William Ruto anapitia kipindi kigumu sana

Daby

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2014
Posts
33,894
Reaction score
76,810
Nadhani anaenda kuwa rais wa Kenya aliyepitia kipindi kigumu saana. Kwanza amechukua nchi kipindi ambacho Dunia nzima inapitia changamoto ya mfumuko wa bei.

Lingine, Raila alishajua anaenda kushinda...Mara vuuupu akaukosa urais. Hasira aliyonayo haielezeki.

Deni nalo linamwandama. Inabidi acheze karata zake vizuri la sivyo nchi inatapakaa.

Tusubiri maandamano ya week inayokuja maana mmoja kajizatiti hakuna maandamano mwingine kashikilia lazima waandamane.
 
Ruto alipania sana Urais.

Akaahidi kila kitu.


Utekelezaji sifuri.



Ingawa waandamanaji wengi ni wajaluo.


Lakini hoja zao zinalata nguvu kutokana na ahadi za uwongo wa kupindukia alizotoa Ruto wakati wa kampeni pamoja lundo la vyeo vya fadhila alivyogawa.
 
Shida ya Ruto ana taka kula peke yake. Wakati awamu zote hula na Raila. Hata wakati wa Mwai Kibaki , Ruto akiwa timu moja na Raila wali kula wote. Hivyo hivyo kwa awamu ya Uhuru. Ila zamu yake, yeye anataka ale mkate wote peke yake. Ngoja akione cha moto na Uroho wake.
 
Jamaa nae alimsumbua sana Kenyatta, afu alikuwa na jeuri balaa
 
Ni ka mwaka tu kamekata.....huwezi ukategemea uchumi wa nchi ujengwe kwa miezi 10.

Dunia inapitia changamoto hii kwasasa.....Aliahidi ahadi ambazo kila mwanasiasa anaweza kuahidi.
 
Ni ka mwaka tu kamekata.....huwezi ukategemea uchumi wa nchi ujengwe kwa miezi 10.

Dunia inapitia changamoto hii kwasasa.....Aliahidi ahadi ambazo kila mwanasiasa anaweza kuahidi.
Apambane sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…