Tatizo hapa sio mada wala mtoa mada. yeye kajielezea anavyojisikia yeye wewe either muunge au usimuunge na utetee hoja yako sio kumwambia amekosea hajakosea chochote. hakuna mwanamke asiependa kutongozwa katu nakataa jamani
saa nyingine tuwe tunaongea na ukweli.mimi huwa napitia sana humu jamvini japo umember nimepata hv karibuni na kuna watu wamejiunga humu nawaona mpaka leo hii wanajiona wametawala hili jamvi.kwa hiyo wamezoeana mmoja akitoa mada wote wanajitia kumsaport.
tuwe wakweli na tuheshimu hoja ya kila mmoja msiangalie nani katoa na kwa nini. tatizo lenu mnakutana mshajuana so kila mdada hapa anajitia ana tabia nzuri anakunja makucha yake asionekane mbaya mbele ya jamii.
Bila mtu kusema anachojisikia nyie mngejuaje kwa hiyo mkubali kwenye jamii kuna kila mtu na kila mtu ana feelings zake jao wengine kujishaua ooo hatutaki kuolewa oooo hatutaki kutongozwa ooo sijui nini.
ndio hawa wanaolewa badae wanatoa makucha wanaume wanawakimbia.
msijiite tu ma great thinker, GT anaangalia strength and weakness na mengine kama hayo
ahsanteni, naomba kuwakilisha
Matokeo ya madhara ya fikra hasi katika kuiangusha na kuivuruga jamii na kuharibu usalama wa kimaadili ni makubwa mno siku hizi, na hayawezi kukataliwa kwa kadiri kwamba hata wale wasiomini dini yoyote hawawezi kukataa ukweli huu. Tukikubali kuruhusu fikra hasi na kuziwacha zitie fora, basi mahusiano na mifungamano ya watu hukatika, na kupelekea hitilafu, utengano na migogoro katika mfumo mzima wa familia na jamii kwa ujumla.
Vitendo na mawazo yetu mwisho wake hufunga ukurasa wa kutojitambua na kuona kuwa tuna haki ya kuithiri jamii kwa mawazo na matendo yetu hasi. Tukichungua kidogo maisha yetu, na wale wanao tuzunguka tunaweza kuona mateso yaliotokana na tabia na vitendo vyetu, tutapata ibra kubwa sana!
Dunia kama njia, kila siku kupitia, Mfano kama njozi, kwenye huo usingizi, kila mtu anaota vile fikra zake zinapo mpeleka.
Naam; watu wanaofikiri kwamba dunia ni medani ya mashindano ya kuishi, kujionesha kuwa wao ni mahodari wa fikra zao na matendo yao machafu. Vilevile hawasiti hata kidogo katika kutetea vitendo vinavyokwenda kinyume na maadili ya ubinadamu.
Kwa bahati mbaya, leo hii tabia na matendo machafu yametia fora katika jamii. Ndimi za moto wa ubalakala zinachoma mavuno ya maisha ya jamii, na zinahatarisha kuziangusha nguzo za ustaarabu wa wanadamu. Watetezi wa maadili potofu wanavuruga haki za jamii ya wanadamu kwa kadiri ya uwezo na nguvu zao. Huwalenga watu wasio na ulinzi hasa watoto wa shule na kuwapoteza kimaadili bila ya kujali kitu.
Uku wakiwahakikishia furaha ya muda mchache, lakini bila kuanisha hasara na kilio cha kudumu, maishani mwao.
Kitu cha pekee kinachoonekana katika jamii hiyo ni sanamu isiyo na roho ya malaika wa uadilifu.
Nafsi ya mtu ni kama mvuke unaopanda daima. Shabaha ya malezi ni kuyafanya matatizo ya nje yachukue sura ya tabia, fikra na hisia za upendo katika akili mmoja wetu. Uadilifu na tabia njema haupatikani kwa kupiga, kudekeza, kutesa wala kufikiri. Tabia njema na uadilifu ni dhana ambayo tujaribu kuitia katika fikra na tabia zetu kidogokidogo. Malezi sahihi ya kiadilifu hupatikana tunapochanganyika na wengine.
Ajabu ni kuwa watu wengi huacha tabia na matendo adilifu na kupapia mila na tamaduni za wale ambao tunaona kuwa wameendelea. Mimi siamini kwamba hisia ya uadilifu ni ya kimaumbile, lakini ninapoona jinsi uadilifu ulivyokua kwa wazazi wetu, nashangaa tabia zile zimepotelea wapi?
Bila shaka ni hali hii ya kushiriki mabaraza ya kwenye mitandao, na kuona kuwa ndio kungwi wetu na walimu wetu wa kutuelekeza nini cha kufanya, na kutupilia mbali mila na tamaduni zetu na kuziona kuwa zimepitwa na wakati.
Basi chonde chonde nyie makungwi na walimu wa mitandaoni, muwe waangalifu yasije mapenzi yenu yakaharibu matendo na tabia za wasomaji wenu kwani furaha yenu inaweza kuwa kilio cha uchungu kwa wale wenye kuwasoma na kuyachukuwa bila ya kuyachuja, yale mnayo yaweka kwenye mabaraza ya kwenye mitandao yenu.
kutojijua mwenyewe falsafa-binafsi