hoja na si kujadili mtoa hoja katika kumtetea Mh. Membe.


Nawatakia Mwaka Mpya Mwema na Wenye Mafanikio.

Omutwale kutoka Kanyigo.
 
- Bro. Rais bora haamuliwi kwa Speech moja UDASA, halafu ungewataja unaowaona wanafaa kuliko Membe!!, Waziri wa Nje miaka 7 kama hafai kuwa Rais ina maana moja tu kwamba hakuna anayeafaa, and that is pathetic wapo na Membe ni mmojawapo!!

Es!

ha ha...kwani kuwa waziri wa mamabo ya nje alikuwa akipitia chujio fulani?Membo ni uozo na amalindwa na huo uozo kwa muda mrefu,kwanza ni puppet.Atakuweje rais hakuweza kuw ana unasiri au kuona shida ya hel aya ghaddafi kw akiasi cha kufunika ukweli kuhusu maisha haramu ya Ghaddafi.

Membe keshatotuloea nchi moja ktk diplomasia yetu nayo ni Libya.Walibya hawana sabbu ya kuwa na sisi, tumewatosa kipindi walituhitaji, na hata kipindi tulipowatosa,wakajituma na kumuondoa ghaddafi hatukuwatambua,.Soon CCM nao wataingia ktk same path kama Ghaddafi.

HUyo Peppert wa Ghaddafi hana faida kwa nchi, atakuwa kibaraka wa watu wengi wa aian ya Ghaddafi.
 
kwetu hatupigi matunda mawe,wala kuwachoma ng`ombe ili kuwaweka alama.Sisi huw atunapiga mawe mti wenye wadudu na wanyama wabaya ambao hawafikiwi kirahisi, kama nyoka , na wanyama waharibifu.Bado mnapiga mawe matunda?Ndio maana basi matunda yanakosa thamani hata kwa mlaji ktk famailia zenu.

Kuna mwanamke mmoja alitaka kujaribu ukweli wa mgaa gaa na upwa hali wali mkavu, hivyo akapika wali wake kisha akaenda zake pwani kugaa gaa kisha akarudi akitegemea kukuta mchuzi, kilicho mkuta unaweza kutabiri. Ndicho ulichokifanya hapa.
 
Kuna mwanamke mmoja alitaka kujaribu ukweli wa mgaa gaa na upwa hali wali mkavu, hivyo akapika wali wake kisha akaenda zake pwani kugaa gaa kisha akarudi akitegemea kukuta mchuzi, kilicho mkuta unaweza kutabiri. Ndicho ulichokifanya hapa.

sidhani kama hiki ndicho ulikuwa ukimaanisha.Sidhani kama utakuwa sahihi, mgaa gaa na napwanihali wali mkavu ni kwamba akigaa pwani basi hawezi kosa hata samaki fulani ambao wavuvi hawaoni shida mpatia, na kwa ajuaye hilo hawezi tegemea mchuzi ujitengeneze wakati anajua anahitajia kurudia na samaki aje tengeneza mchuzi.

Sasa umeanza na premises nzuri ila ukamalizia na wrong conlusion.Na wewe ni gamba nini?Sisi huwa hatupigi mawe miti yenye matunda, kwa vile hatupendi haribu matunda wata mti na eneo lililochini ya huo mti.Huwa tunachuma au kutumia miti au ngazi kuchuma.Nimekuwambia si kupiga mawe tuu hata kuwaweka wanyama alama wka moto hatufanyai kwa vile hatutaki haribu thamani ya ngozi.

Tunapiga miti yenye wanyama na wadudu hatarishi au waharibifu kama nyoka, nyani na ndege waharibifu.Una enjoy kuwa gamba mwenyewe..Sishangai kwanini CCM haiwezi saidia hii nchi kuendelea hata miaka 1000 ijayo.Sishangai kma kabila ulilotoka linaharibu vitu sana, pengine hawana food security kabisa au wakiwa nyuma kabisa.
 
sidhani kama hiki ndicho ulikuwa ukimaanisha.Sidhani kama utakuwa sahihi, mgaa gaa na napwanihali wali mkavu ni kwamba akigaa pwani basi hawezi kosa hata samaki fulani ambao wavuvi hawaoni shida mpatia, na kwa ajuaye hilo hawezi tegemea mchuzi ujitengeneze wakati anajua anahitajia kurudia na samaki aje tengeneza mchuzi.

Sasa umeanza na premises nzuri ila ukamalizia na wrong conlusion.Na wewe ni gamba nini?Sisi huwa hatupigi mawe miti yenye matunda, kwa vile hatupendi haribu matunda wata mti na eneo lililochini ya huo mti.Huwa tunachuma au kutumia miti au ngazi kuchuma.Nimekuwambia si kupiga mawe tuu hata kuwaweka wanyama alama wka moto hatufanyai kwa vile hatutaki haribu thamani ya ngozi.

Tunapiga miti yenye wanyama na wadudu hatarishi au waharibifu kama nyoka, nyani na ndege waharibifu.Una enjoy kuwa gamba mwenyewe..Sishangai kwanini CCM haiwezi saidia hii nchi kuendelea hata miaka 1000 ijayo.Sishangai kma kabila ulilotoka linaharibu vitu sana, pengine hawana food security kabisa au wakiwa nyuma kabisa.

Kweli ya haki husemwa, pano hitaji hekima,
Muungwana akibanwa, busara chini inama,
Kama chupi ikiporwa, si vyema wima simama,
Kwa mwenye zake hekima, huchagua kuchutama.
 
- Bro. Rais bora haamuliwi kwa Speech moja UDASA, halafu ungewataja unaowaona wanafaa kuliko Membe!!, Waziri wa Nje miaka 7 kama hafai kuwa Rais ina maana moja tu kwamba hakuna anayeafaa, and that is pathetic wapo na Membe ni mmojawapo!!

Es!

Field Marshall ES...........angalau unakiri ile hotuba imemwangusha......................na kuhusu uzoefu wa uwaziri wa nje.........jk miaka 10 ya mambo ya nje na 27 in total kwenye baraza la mawaziri kabla y kuwa raisi lakini karibu sote tunamwona ni kilaza.........kumbuka malecela aliikamata hiyo wizara kwa miaka mingi lakini aliishia kuangukia pua..............
 
sidhani kama hiki ndicho ulikuwa ukimaanisha.Sidhani kama utakuwa sahihi, mgaa gaa na napwanihali wali mkavu ni kwamba akigaa pwani basi hawezi kosa hata samaki fulani ambao wavuvi hawaoni shida mpatia, na kwa ajuaye hilo hawezi tegemea mchuzi ujitengeneze wakati anajua anahitajia kurudia na samaki aje tengeneza mchuzi.

Sasa umeanza na premises nzuri ila ukamalizia na wrong conlusion.Na wewe ni gamba nini?Sisi huwa hatupigi mawe miti yenye matunda, kwa vile hatupendi haribu matunda wata mti na eneo lililochini ya huo mti.Huwa tunachuma au kutumia miti au ngazi kuchuma.Nimekuwambia si kupiga mawe tuu hata kuwaweka wanyama alama wka moto hatufanyai kwa vile hatutaki haribu thamani ya ngozi.

Tunapiga miti yenye wanyama na wadudu hatarishi au waharibifu kama nyoka, nyani na ndege waharibifu.Una enjoy kuwa gamba mwenyewe..Sishangai kwanini CCM haiwezi saidia hii nchi kuendelea hata miaka 1000 ijayo.Sishangai kma kabila ulilotoka linaharibu vitu sana, pengine hawana food security kabisa au wakiwa nyuma kabisa.
Last edited by Nicholas; Today at 10:36.

Nicholas usichoke kutoa darasa la bwerere.......
 
Last edited by a moderator:
Nawatakia Mwaka Mpya Mwema na Wenye Mafanikio.

Omutwale kutoka Kanyigo.
[MENTION]
Omutwale[/MENTION]......................waitu amutwale nkhaaaaaa
 
despite hizo weakness huyu ndo rais wenu, wedha u like it or not, and the reason
is obvious, the president of URT is not elected by people/masses as such, but by a bunch of selfish party crooks with support of state apparatuses
 
Kwa kifup mi naona anafanana na mwenzake wa magogon. Kama kwel 2nataka uongoz mpya Ikulu, bas mjue huyu hatakuwa mpya pale, kiutendaji.
 
Kweli ya haki husemwa, pano hitaji hekima,
Muungwana akibanwa, busara chini inama,
Kama chupi ikiporwa, si vyema wima simama,
Kwa mwenye zake hekima, huchagua kuchutama.

n haya nayo unaanisha yalistahili hapa?Au yameponyoka?Sometimes uwe na courtesy ya kukubali kuwa hukuumia mfano vizuri.
 
Field Marshall ES...........angalau unakiri ile hotuba imemwangusha......................na kuhusu uzoefu wa uwaziri wa nje.........jk miaka 10 ya mambo ya nje na 27 in total kwenye baraza la mawaziri kabla y kuwa raisi lakini karibu sote tunamwona ni kilaza.........kumbuka malecela aliikamata hiyo wizara kwa miaka mingi lakini aliishia kuangukia pua..............

ha ha..wanakukumbusha disasater ingine ktk CCM.Hivi kuna namna ya kuwaangalia hawa mawaziri wa nje wanafanya nini?Naona ni mabalozi wazuri wa ujinga duniani.
 
Nicholas usichoke kutoa darasa la bwerere.......

Tataizo la hawa jamaa ni kwamba huwa wanafanya mambo yawe ubishi na hivyo mjadala unakuwa hauna nafasi sana ya kuelimishana.Kiuhasilia watu wangekuwa wanajadili vitu bila ushabiki, kila mtu angeweza mfundisha mwenzie kitu fulami.Ila kuna watu wanaingia humu kilinda kambi zao.Kwa kuropoka au kudai picture.
 
Watu wameashaanza roho mbaya yaani point zote hamna hata yenye maelezo ya kueleweka zaidi ya kujificha nyuma ya misamiati mirefu tu....ukweli ni kuwa Membe au yoyote yule anahaki ya kujitutumua kwa makusudi au kwa kusingiziwa. Wacheni majungu na tusubiri 2015..
 
Back
Top Bottom