Why blacks?

Why blacks?

Jim007 2

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2012
Posts
395
Reaction score
247
Wakuu habarini.

Toka kuumbwa kwa huu ulimwengu mtu mweusi amekua akibaguliwa na mtu mweupe! hivi nini asili ya chuki hii.

Tukikumbuka slavery.

Apartheid.

Nadhani kuna la zaidi kwa hawa wenzetu kuhusu blacks.

Asanteni
 
Hakuna la zaidi kwa hawa wenzetu sema mazingira tu ndo yanayosababisha tunatofautiana.
 
Tangu nilipoulizwa kwa nini hakuna mitume weusi na sikuwa na jibu basi tena!!!!!
 
Mtu mweusi anajishusha mwenyewe, anajibagua mwenyewe. Tatizo liko kwenye akili ya kitumwa kichwani mwa weusi. Mfano mzuri upo kwa viongozi weusi ambao wanajikomba na kuamuliwa na wazungu pamoja na mamlaka yote waliyopewa na watu wao.
Sikiliza kwa makini hotuba za viongozi weusi kwenye hadhara za kimataifa, zote za kuombaomba, kunyenyekea nyekea na mengine yanayofanana na hayo.
Hali hii itabadilika tu baada ya weusi kufanya mapinduzi ya fikra na waweze kujiona wao ni bora zaidi kwa nafasi yao!
 
Mkuu hoja yangu ni katika kujua kuna cha zaidi katika chuki ya mtu mweupe kwa mtu mweusi??kuna ovu gani ambalo mtu mweusi amelitenda kihistoria hadi kufikia hatua ya kudhaurika na kunyanyaswa na mtu mweupe??
 
Toka kuumbwa huu ulimwengu?

Una hakika?

Mkuu Kiranga ninakuheshimu sana kwani nina imani kupata mengi toka kwako.....historia yangu haijakaa sawasawa lakini sikumbuki ni lini mtu mweusi amewahi pata heshima kwa mtu mweupe....nimeanzia kwenye era ya slavery kujustify thread yangu....karibu mkuu unijuze nisiyoyafahamu
 
Tangu nilipoulizwa kwa nini hakuna mitume weusi na sikuwa na jibu basi tena!!!!!

Hahahah mkuu OLESAIDIMU hoja yako inafikirisha kiasi....ila sidhani kama hata hao waliopita kuna ushahidi kua walikua weupe!!!maybe kuna kina TB Joshua siku hizi(am not sure kwa hili)
 
Mkuu Kiranga ninakuheshimu sana kwani nina imani kupata mengi toka kwako.....historia yangu haijakaa sawasawa lakini sikumbuki ni lini mtu mweusi amewahi pata heshima kwa mtu mweupe....nimeanzia kwenye era ya slavery kujustify thread yangu....karibu mkuu unijuze nisiyoyafahamu

Tatizo unaanzia kwenye era ya slavery, ungesema kwa nini mtu mweusi hapati heshima tangu slavery ungekuwa na hoja. Lakini huko nyuma mtu mweusi alifanya biashara na mtu mweupe on equal footing.

Karl Peters alivyokuja kuchukua nchi aliwekeana mikataba na masultani wa pwani ya Tanzania ya sasa. Hakuja na jeshi kuswaga watu tu. Admittedly mikataba ilikuwa ya treachery, lakini aliingia kwa heshima ya treaty.

Kabla ya hapo watu wa Azania walifanya biashara kama watu sawa na Wachina, Waliokaa Uingereza ya sasa walinunua chuma kutoka Afrika mashariki katika biashara iliyohusisha watu sawa, wao hawakujua kutengeneza chuma.

Hata hiyo biashara ya utumwa yenyewe mostly iliendeshwa na machifu wa Kiafrika waliokuwa wanawauza maadui zao na mateka wa vita. Wazungu waliokuja kununua watumwa walifanya biashara na hawa machifu kama watu sawa.

Mansa Musa alivyokwenda kuhiji Mecca mwaka 1324 alimwaga dhahabu hapo Cairo watu bado wanazungumzia habari zake mpaka leo, alifanya mpaka bei ya dhahabu ipungue. Huyu alikuwa mtu mweusi aliyeheshimika dunia nzima. Watu kutoka pande zote za dunia walikuwa wanakuja kwenye chuo kikuu cha Timbuktu kusoma na kukopi vitabu.

Contrary to popular belief, Waafrika wamefanya biashara kwa muda mrefu na sehemu nyingine za dunia kama watu sawa. Matatizo ya kudharauliwa mtu mweusi yameanza baada ya watu weusi kudharauliana wenyewe na kujifungia sana tusitoke huko Afrika.

Waafrika walikuwa majenerali walioheshimika katika majeshi ya Warumi. Wengine waliwapiga Warumi bado kidogo wauangushe ufalme huu mkubwa.

Someni kabla ya kutoa habari ambazo si timilifu.

Shukurani kwa kuanzisha uzi tuweke record straight.

I am not saying this out of racial pride or black supremacy - which I think is just as bad as white supremacy - but historically sound accounts.
 
Tatizo unaanzia kwenye era ya slavery, ungesema kwa nini mtu mweusi hapati heshima tangu slavery ungekuwa na hoja. Lakini huko nyuma mtu mweusi alifanya biashara na mtu mweupe on equal footing.

Karl Peters alivyokuja kuchukua nchi aliwekeana mikataba na masultani wa pwani ya Tanzania ya sasa. Hakuja na jeshi kuswaga watu tu. Admittedly mikataba ilikuwa ya treachery, lakini aliingia kwa heshima ya treaty.

Kabla ya hapo watu wa Azania walifanya biashara kama watu sawa na Wachina, Waliokaa Uingereza ya sasa walinunua chuma kutoka Afrika mashariki katika biashara iliyohusisha watu sawa, wao hawakujua kutengeneza chuma.

Hata hiyo biashara ya utumwa yenyewe mostly iliendeshwa na machifu wa Kiafrika waliokuwa wanawauza maadui zao na mateka wa vita. Wazungu waliokuja kununua watumwa walifanya biashara na hawa machifu kama watu sawa.

Mansa Musa alivyokwenda kuhiji Mecca mwaka 1324 alimwaga dhahabu hapo Cairo watu bado wanazungumzia habari zake mpaka leo, alifanya mpaka bei ya dhahabu ipungue. Huyu alikuwa mtu mweusi aliyeheshimika dunia nzima. Watu kutoka pande zote za dunia walikuwa wanakuja kwenye chuo kikuu cha Timbuktu kusoma na kukopi vitabu.

Contrary to popular belief, Waafrika wamefanya biashara kwa muda mrefu na sehemu nyingine za dunia kama watu sawa. Matatizo ya kudharauliwa mtu mweusi yameanza baada ya watu weusi kudharauliana wenyewe na kujifungia sana tusitoke huko Afrika.

Waafrika walikuwa majenerali walioheshimika katika majeshi ya Warumi. Wengine waliwapiga Warumi bado kidogo wauangushe ufalme huu mkubwa.

Someni kabla ya kutoa habari ambazo si timilifu.

Shukurani kwa kuanzisha uzi tuweke record straight.

I am not saying this out of racial pride or black supremacy - which I think is just as bad as white supremacy - but historically sound accounts.

Mkuu Kiranga,

Yaliyopita si ndwele, tungange yajayo!

Tunatakiwa kuwajengea uelewa watu wetu na hasa watoto wetu kuwa wanaweza kuwadhibiti watu wa rangi zote duniani na wasikubali kujishusha na kudharauliwa. Mtu yeyote yule akijifanya yuko juu yao, hasa mgeni wamshughulikie inavyostahili bila kujali sana madhara kwake bali wajali zaidi madhara kwetu! Kwa msingi huo jamii yetu itaanza kuinuka.
 
Mkuu mtoa mada Hannibal Barca the greatest military general of all time alikuwa mweusi tiii

Ancient Egyptians builders of the pyramids walikuwa weusi

Waafrika toka enzi walikuwa great people
 
Wakuu habarini.....toka kuumbwa kwa huu ulimwengu mtu mweusi amekua akibaguliwa na mtu mweupe!!hivi nini asili ya chuki hii...tukikumbuka slavery...apartheid!!nadhani kuna la zaidi kwa hawa wenzetu kuhusu blacks...asanteni

Hata weusi kwa weusi tunabaguana. Watu wanajibadili rangi ili wawe weupe. Wanashonea manywele yanayofanana na ya Wazungu. Tunajipa majina ya Kizungu. Tunaona mtu anayeongea Kiingereza kana kwamba ndo ana akili sana.

Ili uonekane umestaarabika na huna mambo ya Kiswahili, ni lazima ujiweke ki-namna flani flani. Ama kwa kuongea Kiswahili na kuchanganya changanya sana na Kiingereza, kuongea Kiingereza na kujifanya kama hujui Kiswahili au kufuatilia sana mambo ya Ulaya na Marekani (vipindi vya runinga, muziki, sinema, na kadhalika).

Tunazigawa sehemu zetu kulingana na hadhi za watu. Watu wanaojiweza wanaishi Uzunguni. Kwingine ni Uswahilini. Hivi kwa nini iko hivyo?

Kama sisi kwa sisi hatuheshimiani wala kuthaminiana, kama sisi wenyewe hatupendi wala kuthamini vya kwetu, basi wala sishangai hao wengine kutudharau na kutubagua.
 
Wakuu habarini.....toka kuumbwa kwa huu ulimwengu mtu mweusi amekua akibaguliwa na mtu mweupe!!hivi nini asili ya chuki hii...tukikumbuka slavery...apartheid!!nadhani kuna la zaidi kwa hawa wenzetu kuhusu blacks...asanteni

If you employ some of "them" like I did, they will call you SIR. I am Sir to them, No low self esteem here. You got to be ahead of the game.
 
Mkuu Kiranga,

Yaliyopita si ndwele, tungange yajayo!

Tunatakiwa kuwajengea uelewa watu wetu na hasa watoto wetu kuwa wanaweza kuwadhibiti watu wa rangi zote duniani na wasikubali kujishusha na kudharauliwa. Mtu yeyote yule akijifanya yuko juu yao, hasa mgeni wamshughulikie inavyostahili bila kujali sana madhara kwake bali wajali zaidi madhara kwetu! Kwa msingi huo jamii yetu itaanza kuinuka.

Kwa kiasi fulani naweza kukubali kwamba yaliyopita si ndwele.

Lakini pia kinga na kinga ndipo moto uwakapo, na tena mtondoo haufi maji kama vile jungu kuu lisivyokosa ukoko.

Kwa hiyo kueleweshana ni ada.

Bila kujua yaliyopita, hata hayo yajayo kuganga itakuwa vigumu, watoto ambao hawajasoma Herodotus na Homer watafikiri watu weusi siku zote walikuwa wanyonge kwa weupe tu. Wakati Herodotus kaandika habari za majeshi ya Cambyses yalivyokula kichapo kikali mpaka ku retreat kutoka kwa healthy "Ethiopian" (the ancient name for black Africans) soldiers. Herodotus kaandika kwamba Ethiopians walikuwa warefu, wazuri na wanaishi maisha marefu kuliko sehemu yoyote.

Hakuna kujenga uelewa mzuri unaotazama mbele kwa kuzingatia usawa wa binadamu kama hatujaeleweshana kwamba hii hali ya unyonge tuliyonayo sasa imeanza relatively late na haikuwa hivi siku zote.

Vijana wakijua kwamba kuna wakati mtu mweusi alikuwa ni mtu mwingine tu dunia hii, si mtu wa chini kwa mwingine, labda wataweza kujua kwamba tunaweza kurudi hapo tena.

Kwa hiyo, kwa mtazamo huo, yaliyopita yanaweza kuwa na umuhimu hata kama tunajua kwamba hatuwezi kuishi kwenye past glory.
 
Pia waafrika walipata heshima kutoka kwa weupe hasa pale waethiopia walipompiga Ufaransa...
 
Back
Top Bottom