TANZIA William Kusila (waziri wa zamani) afariki Dunia

TANZIA William Kusila (waziri wa zamani) afariki Dunia

theory of population and ageing nazipenda sana namba huwa hazidanganyi ishi utakavyoishi weka matozo unavyoweza waambie watakula nyasi waambie watalima kwa meno waite farasi na wewe ndo chama umeshika hatamu unawanyoosha waite raia wana akili za kawaida waambie asietaka tozo ahamie Burundi waite kichwa cha mwendawazimu wewe ni waziri kwamisha bwawa lao la umeme waambie raia wanaolala njaa kuwa hivi ni vijisenti tu sijui pesa ya mboga watukane raia unavyoweza ila uzee upo unakuja mdogo mdogo na vigogo wote tutaenda nao tu na mashangingi yao yale ambayo ni kodi za wanyonge watayaacha yamepaki uani!!
wakiifisadi nchi waacheni tu kaburi ndo kiboko ya kila mmoja wetu!! yatapukutika yote in 20 years Allahu Aaalam maana mengi maviongozi ni mazee vijana hawana ajira wala ofisi
Anazeeka akiwa na good life, anaacha kizazi chake kikiwa kwenye hali nzuri.
Hizi faraja ulizojipa hapa wala hazina maana yoyote.
 
Huyu ndio alifunguliwa makesi na mkapa
Sio yule alikuwa Nalaila Kyura (?)alikuwa waziri wa mawasiliano na mwenyeji wa Singida kuna wakati alikuwa na nguvu sana aliwahi hata kuwa waziri wa mambo ya ndani kama sijakosea na alitegemewaangekuwa kiranja mkuu wa nchi hii nasikia baadae alishinda kesi yake ,kutokana na masaibu yaliyomkuta akaokoka na baadae akashinda kesi na kulipwa mamilioni ambayo yaliishia kanisani kwa marehemu Dr mama wa kanisa la moto ,mwishowe akafariki akiwa mtu mwenye majonzi kwa vile alikimbiwa na wenzake wote
 
theory of population and ageing nazipenda sana namba huwa hazidanganyi ishi utakavyoishi weka matozo unavyoweza waambie watakula nyasi waambie watalima kwa meno waite farasi na wewe ndo chama umeshika hatamu unawanyoosha waite raia wana akili za kawaida waambie asietaka tozo ahamie Burundi waite kichwa cha mwendawazimu wewe ni waziri kwamisha bwawa lao la umeme waambie raia wanaolala njaa kuwa hivi ni vijisenti tu sijui pesa ya mboga watukane raia unavyoweza ila uzee upo unakuja mdogo mdogo na vigogo wote tutaenda nao tu na mashangingi yao yale ambayo ni kodi za wanyonge watayaacha yamepaki uani!!
wakiifisadi nchi waacheni tu kaburi ndo kiboko ya kila mmoja wetu!! yatapukutika yote in 20 years Allahu Aaalam maana mengi maviongozi ni mazee vijana hawana ajira wala ofisi
Umeandika Kwa hasira sana kiasi kwamba umeingiza feelings and emotions zaidi,but you touched the facts mkuu.
Kwa mtazamo wangu ni kuwa,hii dunia ya tatu au hizi nchi masikini Hawa wakubwa wanapata Mali Kwa ufisadi mwingi sana,sio Kwa ku crack mind zao na kuleta real solutions katika jamii zao.
Sasa kikawaida Kabisa Kama unakula bila jasho na jasho halitoki hiyo ni TOXIC.
Watu wengi hilo hawalijui,wewe angalia hata Dr,PhD holders wa nchi za kiafrika na hususani hapa nchini kwetu,wakipata nafasi tu ambazo ni nyeti ndani ya muda mfupi tu wanakuwa wa duara,wanakuwa shapeless wananenepa Ile mbaya bila Kujua hali hiyo ni magonjwa.
Kifupi lifestyle ya uchovu na uvivu ndio shida plus mindset ya ulafi ndio Kabisa.
Mtu anakuwa kiongozi lakini hata kuandika vitabu haandiki ili kuacha legacy utaachaje kukaribisha toxic kwenye mwili wako na mindset yako?
Mtu umepata Mali za kifisadi utaachaje kuwa mvivu Kwa sababu most of the things you do are shortcuts sio real solutions to the community.
Na wengi Kwa kuwa wanatoka familia fukara zaidi basi matokeo yake ndio hayo.
Nasema hivi sio kuwa hatufi,hapana wote tutakufa lakini Kuna tofauti kati ya mwenye nafasi kimaisha na asiye na nafasi kimaisha.
Kwa wenzetu specifically Japan,78 years ni umri wa kati tu.
Yule Shizo Abe waziri mkuu wa zamani aliyepigwa risasi just imagine mama yake mzazi yupo hai na yuko fresh tu.
Hiyo yote ni lifestyle Yao na mindset Yao Iko vizuri sana sio kama sisi kwenye jamiii yetu.
Sisi huku mtu anaweza akakaa na malaria bila kutibiwa hata mwezi na anaona ufahari tu kuwa yuko ngangari lakini Kwa undani Kabisa ni anajiua taratibu.
Mtu anakaa na njaa kutwa nzima na anaona sawa tu kama kaujanja Fulani hivi kumbe ndio unajiondoa taratibu.
Mtu ana sex mara nyingi zaidi ya anavyokula au zaidi ya protein input yake na anaona sawa tu.
Mtu anakunywa pombe na kula hovyo tena bila mazoezi anaona sawa tu.
Sasa hayo yote ujanani yanawezekana lakini huko uzeeni kuanzia miaka 45 na kuendelea shida zinaanza.
Ndio maana hizi nchi zetu ni kawaida sana watu kulamba Lolo kati ya miaka 50 na 70 hapa.
Kwa wenzetu sio rahisi Sana,hata Kwa baadhi ya jamii hapa hapa kwetu sio rahisi Sana kutokana na lifestyle na mindset zao.
Mfano jamii za wamasai Wanatoboa 95 plus hata jamii za watu wa kanda ya ziwa.
 
Huyu mzee hata taarifa za maziko yake hatukusikia ! hivi amezikwa au bado ?
 
Waziri wa zamani wa Uchukuzi William Kusila (78) amefariki dunia leo mchana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili .

Chanzo : Mwananchi
Wimbi na upepo Ule umeanza mdogo mdogo baada ya kupinduka mwaka!!!

Tusubiri!!!!
 
RIP Mwalimu Kusila.

Mtu huyu alinifundisha Physics Tabora School kabla hajaingia Usalama wa Taifa na baadaye kuwa mwanasiasa. Alikuwa anaijua Physics ndani na nje utadhani unafundishwa na Newton, Wheatstone, Ohm, Faraday, au Maxwell mwenyewe. Nelkon alikuwa hamfikii ingawa tulikuwa tunatumia vitabu vya Nelkon, Kusila alikuwa anaweza kusema kuwa Nelkon alikosea kidogo na ukilinganisha na Abott ndipo unaona wapi Kusila alikuwa sahihi kuliko Nelkon.

Physics aliyonifundisha ilinifanya niwe "injinia wa kuigwa." Pumzika salama mwalimu
 
RIP Mwalimu Kusila.

Mtu huyu alinifundisha Physics Tabora School kabla hajaingia Usalama wa Taifa na baadaye kuwa mwanasiasa. Alikuwa anaijua Physics ndani na nje utadhani unafundishwa na Newton, Wheatstone, Ohm, Faraday, au Maxwell mwenyewe. Physics aliyonifundisha ilinifanya niwe "injinia wa kuigwa." Pumzika salama mwalimu
Walimu wasiwe wanasiasa

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
 
Walimu wasiwe wanasiasa

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
Unasema ukweli 100% lakini hata hivyo ni lazima walipwe vizuri kama ambavyo wakati wa kikoloni walivyokuwa wanalipwa kiasi cha kazi ya ualimu kuwa inaheshimiwa sana. Leo hii waalimu wanakaa bila mishahara kwa miezi kadhaa wakati wanasiasa wanakula rundo la posho za vikao!
 
Unasema ukweli 100% lakini hata hivyo ni lazima walipwe vizuri kama ambavyo wakati wa kikoloni walivyokuwa wanalipwa kiasi cha kazi ya ualimu kuwa inaheshimiwa sana. Leo hii waalimu wanakaa bila mishahara kwa miezi kadhaa wakati wanasiasa wanakula rundo la posho za vikao!
@Mpwayungu Village

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
 
RIP Mwalimu Kusila.

Mtu huyu alinifundisha Physics Tabora School kabla hajaingia Usalama wa Taifa na baadaye kuwa mwanasiasa. Alikuwa anaijua Physics ndani na nje utadhani unafundishwa na Newton, Wheatstone, Ohm, Faraday, au Maxwell mwenyewe. Nelkon alikuwa hamfikii ingawa tulikuwa tunatumia vitabu vya Nelkon, Kusila alikuwa anaweza kusema kuwa Nelkon alikosea kidogo na ukilinganisha na Abott ndipo unaona wapi Kusila alikuwa sahihi kuliko Nelkon.

Physics aliyonifundisha ilinifanya niwe "injinia wa kuigwa." Pumzika salama mwalimu
Jf members bana

Ehe,alipojiunga usalama aliwambieni

Ova
 
Si suala la kuna nini Muhimbili. Kuna masikini wengi pale wanakufa kila siku tena kwa kukosa pesa ya kujitibu. Hufuatilii kwa sababu wao siyo maarufu.
Umeugusa moyo wangu.

Umenena ukweli mchungu
 
RIP Mwalimu Kusila.

Mtu huyu alinifundisha Physics Tabora School kabla hajaingia Usalama wa Taifa na baadaye kuwa mwanasiasa. Alikuwa anaijua Physics ndani na nje utadhani unafundishwa na Newton, Wheatstone, Ohm, Faraday, au Maxwell mwenyewe. Nelkon alikuwa hamfikii ingawa tulikuwa tunatumia vitabu vya Nelkon, Kusila alikuwa anaweza kusema kuwa Nelkon alikosea kidogo na ukilinganisha na Abott ndipo unaona wapi Kusila alikuwa sahihi kuliko Nelkon.

Physics aliyonifundisha ilinifanya niwe "injinia wa kuigwa." Pumzika salama mwalimu
Japo Mimi siyo engineer ila ukitaja majina kama Newton Mwili unanisisimka. Mathematical Principal of Natural Philosophy ilibeba transformative thinking. Kabla yake, Revolutionary of heavenly spheres ya Nick Copernicus, akamuambukiza Johannes Kepler na mwishowe Bwana Newton.

RIP Mwalimu uliyemzidi Nelkon!!
 
Back
Top Bottom