Wimbo mpya wa Young Killer, jumba bovu anaangushiwa Harmonize

utakuta hawa hawa ndio wanamponda mavoko amepotea kwenda WCB leo wanamuona bora kuliko harmonize dah binadamu wabaya sana!!
 
unatumia neon "Nyimbo" zikiwa nyingi na "wimbo" ukiwa ni mmoja. Huwezi kuwa na "nyimbo mpya ya..." maneno sahihi ni "wimbo mpya wa..."
 
hapo kwenye the most subscribed artist muda si mrefu rayvanny atampita mmakonde, ukweli ni kwamba harmonize ameanza kabla ya rayvanny na ana ngoma nyingi kuliko rayvanny lakini wanakimbizana, kama unakumbuka wakati harmonize ametoa niambie na rayvanny akatoa mbeleko, mbeleko ilikuwa inaongoza kwenye mauzo wasafi.com. hata kuhusu views angalia nyimbo zao za mwisho na muda walioweka au angalia idadi ya likes na dislikes walizopata kila mmoja utagundua rayvanny kwa sasa yupo juu kuliko harmonize!!
 
Kuanza kwa maana ipi .......... Maana kama wewe ni mfuatiliaji basi utajua kuwa Rayvanny alianza zamani sana tokea Tip Top ya Madee. Tena "inawezekana" Rayvanny na Mond Rayvanny wa siku nyingi.
 
Haters gonna hate, wimbo uko poa, video classy
 
rayvanny anajua sana ila yule anayemtengenezeaga biti sijui wanamuita laizer ndio atamfelisha jamaa, anamtengenezea biti kama za ya moto band bana!!
Huyo jamaa ndio aliyetengeneza wimbo unayoongoza kwa mauzo East Africa, na ndio iliyoongoza kwa kutazamwa na watu wengi sana kule Youtube,wimbo Salome.
 
Halafu wewe mkuu hujui kitu,wenzako wanalinganisha na kazi zake za mwanzo ndio unasema kitu kama hiki, je umefananisha na wimbo wake upi wa Young Killer ambao ulifanya vizuri zaidi ya huu ......... Wimbo wake upi ulipata views 100,000 ndani ya saa 18 ????
 
Me naona kwa pale wasafidotcom harmonize ndo anaongoza kwa mauzo
 
Halafu hii saga ya [emoji107] nyingi naona ikitrend sana huko tube. Watu wana visa wanakaa attention wakiona wimbo umetoka wanaweka dislike
 
Pambaneni na Khali zenu..... Mwenzenu kutengeneza mpaka watu mnamzumgumzia..
 
Naona vijana wangu wameona ngumu nyeusi hazilipi wamekimbilia kwenye biashara rasmi,Msodoki anaonyesha atakaa kwenye ramani kwa muda mrefu sana akikaza hii ngoma iko poa kila kitu na kuhusu Harmonize nadhani watu wamzoee kua ni nusu ya diamond.
 
Halafu hii saga ya [emoji107] nyingi naona ikitrend sana huko tube. Watu wana visa wanakaa attention wakiona wimbo umetoka wanaweka dislike

Kuna vita ya kibwege mashabiki wanaiendesha wapo ambao bila hata kuiangalia video anashusha kitu cha [emoji1532]
 
Hamjagundua tu huu uzi umeanzishwa ili kutafuta viewers wa hiyo ngoma mpya...

Hongera mleta uzi
 
"....na kusema kuwa harmonize amezidi kumuiga sana boss wake mpaka imekuwa kero kwani wanashindwa kutofautisha sauti za watu hao wawili"

HII ISHU INAMUUMIZA KICHWA HADI LEO RAJJ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…