Why Magufuli administration misses the point on Government splurge

Why Magufuli administration misses the point on Government splurge

Status
Not open for further replies.
Do we learn anything or do we blithely play the same old tune time and time again until a Burkina Faso style of revolution removes the stylus from a defective record to end playing repeated tunes again and again to our own detriment.
 
Politicizing environmental issues for political gain sucks!

[emoji116]

1472728525836.jpg
 
Mbowe may cloak himself under political victimization but his tormentors saw his weaknesses too.

The guy is powermonger and while sympathizing with him makes sense but we cannot overlook the sheer size of his carelessness, managerial wants and crooked inclinations!

The hovering question remains where is his leadership credibility after this public humiliation?


The jury is unanimously decided that he should pass the chadema baton to more attractive youth there paving ways to a new leadership dawn.
 
TAARIFA YA MHE. FREEMAN AIKAELI MBOWE KUHUSU MADAI YA NHC.

Nimepata taarifa ya mkutano wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Waandishi wa habari kuhusu kilichoitwa "wadaiwa sugu" wa NHC ambapo katika orodha hiyo kampuni ambayo nina hisa ya Mbowe Hotels Co.Ltd imeorodheshwa kama mdaiwa anayedaiwa zaidi ya Shilingi Bilioni moja.

Nakiri kuwepo kwa mgogoro wa kibiashara wa miaka mingi baina ya Kampuni hii na NHC. Aidha kampuni hii imekuwa ikilipa kodi stahiki kwa NHC kwa mujibu wa makubaliano yetu ya kibiashara.

Kumekuwepo na ukakasi wa muda mrefu kuhusiana na mkataba wetu wa umiliki, uendelezaji na uendeshaji wa jengo hili unaochagizwa na msimamo wangu wa kisiasa.

Haki na Uhuru wetu wa kufanya biashara kama raia wengine umekuwa ukiingiliwa mara kwa mara katika mazingira yanayoambatana na Vitisho kiasi ambacho Maamuzi kadhaa hayafanyiki kwa hofu ya kisiasa kwamba "Itakuwa kumwongezea nguvu Mpinzani".

Hivyo, ningependa umma wa Watanzania uelewe kuwa sidaiwi na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC).

Kufuatia utata huu wanasheria wa Kampuni wanashughulikia jambo hili kwa taratibu za kibiashara na kisheria.

Naomba kuweka wazi kwa yeyote anayehusika. Sitafungwa fikra, sitafungwa mdomo na sitaacha kuutetea Ukweli, Haki na Demokrasia katika nchi hii kwa misingi ya "kulinda kinachodhaniwa ni maslahi yangu ya kibiashara".

Wafanyabiashara wengi wanafungwa fikra na midomo ndani ya nchi hii kwa kuogopa hila na ghiliba za watawala.

Ni heri kufa masikini nikiwa nimesimamia ukweli, kuliko kuishi tajiri niliyetawaliwa na ubinafsi, woga, hofu na ubatili.

Natambua kuna jitihada za kutumia kila silaha na kila hila dhidi yetu katika Kipindi hiki.

Mwisho, Natoa rai kwa wanachama na wapenzi wa Haki katika Taifa hili, wasiogope. Haki itaweza kucheleweshwa kwa muda tu, lakini kamwe haiwezi kuzuiwa. Binadamu akikufungia mlango Mungu wa Haki atakufungulia dirisha.

Ubatili ni wa mpito lakini Haki ni ya milele.

Imetolewa

Leo Jumatano Agosti 31st 2016 Na:

Freeman Aikaeli Mbowe
Mfanyabiashara.

Time will tell who is squeaking the truth!
 
Ben Saanane: Kama watu wameficha fedha majumbani, TRA wanapata wapi makusanyo mnayodai yameongezeka?
Ombi: Rais Magufuli tumia zile Push-Ups ulizotuaminisha kuwa ndio kipimo cha Uongozi Shupavu badala ya kusingizia kwa vilio vya Lawama kuwa kuna watu wanaficha fedha ndio maana hali mbaya ya uchumi ili Uonewe huruma. Kama ulivyoonesha ushujaa kwenye Sakata la Sukari ,basi onesha Uhodari tena kwa hili la Walioficha fedha. Waagize wakuu wa mikoa na Wilaya kama akina Makonda waanze msako wa nyumba kwa nyumba kutafuta Maburungutu ya fedha zilizofichwa kama walivyofanya kwenye Sukari.Onesha Uimara na Ushupavu wako kama ulivyoonesha kwenye Kampeni Mzee Wetu. Vinginevyo isijekuwa Zile Pushups za kipindi kile zililenga kuwapumbaza watu wasiokuwa waelewa kama wale Raia walioishukuru kwa dhati kabisa serikali yako ya awamu ya Tano jana kwa kupeleka Tukio (Wao walisema Tamasha) la kupatwa na Jua Kule Mbarali jana.Wao waliamini ni wewe ulifanikisha kupatwa kwa Jua jana.Ona ulivyowajengea watu imani kwa Zile Push-ups Vilevile niandike kidogo tu kuhusu hili suala la kuficha fedha.Nimeshatahadharisha mara nyingi tu juu ya hatari ya kutoa matamshi ambayo sio taaluma au fani uliyobobea. Kwa mfano kwa mwanauchumi yeyote aliyesoma vizuri hawezi kuamini kuwa kuna fedha nyingi kiasi hicho ambazo zimefichwa hadi utoe uamuzi kuwa utachapisha noti mpya ili zilizofichwa ziwe karatasi tu Huku ni kutafuta kisingizio na kutafuta kuonewa huruma tu kwa ugumu wa maisha Niliwahi kusema kwa uchumi kama wa Tanzania ambako sekta binafsi bado haijatengamaa basi serikali ndio inapaswa kusisimua(Stimulate) uchumi kwa matumizi(Government expenditure). Serikali ndio iliyokua Consumer(Mlaji) wa huduma na bidhaa .Mfano mahotelini vikao vilikua vikifanyika.Kukawa na mzunguko wa fedha. Pia kwa sasa wawekezaji wanasita kuwekeza kwa sababu serikali ya awamu ya Tano haitabiriki na wawekezaji wengi hasa wenye asili ya kiasia(Wahindi) mara nyingi wapo makini kuwekeza.Niliwahi kuonya kwenye makala niliyomjibu Mwanahabari na Mchambuzi maahiri Godfrey Dilunga kuwa "Hatuhitaji Udikteta Kufikia Estada Novo(Taifa Jipya) " kwani serikali zinazofanya maamuzi ya kiimla hazitabiriki na hivyo wawekezaji husita kuwekeza Serikali inapotia pua yake kwenye kila biashara na kodi zisizotabirika inawafanya wawekezaji wa aina hii kuondoa fedha zao benki.Utawala wa awamu ya Tano unajua kukamua badala ya kutengeneza mazingira ya ukamuaji endelevu.Wao wanasimamia tax quantity badala ya Quality in terms of Efficiency Kauli ya Rais kuna walioficha fedha ni njia ya kutangaza hali ya uchumi ni ngumu lakini akataka kujinasua hapohapo kwa kusingizia watu. Anakwepa wajibu wake. Tuseme kuna watu walificha fedha tangu Novemba alipoingia madarakani ,hadi sasa karibia mwaka mzima si watakua wamezibadili ? Na wakizibadili zikawa kwa Dola ambayo ni stable currency and Internationally accepted si bado hizo shilingi zitakua kwenye mzunguko? Kwenye Uchumi kuna kitu kinaitwa Money Supply(MS) yaani Ugavi wa Fedha na kuna vizio M1, M2,M3 M1 ina kanuni zake yaani M1 Unazungumzia CC+DD CC ni Currency In Circulation(Fedha zilizopo kwenye Mzunguko + Demand Deposit(Amana) Sasa Rais Alizungumzia fedha imepungua kwenye Mzunguko na hivyo inahitajika ili mabenki yashushe Riba kisha Uwekezaji Uongezeke Kazi ya Benki ni kusisimua uchumi na inaitwa Financial Intermediary(Yaani Taasisi ya Kati kifedha) ambapo hupokea pesa za watu wanaoweka akiba/amana na benki wao hukopesha kwa watu Huwa benki wanawekewa kiwango na Benki Kuu.Benki kuu hutumia hizi benki za biashara kisheria na kikanuni katika kupunguza fedha mikononi mwa watu au kuongeza na hivyohivyo kudhibiti mfumuko wa bei Kukiwa na fedha nyingi mitaani Benki kuu hupandisha Riba inayowalazimu benki ya Biashara kupandisha riba na masharti magumu zaidi unapoenda kukopa na kinyume chake Sasa Rais anajua Gavana ndie alipaswa kuliongelea hili kitaalamu zaidi Hili la kuchapisha Noti mpya lingekuja ikiwa kuna noti bandia nyingi.Tena inakuja kama last resort. Rais angejihangaisha na washauri wake kuangalia kuwa Tanzania ni mojawapo wa vinara wa Mobile Banking Hapa Afrika kwa mzunguko mwingi kupitia Simu za Mikononi kama M-Pesa na Tigo Pesa Pia Rais alipaswa ku-address kwanza tatizo kubwa tulilo nalo hasa udhibiti wa Uwekezaji kwenye ardhi na Majengo(Real Estates Regulation) Watakatishaji fedha (Money Launders)wote hodari hutakatisha fedha kwa kutumia Real Estates Badala ya Kuweka fedha nyumbani hununua majengo .Angejiuliza ni kwanini bei za majumba zimepanda kwa kasi ya kutisha? Lakini hata kama walinunua bado fedha zingekua kwenye mzunguko Kuchapa fedha ni gharama. Mbinu hizi za kuchapa fedha mpya ziliwahi kwenda out of control mwaka 1920 kule Ujerumani na kusababisha Mfumuko wa Kutisha Dikteta Idd Amini alipoona uchumi mbaya aliamuru fedha zichapishwe.Yaani it was crazy Mugabe nae hapo Zimbabwe hivi majuzi Mbinu ya Rais kutishia kuchapisha fedha ni kutaka kutumia mwanya huo kuchapisha fedha kuongeza kwenye mzunguko badala ya anachotaka kuaminisha kuwa anafanya replacement ya fedha zilizofichwa Uchapishaji huo ni hatari zaidi kwa uchumi Inaweza kupelekea kukawa na fedha nyingi kwenye mzunguko hivyo kusababisha uhaba wa bidhaa na huduma kulingana na idadi kubwa ya fedha zilizopo mitaani(Too much money chasing few products) na pia ununuzi wa bond za Serikali kusababisha kupanda bei katika masoko ya fedha kimataifa na hivyo kushusha thamani ya sarafu yetu zaidi na nchi yetu hii "Tanzania Ya Magufuli ya Viwanda" ikazidi kuwa hatari Rais amuagize Gavana,Washauri wake wa Uchumi na wadau wengine waangalie mfumo wetu wa Kodi,Real Estates na Banking System katika kuleta harmonization katika ujenzi wa Uchumi na piakupambana na ufisadi Uchumi wa nchi huendeshwa kwa principles za kiuchumi na sio presidential decrees kama zile za akina Idd Amin,Mugabe hivi majuzi na Weimer kule Ujerumani ya 1920 Hatutaki kununua mchicha sokoni tukajikuta tunafunga safari na viroba vya Fedha kama Ujerumani na zimbabwe Vinginevyo ule ufanisi wa Pushups kwenye sukari unaweza kuzaa matunda hapa labda Sijui leo Huko Pemba atatoa lipi jipya tena maana kila aongeapo huzua mtafaruku.Usishangae akajisahu na kujisifu TRA wamevuka malengo ya kukusanya kodi.Ina maana hela zinatoka wapi? Sitarajii Waziri au Gavana aibuke na kudai Rais alikua anatania kuwa atachapa fedha mpya ndani ya Siku mbili wakati anajua kuna process ndefu . Ni Mwendo wa Kufyatua Watoto,Kufyatua Maneno na kisha kufyatua fedha na kisha .... Asisahau kuwakumbusha Wazanzibari kuwa yeye kaenda tuu huko kwao ambako hana mamlaka nako maana kuna tume yake na Rais Wake... Aluta Continua,Victory Ascerta.... Ben Saanane
https://www.jamiiforums.com/index.php?posts/17450347/
Sarcastic or realistic?
 
RAiSI KUBADILI NOTI SIO SUlUHU
Mnamo hapo jana MH.JP Magufuli alitishia
kubadili noti ili kuwakomesha wale waliozificha
lengo ni kuwataka waweke fedha benki ili ziingie
kwenye mzunguko. Kisiasa ni rahisi sana kufanya
hivyo ila ni kiuchumi ni vigumu sana kufanya
hivyo.
Kumbukumbu zinaonyesha ili fedha ipotee
kwenye mzunguko inachukua zaidi ya miaka
mitano na kuendelea which means hata Noti
zikibadilishwa leo bado wale waliozificha
wataendelea kuzitumia mpaka Mwaka 2021 kwa
mantiki hiyo tatizo la upotevu wa fedha kwenye
Taasisi mbalimbali za kifedha halitatatuliwa
kirahisi.
Fedha kwenye mashirika ya fedha ipotelea wapi?
Mojawapo ya maswali magumu ambayo
watanzania wengi wameshindwa kuyaelewa kwa
kina ni wapi fedha imepotelea.
1.Ongezeko la kodi kwenye miamala ya fedha
(increase in transaction cost). Serikali
ilipotangaza ongezeko la kodi ya ongezeko la
thamani (VAT) iliwaathiri moja kwa moja
watumiaji wa sarafu ya shilingi. Mfano rahisi
Asilimia 18 ilioongezwa kwenye bei ya kufanyia
miamala ilipunguza kwa kiasi kikubwa Bank
deposits za watu kitu kilichopelekea pesa nyingi
kurudi mikononi mwa watu na benki nyingi
kukosa pesa kwa ajili ya kufanya shughuli za
kifedha nchini. Hapo utaona aienufaika ni TRA
kwani mapato yameongezeka kwa asilimia 18 ya
kila muamala anaofanya mtu mmoja.
2.Ongezeko la bei za vitu muhimu kama sukari.
Ugumu mwingine uliosababisha fedha ipungue
benki na kurudi mikononi mwa watu imechangiwa
kwa kiasi kikubwa na kuongezeka kiholela kwa
bei ya sukari which means sukari iliokua inauzwa
sh.2000 ilipanda hadi Zaidi ya shilingi
2700,matokeo yake kiuchumi Ilipunguza kwa kiasi
kikubwa pesa mikononi mwa watu kwa zaidi ya
asilimia 40 na kupelekea pesa benki kupungua
kwa asilimia zaidi ya 40 kwa kila kilo ya sukari
ilionunuliwa.
3. Serikali kubana matumizi(Reduction in
government expenditure). Hapa napo tulifeli kwa
kiwango kikubwa serikali ilibana matumizi
yaliosadikiwa sio ya lazimaa,hapa napo pesa
badala ya kwenda kwenye mikono ya watu wengi
iliishia kwenye mkono mmoja wa serikali hivyo
kupunguza kiwango kikubwa cha pesa kwenye
mzunguko
4.Kodi kubwa na mizigo kwenye sekta ya utalii
na bandarini. Mwezi uliopita iliripotiwa kua
Magari kwenye bandari ya Dar es salaam
yamepungua kutoka magari 3000 hadi magari
1500 kwa siku moja,na hii ilisababishwa kwa
kiasi kubwa na ongezeko la kodi huku serikali
ikidhamiria kukusanya mapato mengi ndani ya
muda mfupi.Hapo tulifeli kwa kiasi kikubwa kwani
tunazungukwa na nchi washindani wenye bandari
kubwa kuliko yetu kwa Mfano Msumbiji na
kenya.Wafanya biashara wengi wamekimbilia
huko kwa hofu ya kupata hasara,madhara yake ni
watu wengi kukosa ajira na hivyo kupelekea
kukosekana kwa ujira ambao ungeweza kuongeza
pesa kwenye mzunguko.
Nini kifanyike sasa?
Ni dhambi kubwa kuwakomoa watu waliojiwekea
fedha walizotafuta kwa jasho lao wenyewe na
hata sarafu ikibadilika bado hawataweza
kuathirika moja kwa moja. Serikali ingejitahidi
kuongeza idadi ya pesa nyingi kwenye mzunguko
kwa kutumia benki kuu ya Tanzania. Hapa Benki
kuu inatakiwa kununua bonds kutoka kwa watu
binafsi na mashirika ya watu binafsi ili ku
dispense more amount kwenye mzunguko, pili
kodi zisizo za msingi zipunguzwe ili
kuwashawishi watu waendelee kutumia mashirika
ya kifedha. Benki ni kama mfanyabiashara tu
ambae yupo pale kwa ajiri ya kujipatia faida sasa
ukiongeza kodi ina maanisha mtu wa mwisho au
benki yenyew inaweza kubeba mzigo mzito
ambao ni vigumu kuutua na utaangukia uchumi
wa nchi nzima (Macroeconomics)
Owen j chimela

Money circulation is affected mostly by the cost of doing business which in turn is shaped by taxation environment, predictability of government policies, security, productivity, profitability and non tariff barriers among others.

In all these parameters we are lagging behind so changing currencies will not interfere with these hurdles but may even worsen them.
 
[emoji144][emoji144][emoji144][emoji144]


[emoji69] Rais J.P
Magufuli
Unguja Leo: 03/09/2016

[emoji115][emoji15] "Dkt. Shein ana moyo wa tofauti sana.

[emoji125]Yeye alipata ushindi 92% lakini ameteua wapinzani kuingia katika serikali yake.

Mimi nilipata 58% lakini hakuna hata mmoja aliyeingia na hatakaa aingie.

-Dr. Shein ni mpole sana... [emoji35]Mimi nitoe mkono wangu, uukatae halafu eti kesho nisaini makaratasi yako...? Si rahisi sana!" [emoji35]


⚖⚖⚖⚖⚖

Anaandika Rashid Chilumba mwanachama mtiifu wa CCM.

⚖ Matamshi aliyoyatoa Ndugu [emoji69] Rais leo hapa Unguja sikuyatarajia yatoke kwenye kinywa cha mkuu wa nchi, Haya yanamwagia mafuta kwenye moto.[emoji108]

Suala kama la pensheni au matibabu ya mtu aliyewahi kuwa Kiongozi ni la kisheria siyo hiyari ya mtu, Yaan hata umfumanie na mkeo Sheria inakutaka usaini na apewe. Mengine mmalizane wenyewe.

[emoji12]Na kwa kuwa Tumesema siasa zimeisha Basi tujitahidi kuzimaliza kweli, sare za vyama, vijembe na maneno ya ngebe kwenye mikutano ya serikali inawagawa raia. [emoji120]

[emoji117]Siku zijazo wasio wana CCM wanaweza kuacha kuhudhuria mikutano ya Kiongozi mkuu wa nchi kwa sababu wanajihisi wanyonge na wakiwa.

[emoji108]Tuzungumze Maendeleo, kufanya kazi na kubadili maisha yetu, hawa Wakosoaji na wapinzani watakuwepo daima, kuwashambulia katika jukwaa lililolipiwa kodi na watu wote ikiwemo wao si jambo la kiungwana.

[emoji144]Msema kweli ni mpenzi wa Mungu, Hotuba za Ndugu Rais katika ziara yake visiwani hazijanivutia wala kusisimua. [emoji174]Zimeiacha Zanzibar katika mtafaruku ule ule au mkubwa zaidi.


[emoji144][emoji144][emoji144][emoji144][emoji144]

Words are furnaces of fire depending on how they are used.

Wisely used, words heal but badly used can lead to bad things happening despite good intentions.

Polarizing and alienating others is the epitome of irresponsibility.
 
https://www.jamiiforums.com/index.php?posts/17478331

I said early that cannibalism is running our economy to a grinding halt.

How do you explain locking out east Africans here and expect to succeed?

Regional cooperation removes technological, labour and economical constraints but we have dinosaurs thinking leaders who are backward looking but still expecting to move this nation forward with Chinese fragments and western morsels!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom