wimbo bora wa injili kwa mwaka 2009

wimbo bora wa injili kwa mwaka 2009

Wimbo wa WARAKA wa Bahati Bukuku ni bomba ile mbaya. hata mimi naufagilia ile mbaya. Nilijitahidi kutuma namba yake 130 messages 100 ili ashinde.
 
Naomba nikusahihishe kidogo nafasi ya pili ilishikwa na Solomon Mukubwa na wimbo wake wa MFALME WA AMANI.

Nawapa hongera waimbaji wote walioshiriki.

Wimbo Nibebe wa Rose Muhando umechaguliwa na watanzania kuwa Wimbo bora wa Injili kwa mwaka 2009. Wimbo huu umeshika namba 1 baada ya kuzipiku nyimbo 30 zilizotolewa na TBC1 kama zawadi ya x-mass. kwa kushindanishwa kwa siku tatu kuanzia tarehe 25 - 27 Desemba, 2009.

Wimbo wa Nibebe umepigiwa kura zaidi ya 7000 na kushika nafasi ya kwanza ukifuatiwa na wimbo wa Bwana Yesu ni tegemeo langu na Wimbo wa tatu ni Waraka wa Bahati Bukuku uliopata kura 6000. Washindi wamejipatia vikombe pamoja na pesa taslimu Tshs 50,000 kwa mshindi wa tatu; Tshs 100,000 kwa mshindi wa pili na Tshs 200,000 kwa mshindi wa kwanza.

Hongera TBC1 kwa kipindi kizuri na hongereni waimbaji wote maana nyimbo zenu hakika ni nzuri na mchuano ulikuwa ni mkali sana kiasi kwamba ilikuwa vigumu kutabiri mshindi.
Nahisi huu ni mgongano wa mawazo!
 
Jamani mbona zawadi zenyewe kiduuunchuuu!!! Laki mbili mwimbaji bora wa mwaka, heh! Wangewaambia Cocacola, etc etc wawasaidie, wangepata zawadi zaidi mbona?
Wimbo wa Nibebe kelele tu, na sijui watu wanaupendea nini?

TBC wamefanya ufisadi

em angalia zile short codes haiwezi kuwa chini ya 250 per msg

sasa mshindi wa kwanza kapata kura 7000, wapili 6000....sasa walikua

washiriki 30. em weka roughly hapo assume wote waliosalia wastani wa

kura ni 1000(which is minimum expected) alafu zidisha mara 28= 28000 +

7000 +6000=41000 * 250=10,250,000

toa tsh50 * 41000=2,050,000-malipo kwe kampuni ya simu = 8,200,000

alafu wanakuja kutoa laki tano tu kwa washindi. hapo ni gharama ya chini kabisa, kwanza ur not sure kama kweli walipata exactly figure kama walivyoainisha et 7000,6000..nk, any way katika ulimwengu wa roho pesa haimati sana, bali recognition and appreciation.
 
kwani AIC ni ya kikabila????


Aaah, hapanaaaa, ilaaaa, siyo nakuwa mkabila, ila wasukuma wanaipenda sana ile kwaya. Nasikia misa za AIC zinaweza kuendeshwa kilugha chao wakaelewa woooteee. Ni swali tu, ila laweza lisijibiwe.
Ila ule wimbo wao kidogo umekaa ndivyo sivyo, mwanzoni wako too physical.
 
TBC wamefanya ufisadi

em angalia zile short codes haiwezi kuwa chini ya 250 per msg

sasa mshindi wa kwanza kapata kura 7000, wapili 6000....sasa walikua

washiriki 30. em weka roughly hapo assume wote waliosalia wastani wa

kura ni 1000(which is minimum expected) alafu zidisha mara 28= 28000 +

7000 +6000=41000 * 250=10,250,000

toa tsh50 * 41000=2,050,000-malipo kwe kampuni ya simu = 8,200,000

alafu wanakuja kutoa laki tano tu kwa washindi. hapo ni gharama ya chini kabisa, kwanza ur not sure kama kweli walipata exactly figure kama walivyoainisha et 7000,6000..nk, any way katika ulimwengu wa roho pesa haimati sana, bali recognition and appreciation.



Kama wameandaa mashindano hayo bure sawa wangeweza kuwapa washindi hela zaidi, ila usisahau kuna airtime yao maana wamerusha kwa siku kadhaa na masaa mengi. Mi nadhani wangetafuta sponsor tu anayeendana na maudhui hayo (ofcourse sio Mfalme Chui) wangepata mihela kibao.
 
Umechaguliwa kwa sababu unaimbwa mpaka kwenye vilabu vya gongo, komoni, wanzuki na kwingineko unakojua wanaimba huku wamelewa na hawaelewi wanacho imba, mimi ningechagua sitanyamaza, wa Huyo Rose,
 
Umechaguliwa kwa sababu unaimbwa mpaka kwenye vilabu vya gongo, komoni, wanzuki na kwingineko unakojua wanaimba huku wamelewa na hawaelewi wanacho imba, mimi ningechagua sitanyamaza, wa Huyo Rose,

huo wa sitanyamaza ndio wimbo wetu wa kuingilia pale CHAWOTE!😀
 
Wimbo wa Nibebe kelele tu, na sijui watu wanaupendea nini?


Mmmhh!!! Wimbo wa Nibebe wa Rose Mhando kwangu mimi ni kati ya nyimbo bora kabisa za dini kuwahi kuzisikiliza toka nifike nnji hii!!

Una touch za hatari!!
 
TBC wamefanya ufisadi

em angalia zile short codes haiwezi kuwa chini ya 250 per msg

sasa mshindi wa kwanza kapata kura 7000, wapili 6000....sasa walikua

washiriki 30. em weka roughly hapo assume wote waliosalia wastani wa

kura ni 1000(which is minimum expected) alafu zidisha mara 28= 28000 +

7000 +6000=41000 * 250=10,250,000

toa tsh50 * 41000=2,050,000-malipo kwe kampuni ya simu = 8,200,000

alafu wanakuja kutoa laki tano tu kwa washindi. hapo ni gharama ya chini kabisa, kwanza ur not sure kama kweli walipata exactly figure kama walivyoainisha et 7000,6000..nk, any way katika ulimwengu wa roho pesa haimati sana, bali recognition and appreciation.


Mkuu unasahau kuwa hii ni dunia ya kibepari ambayo inaongozwa na faida (hata ikibidi kutogharamia chochote) tuwashukuru TBC1 kwa kutuburudisha na kuwazawadia zawadi 'nono' waimbaji wetu ambayo probably hawakuitarajia!!

Mpaka wanamuziki wetu watakapozinduka, wadosi watakuwa tayari mabilionea!!
 
Nahisi kama washindi walipangwa au julikana kabla.

Kuthibitisha hili, ni wale wapokeaji wa zawadi kwa niaba ya washindi, walikua wamekaa kwa mtindo maalumu au makusudi toka mwanzo na haikua coincidence at all.

That is;mshindi wa kike apewe zawadi na mwakilishi wa kike and vise versa.
 
Mi naukubali ule wimbo wa marehemu chibalonza...Toka chini kwenda juu...

http://www.youtube.com/watch?v=meixmZOZi0o tumempoteza mmoja wa waimbaji

wazuri ambao hawajawahi tokea.....lakini si mbaya sana kwa sababu yule alieshika

namba mbili(SOLOMON MUKUBWA) ndie alienusurika kwenye ile ajali iliyomuua angela(ndipo alipopoteza ule mkono mmoja)
hakuna lisilowezekana kwa mungu.....RIP angel chibalonza
Jana (27Dec09) asubuhi niliangalia kipindi cha Jambo cha TBC1. Solomon Mukubwa alihojiwa na TBC1. Kati ya maswali aliyoulizwa ni kuhusu ulemavu wa mkono wake. Akasema aliumwa sana mkono (ulivimba) na alihusisha ugonjwa huo na nguvu za giza. According to him - madaktari walishindwa na hata waganga wa jadi hawakuweza. Ndipo aliporudi tena hospitali akaambiwa inabidi akatwe mkono. Hakuwa na jinsi bali kukubali. Mkono ukakatwa, and there he is! Happily serving the living God. (Nimejaribu kufupisha).

Katika mahojiano hayo hakutaja lolote lililohusisha ulemavu wake na ajali iliyomuua Angela. Labda kama aliruka sehemu ya hiyo habari maana alikuwa anasisitiza mara kwa mara kwamba anaeleza kwa kifupi tu.
Wenye uhakika watuondoe doubts.
Naomba kuwasilisha.
 
Mi naukubali ule wimbo wa marehemu chibalonza...Toka chini kwenda juu...

http://www.youtube.com/watch?v=meixmZOZi0o tumempoteza mmoja wa waimbaji

wazuri ambao hawajawahi tokea.....lakini si mbaya sana kwa sababu yule alieshika

namba mbili(SOLOMON MUKUBWA) ndie alienusurika kwenye ile ajali iliyomuua angela(ndipo alipopoteza ule mkono mmoja)

hakuna lisilowezekana kwa mungu.....RIP angel chibalonza

Kumbeeeeeeeeeee,sikujua hilo.Jina la bwana libarikiwe.
 
Umechaguliwa kwa sababu unaimbwa mpaka kwenye vilabu vya gongo, komoni, wanzuki na kwingineko unakojua wanaimba huku wamelewa na hawaelewi wanacho imba, mimi ningechagua sitanyamaza, wa Huyo Rose,


Lazima mkubali kuwa rose muhando hana nyimbo yeyote mbaya.....angeamua kuingiza nyimbo yeyote ingeshinda alafu watu wangelalamika kuwa ameshinda nafasi mbili au tatu!

Lazima tukubali kuwa rose muhando is the best gospel artist of all the time....wanaosema kuwa nyimbo zake zinaimbwa na walevi wanasahAu kuwa hata yesu walimsema kuwa alikuwa anakula na watoza ushuru na malaya....anasema alikuja iili watu wote wapate wokovu ...wote wawe na uzima tena wawe nao tele.....sasa nilidhani wanaompinga rose wangemshukuru kwa kufuata maandiko amefanya hadi walevi ,wapagani na wasiokuwa wakristo walisifu jina kuu kuliko yote ...jina la yesu!....si kazi rahisi ...msimpinge ..mpeni sifa zake stahili na yeye anasema kuwa sifa na utukufu ziende kwa bwana! Mnataka nini zaidi!


Hongera rose muhando!!!!!!!
 
hahahha.Binamu bwana.Ntakupa na dhawadi ya new year,Kumbe unanikumbukaga eee?
aseeee, we acha!,
ujue wapwaaazzzz wako kichwani sana, sema WIFI yako ananibana sanaa, nakua nawamisi wapwazzz na mabinanamuzzzz.
vipi za MOSHI??
 
Quote:


Mi naukubali ule wimbo wa marehemu chibalonza...Toka chini kwenda juu...

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=meixmZOZi0o"]http://www.youtube.com/watch?v=meixmZOZi0o[/ame] tumempoteza mmoja wa waimbaji

wazuri ambao hawajawahi tokea.....lakini si mbaya sana kwa sababu yule alieshika

namba mbili(SOLOMON MUKUBWA) ndie alienusurika kwenye ile ajali iliyomuua angela(ndipo alipopoteza ule mkono mmoja)
hakuna lisilowezekana kwa mungu.....RIP angel chibalonza

Quote:


Mi naukubali ule wimbo wa marehemu chibalonza...Toka chini kwenda juu...

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=meixmZOZi0o"]http://www.youtube.com/watch?v=meixmZOZi0o[/ame] tumempoteza mmoja wa waimbaji

wazuri ambao hawajawahi tokea.....lakini si mbaya sana kwa sababu yule alieshika

namba mbili(SOLOMON MUKUBWA) ndie alienusurika kwenye ile ajali iliyomuua angela(ndipo alipopoteza ule mkono mmoja)
hakuna lisilowezekana kwa mungu.....RIP angel chibalonza


Mi naukubali ule wimbo wa marehemu chibalonza...Toka chini kwenda juu...

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=meixmZOZi0o"]http://www.youtube.com/watch?v=meixmZOZi0o[/ame] tumempoteza mmoja wa waimbaji

wazuri ambao hawajawahi tokea.....lakini si mbaya sana kwa sababu yule alieshika

namba mbili(SOLOMON MUKUBWA) ndie alienusurika kwenye ile ajali iliyomuua angela(ndipo alipopoteza ule mkono mmoja)
hakuna lisilowezekana kwa mungu.....RIP angel chibalonza




Jana (27Dec09) asubuhi niliangalia kipindi cha Jambo cha TBC1. Solomon Mukubwa alihojiwa na TBC1. Kati ya maswali aliyoulizwa ni kuhusu ulemavu wa mkono wake. Akasema aliumwa sana mkono (ulivimba) na alihusisha ugonjwa huo na nguvu za giza. According to him - madaktari walishindwa na hata waganga wa jadi hawakuweza. Ndipo aliporudi tena hospitali akaambiwa inabidi akatwe mkono. Hakuwa na jinsi bali kukubali. Mkono ukakatwa, and there he is! Happily serving the living God. (Nimejaribu kufupisha).

Katika mahojiano hayo hakutaja lolote lililohusisha ulemavu wake na ajali iliyomuua Angela. Labda kama aliruka sehemu ya hiyo habari maana alikuwa anasisitiza mara kwa mara kwamba anaeleza kwa kifupi tu.
Wenye uhakika watuondoe doubts.
Naomba kuwasilisha.


mkanganyiko mwingine huo...
 
watuletee na ile mingoma yetu ya kiislamu nasi tushindane tupate mihela kama wao mbvona mnapendelea hivo?.....tehe....teeeee
 
Back
Top Bottom