Wikileaks yajibu kitendawili cha kwanini Muammar Gaddafi aling'olewa madarakadi na hatimae kuuawa

Wikileaks yajibu kitendawili cha kwanini Muammar Gaddafi aling'olewa madarakadi na hatimae kuuawa

USSR Na US walipokuwa wanapiganisha vita Angola uliona kuna Mrusi Au Mmarekani?

Ukijifunza Imperialism technique and technics kwenye Invasion maeneo yenye resources utaelewa!
Nacho muelewa Zitto junior ni kwamba hapingi wazungu ndio walio mtoa ila anasema kuna sehemu ya wananchi (hata kama ni ndogo) walikuwa hawamtaki Gardaffi. Situation ikisha kuwa hivyo ni rahisi hata watu wa nje kutumia huo upenyo kufanya na ya kwao hasa sehemu ambayo ina rasilimali wanazo zitaka. Kwa hiyo kabla ya kutupa lawama kwa hayo mataifa makubwa kuwa ndio wasababishi lakini tukiangalia chanzo kabisa unakuta kinaanzia ndani ya nchi. Ila kama nchi ndogo zitaweza kutatua matatizo yao kwa kukaa kuzungumza (wenyewe kwa wenyewe, ndani ya nchi) nadhani kuna baadhi ya mianya ya watu wa nje kupandikiza watu wao tutaipunguza kama sio kuiziba kabisa.
 
Lakini bado Angola nako kulikuwa na strife kwahiyo kuomba support ya kivita kwa waasi au serikali ilikuwa haiepukiki kwa pande zote

Nachokataa ni watu kuaminishwa humu kuwa watu wadhalimu hutolewa na wazungu na sio kwamba wananchi wamewachoka !! Mfano savimbi alikuwa na support ya nusu ya wananchi wa angola sasa unaanzaje kusema wazungu ndio walivuruga angola wakati vita ilianzwa mapema na savimbi mwenyewe kwa uroho wa madaraka!!

Ambacho mnatakiwa mseme ni kwamba wazungu wanapenda kuingilia VITA kma syria kwa ajili ya maslahi yao binafsi ila sio kuwawekea lawama hata pale wananchi wakionyesha kumkataa huyo kiongozi.

Rais wa Tunisia aliondolewa Kwa Mass uprising lakin Ghadafi na Assad wa Syria ile Sio Mass uprising ni Waasi wenye Silaha ndio walimuangusha

NATO ilikuwa inatangulia mbele na kushambulia Kambi na Maghala ya Silaha ya Ghadafi ili kumdhoofisha!

Baada ya kuondolewa Rais WA Tunisia bado Tunisia ilitawalika Kwa kuwa aliondolewa na Raia lakin Libya Mpaka Leo haitawaliki Kwa Kuwa Waasi waliomtoa Ghadafi hawakuwa Na Makubaliano ya namna ya kuitawala Libya baada ya Ghadafi
 
Nacho muelewa Zitto junior ni kwamba hapingi wazungu ndio walio mtoa ila anasema kuna sehemu ya wananchi (hata kama ni ndogo) walikuwa hawamtaki Gardaffi. Situation ikisha kuwa hivyo ni rahisi hata watu wa nje kutumia huo upenyo kufanya na ya kwao hasa sehemu ambayo ina rasilimali wanazo zitaka. Kwa hiyo kabla ya kutupa lawama kwa hayo mataifa makubwa kuwa ndio wasababishi lakini tukiangalia chanzo kabisa unakuta kinaanzia ndani ya nchi. Ila kama nchi ndogo zitaweza kutatua matatizo yao kwa kukaa kuzungumza (wenyewe kwa wenyewe, ndani ya nchi) nadhani kuna baadhi ya mianya ya watu wa nje kupandikiza watu wao tutaipunguza kama sio kuiziba kabisa.
Mkuu johnmweusi naona umenielewa vyema kabisa great thinker
 
Tatizo mkuu sisi watu weusi wengi wetu ni njaaa tu mtu akipewa maslahi mazuri yupo tayari kusaliti nchi yake, watu wake , jamii yake hata dini yake.

Kuna watu wengi ambao ni wafuasi wa nchi za magharibi mfano mzuri ni Dr shika tangu aondoke nyumbani kwao hajawahi kurudi kisa ni CIA wa marekani .

Hawa tunaowengi sana ndani ya nchi zetu , wao wakiona inshu wanafanya mobilization ya jamii husika, mataifa ya juu yanatoa pesa za kutosha , wanafanya underground mass movement kisha mnavaana ninyi wenyewe harafu kwa maslahi yao wwnashuka na kujifanya kusaidia wapi na wapi?

Nakubali kuwa Libya ilivamia na mataifa ya magharibi kwa manufaa yao na walitumiwa watu wao kukamilisha azma yao, wakafanya mobilization na wakafanikiwa
 
Nacho muelewa Zitto junior ni kwamba hapingi wazungu ndio walio mtoa ila anasema kuna sehemu ya wananchi (hata kama ni ndogo) walikuwa hawamtaki Gardaffi. Situation ikisha kuwa hivyo ni rahisi hata watu wa nje kutumia huo upenyo kufanya na ya kwao hasa sehemu ambayo ina rasilimali wanazo zitaka. Kwa hiyo kabla ya kutupa lawama kwa hayo mataifa makubwa kuwa ndio wasababishi lakini tukiangalia chanzo kabisa unakuta kinaanzia ndani ya nchi. Ila kama nchi ndogo zitaweza kutatua matatizo yao kwa kukaa kuzungumza (wenyewe kwa wenyewe, ndani ya nchi) nadhani kuna baadhi ya mianya ya watu wa nje kupandikiza watu wao tutaipunguza kama sio kuiziba kabisa.

Ni kweli. Tukikaa tukaya maliza matatzo yetu wenyewe tutapunguza kuchonganishwa. Lakini hii ni ngumu ajabu. Viongozi wenyewe mara ingine wanakuwa wa kupandikizwa. Watu wa ovyo ovyo tu mnashitukia ndio wapo katika nafasi ya kuwaongoza. Hao wanawezeshwa waweze kushika nafasi na wanalindwa mwanzo mwisho

Mwisho tunakuwa katika nafasi ya kupata vichwa maji kwenye ikulu za Africa.

Katika nchi yoyote hamuwez kukosa wa kulalamikia serikali. Hata marekan na ufaransa watu huandamana. Sasa hao waandamanaji wakiwezeshwa unategemea nini? Uchina kwenyewe watu huandamana na kujichoma moto. Hao wakiwezeshwa itakuwaje.

Ilichofanya ulaya na marekani kumdungua Gaddafi ni ushetani
 
Fact. Nilishangaa sana kipindi kile mpakaMugabe aawatusi wazungu lakini hawakuwa na muda wa kumuondoa kumbe Mugabe hakuwa na G.O.D
 
Ni kweli. Tukikaa tukaya maliza matatzo yetu wenyewe tutapunguza kuchonganishwa. Lakini hii ni ngumu ajabu. Viongozi wenyewe mara ingine wanakuwa wa kupandikizwa. Watu wa ovyo ovyo tu mnashitukia ndio wapo katika nafasi ya kuwaongoza. Hao wanawezeshwa waweze kushika nafasi na wanalindwa mwanzo mwisho

Mwisho tunakuwa katika nafasi ya kupata vichwa maji kwenye ikulu za Africa.

Katika nchi yoyote hamuwez kukosa wa kulalamikia serikali. Hata marekan na ufaransa watu huandamana. Sasa hao waandamanaji wakiwezeshwa unategemea nini? Uchina kwenyewe watu huandamana na kujichoma moto. Hao wakiwezeshwa itakuwaje.

Ilichofanya ulaya na marekani kumdungua Gaddafi ni ushetani
Unacho kisema ni kweli. Ila sasa kama hatutaweza kumaliza changamoto zetu mwenyewe basi tutegemee kufanyiwa maamuzi yote ya wazungu na tusilalamike maana litakuwa ni kosa letu wenyewe.

Kuhusu viongozi kupandikizwa hili nalo ni janga KUBWA japo wapo na ambao hawajapandikizwa ila akili zao fupiii.

Kiujumla matatizo Mengi ya wa Afrika yanaletwa na sisi wenyewe na wa kututoa hapa ni sisi wenyewe.
 
Kikubwa kilicho mponza gadaf ni kuutangazia ulimwengu, bara la africa linataka liungane na liwe linatumia sarafu moja na kuwe na Bank of Africa, yaani Africa isiwe inaitengemea tena WB

Baada ya hapo Africa ijitoe Federal Reserve System, Ukifanikiwa kujitoa kwenye huo mfumo ni sawa na kutangaza umejitenga na dunia, nchi ambazo hazipo kwenye huo mfumo ni N.Korea, Iran na Cuba

Gadaf angeifikisha Africa mbali sana kama siyo unafiki wa mtu mweusi, na nguvu walio kuwa nao wazungu ya propaganda...

Raia wa libya walikuwa na luxury life eti wanahaidiwa maisha mazuri mengine tena huu ni uzuzu, Gadaf alikuwa tishio kwa western country

Nasema wacha libya wachapane hadi waishe wote
 
Unacho kisema ni kweli. Ila sasa kama hatutaweza kumaliza changamoto zetu mwenyewe basi tutegemee kufanyiwa maamuzi yote ya wazungu na tusilalamike maana litakuwa ni kosa letu wenyewe.

Kuhusu viongozi kupandikizwa hili nalo ni janga KUBWA japo wapo na ambao hawajapandikizwa ila akili zao fupiii.

Kiujumla matatizo Mengi ya wa Afrika yanaletwa na sisi wenyewe na wa kututoa hapa ni sisi wenyewe.

Kweli mkuu. Wakututoa hapa ni sisi wenyewe. Lakin haitokaa itokee sisi wote katika nchi tuwe na akili zinazofanana. Kutakuwa na vibaraka tu. Hebu kumbuka kipindi cha Patrice lumumba. Alikuwa mzur lakin alikuwa kikwazo kwa wazungu. Wakampoteza na kumuweka mobutu. Walimlinda mpaka akafa kifo cha Mungu.

Angalia Libya majuz kati. Gaddafi Kaja na akili ya kututoa wakasaidia atolewe.

Kote Kongo na Libya ndo nyota ya kuendelea kwa afrika, ni ukwasi na utajiri wa afrika. Li Kongo lingekuwa vizuri lingeambukiza maendeleo kwa majiran zake.

Hizo ni hujuma mbili za wazi kabisa. Vipi kuhusu hujuma zingine tufanyiwazo ambazo hatutokaa tuzijue?
 
Kweli mkuu. Wakututoa hapa ni sisi wenyewe. Lakin haitokaa itokee sisi wote katika nchi tuwe na akili zinazofanana. Kutakuwa na vibaraka tu. Hebu kumbuka kipindi cha Patrice lumumba. Alikuwa mzur lakin alikuwa kikwazo kwa wazungu. Wakampoteza na kumuweka mobutu. Walimlinda mpaka akafa kifo cha Mungu.

Angalia Libya majuz kati. Gaddafi Kaja na akili ya kututoa wakasaidia atolewe.

Kote Kongo na Libya ndo nyota ya kuendelea kwa afrika, ni ukwasi na utajiri wa afrika. Li Kongo lingekuwa vizuri lingeambukiza maendeleo kwa majiran zake.

Hizo ni hujuma mbili za wazi kabisa. Vipi kuhusu hujuma zingine tufanyiwazo ambazo hatutokaa tuzijue?
Kwa hiyo Mkuu hapo ndio kusema kuwa Waafrika hatuwezi kutoka kwenye tope tulilozama auu kuna njia gani tufanye ili tutoke tulipo ??
 
Kwa hiyo Mkuu hapo ndio kusema kuwa Waafrika hatuwezi kutoka kwenye tope tulilozama auu kuna njia gani tufanye ili tutoke tulipo ??

Kutoka naona tunaweza mkuu, japo mimi sio mtaalam wa mambo yenyewe

Wazungu wako mbele Kwasababu wametuzidi maarifa au teknolojia. Kwa kutumia mauchawi hayo wanatengeneza vitu na kutuuzia kwa bei watakapo wao. Unaweza kuta maligafi wanaiba kwetu. Kwa hili laiti bei za maligafi na final product zingewiana wasinge tuacha mbali kihivyo. Lakini, mfano wanaiba coltan Kongo na kutengeneza simu halafu bei wanatupangia na sisi tunahitaji simu. Inakula zaidi kwetu

Uarabuni wako mbele sababu ya mafuta. Naona kwa kiasi kikubwa wamedhibiti mali asili yao. Inawanufaisha. Nasisi tungekuwa na utajiri wa madini kama Kongo halafu tukahakikisha tunafaidika nayo tungekuwa mbali.

So, naona ni teknolojia na maliasili ambayo kwingineko inahitajika sana

Kwa Teknolojia ni ngumu. Kufanya kama wachina wanaosifika kwa kuibia wazungu teknolojia zao ni ngumu kujipanga, mfano tu. Lakini linawezekana


Tangia kipindi cha mkapa kama tungejipanga vizuri katika ubinafsishaji na uchimbaji wa madini uliokuwa unafanywa na wageni naona hali zetu zingekuwa bora zaidi. Na hili ni pamoja na kuwa na mipango bora na kuwa na vipaumbele vizuri

Kutoka tunaweza. Lakini ni vita kali. Kenya wasingependa tuwe na viwanda vya blueband ili tuendelee kuwa mateja wao, mfano tu. Kuna watu wangependa waje wamhonge rais na wasaidizi wake ili wachimbe bure dhahabu na nk. Sasa hela za kujengea barabara na kununulia vifaa vya shule zitatoka wapi?
 
Kwa hiyo Mkuu hapo ndio kusema kuwa Waafrika hatuwezi kutoka kwenye tope tulilozama auu kuna njia gani tufanye ili tutoke tulipo ??

Kutoka naona tunaweza mkuu, japo mimi sio mtaalam wa mambo yenyewe

Wazungu wako mbele Kwasababu wametuzidi maarifa au teknolojia. Kwa kutumia mauchawi hayo wanatengeneza vitu na kutuuzia kwa bei watakapo wao. Unaweza kuta maligafi wanaiba kwetu. Kwa hili laiti bei za maligafi na final product zingewiana wasinge tuacha mbali kihivyo. Lakini, mfano wanaiba coltan Kongo na kutengeneza simu halafu bei wanatupangia na sisi tunahitaji simu. Inakula zaidi kwetu

Uarabuni wako mbele sababu ya mafuta. Naona kwa kiasi kikubwa wamedhibiti mali asili yao. Inawanufaisha. Nasisi tungekuwa na utajiri wa madini kama Kongo halafu tukahakikisha tunafaidika nayo tungekuwa mbali.

So, naona ni teknolojia na maliasili ambayo kwingineko inahitajika sana

Kwa Teknolojia ni ngumu. Kufanya kama wachina wanaosifika kwa kuibia wazungu teknolojia zao ni ngumu kujipanga, mfano tu. Lakini linawezekana


Tangia kipindi cha mkapa kama tungejipanga vizuri katika ubinafsishaji na uchimbaji wa madini uliokuwa unafanywa na wageni naona hali zetu zingekuwa bora zaidi. Na hili ni pamoja na kuwa na mipango bora na kuwa na vipaumbele vizuri

Kutoka tunaweza. Lakini ni vita kali. Kenya wasingependa tuwe na viwanda vya blueband ili tuendelee kuwa mateja wao, mfano tu. Kuna watu wangependa waje wamhonge rais na wasaidizi wake ili wachimbe bure dhahabu na nk. Sasa hela za kujengea barabara na kununulia vifaa vya shule zitatoka wapi?
 
hivi malkia Elizabeth sio dictator?mbona katawala muda mrefu sana,naye atolewe?

waache kuingilia internal affairs za watu
 
Back
Top Bottom