Pre GE2025 Willibrod Slaa: Anachopigania Tundu Lissu ni kuisafisha CHADEMA

Pre GE2025 Willibrod Slaa: Anachopigania Tundu Lissu ni kuisafisha CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt. Willibrod Peter Slaa akizungumza hivi karibuni kupitia jukwaa la Kumekucha la mtandao wa Clubhouse.
IMG_2019.jpeg

"Mimi kwa maoni yangu Tundu Lissu (Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo- CHADEMA bara) anachopigania ni kukisaficha chama (CHADEMA) na kukipeleka kwenye hatua ya mbele na ndiyo maana ametoa sera yake na ilani yake ya uchaguzi, kwasababu alichotangaza ni kwanini ametaka kuingia kwenye uongozi (Kugombea uenyekiti wa CHADEMA taifa) na akipata uongozi anaogombea atafanya nini.

Ninadhani aliorodhesha dosari kadhaa ndani ya chama ikiwa ni pamoja na uwezekano wa rushwa ndani ya chama, rushwa ndani ya chaguzi za chama, yeye akaeleza kwamba akichaguliwa atafanyia kazi hayo mambo.

Ikumbukwe kwenye katiba ya CHADEMA ya sasa, haizungumzii majukumu ya Makamu Mwenyekiti, haimpi nafasi ukiachana na wajibu wa Makamu Mwenyekiti kama Mwenyekiti wa maadili pale ambapo jambo linapelekwa kwake, haimpi hiyo nafasi yoyote ya kurekebisha jambo lolote isipokuwa lile lililokabdhiwa kwake na Mwenyekiti au lalamiko lililopelekwa kwake na Ofisi ya Katibu Mkuu wa Chama ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa Chama.

Kwahiyo yeye Lissu anatumia mambo hayo kama nyenzo ya kampeni yake kwamba nikiingia kwenye uongozi haya ndiyo nitakayoyafanya kuimarisha chama chetu.

Sasa masuala ya kama yameshatokea mazingira ya rushwa ndani ya CHADEMA, ninadhani Lissu ameyaweka wazi"
 
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt. Willibrod Peter Slaa akizungumza hivi karibuni kupitia jukwaa la Kumekucha la mtandao wa Clubhouse.
View attachment 3185396
"Mimi kwa maoni yangu Tundu Lissu (Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo- CHADEMA bara) anachopigania ni kukisaficha chama (CHADEMA) na kukipeleka kwenye hatua ya mbele na ndiyo maana ametoa sera yake na ilani yake ya uchaguzi, kwasababu alichotangaza ni kwanini ametaka kuingia kwenye uongozi (Kugombea uenyekiti wa CHADEMA taifa) na akipata uongozi anaogombea atafanya nini.

Ninadhani aliorodhesha dosari kadhaa ndani ya chama ikiwa ni pamoja na uwezekano wa rushwa ndani ya chama, rushwa ndani ya chaguzi za chama, yeye akaeleza kwamba akichaguliwa atafanyia kazi hayo mambo.

Ikumbukwe kwenye katiba ya CHADEMA ya sasa, haizungumzii majukumu ya Makamu Mwenyekiti, haimpi nafasi ukiachana na wajibu wa Makamu Mwenyekiti kama Mwenyekiti wa maadili pale ambapo jambo linapelekwa kwake, haimpi hiyo nafasi yoyote ya kurekebisha jambo lolote isipokuwa lile lililokabdhiwa kwake na Mwenyekiti au lalamiko lililopelekwa kwake na Ofisi ya Katibu Mkuu wa Chama ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa Chama.

Kwahiyo yeye Lissu anatumia mambo hayo kama nyenzo ya kampeni yake kwamba nikiingia kwenye uongozi haya ndiyo nitakayoyafanya kuimarisha chama chetu.

Sasa masuala ya kama yameshatokea mazingira ya rushwa ndani ya CHADEMA, ninadhani Lissu ameyaweka wazi"
Lissu asubiri siku ya kupiga kura!
Atakosa bara na pwani
 
Lissu hana bei..

Angekuwa ana bei angekuwa ameshanyamaza siku nyingi na yeye ale asali..

Ana nia ya dhati ya kukisafisha chama..

Dua kwake
Hata Mbowe alikuwa hanunuliki, ccm wana namna yao ya kuwapata hawa jamaa. Ingekuwa rahisi wangeshatoka madarakani mda sana.

Kwa hivi ninavyoona, ccm inaweza kuonhoza nchi kwa karne moja.
 
Kuna kitu kimoja kinashangaza.., baada ya LISSU kupishana na mwenyekiti wake simuoni Erythrocyte, kaacha kuanzisha nyuzi zake za kumsifia Mbowe hata kuchangia, sijui hajui aende kwa LISSU au Mbowe, bora karatasi ya mshahara(,salali silipu),ameshaonyesha upande gani anaukubali.
Huyo jamaa ni chawa asietumia akili hata kisoda, kwasasa atakuwa analilia chooni.
 
Huyu slaa aliyepewa cheo na mwendazake baada ya kukisaliti chama ktk wakati mgumu wa kuelekea ktk uchaguzi mkuu na kwenda Canada kula Bata ndiye wa kuamini kweli hacheni miZaa bwana
 
Back
Top Bottom